Dar: Omary, Juma, Amos, Mokolo wakamatwa kwa wizi wa nyaya za TANESCO

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Jeshi la Polisi limewakamata watu wanne (4) kwa tuhuma za kujaribu kuhujumu miundombinu ya Shirika la Umeme Tanesco ikiwemo Nyaya aina ya Copper kwa lengo la kuziuza.

Watuhumiwa hao; ni OMARY ALLY, miaka 28, Mkazi wa Tegeta na mwenzake JUMA SULLEIMAN, Miaka 30, Mrangi, mkazi wa Wazo na wanunuzi wa vifaa hivyo ni AMOS JOHN, miaka 30, mkazi wa Tegeta na MOKOLO MACHAGE, miaka 26, mkazi wa Bunju walikamatwa tarehe 10/04/2022.

Watuhumiwa wote hawa wamehojiwa kwa kina na kukiri kuhusika katika matukio ya namna hiyo. Baada ya kupekuliwa maeneo yao walikutwa na viroba vinne vya Nyaya za Copper zilizochunwa.

Jeshi la Polisi linaendelea kutoa onyo kali kuwa halitamvumilia mtu au kikundi chochote kinachojihusisha kwa namna yoyote ile kujaribu kuharibu miundombinu ambayo imejengwa kwa manufaa ya umma na atakayejaribu atakamatwa na mifumo ya kumfikisha kwenye vyombo vya sheria itazingatiwa.

Muliro J. MULIRO – ACP
KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAM.
 
Jeshi la Polisi limewakamata watu wanne (4) kwa tuhuma za kujaribu kuhujumu miundombinu ya Shirika la Umeme Tanesco ikiwemo Nyaya aina ya Copper kwa lengo la kuziuza.

Watuhumiwa hao; ni OMARY ALLY, miaka 28, Mkazi wa Tegeta na mwenzake JUMA SULLEIMAN, Miaka 30, Mrangi, mkazi wa Wazo na wanunuzi wa vifaa hivyo ni AMOS JOHN, miaka 30, mkazi wa Tegeta na MOKOLO MACHAGE, miaka 26, mkazi wa Bunju walikamatwa tarehe 10/04/2022.

Watuhumiwa wote hawa wamehojiwa kwa kina na kukiri kuhusika katika matukio ya namna hiyo. Baada ya kupekuliwa maeneo yao walikutwa na viroba vinne vya Nyaya za Copper zilizochunwa.

Jeshi la Polisi linaendelea kutoa onyo kali kuwa halitamvumilia mtu au kikundi chochote kinachojihusisha kwa namna yoyote ile kujaribu kuharibu miundombinu ambayo imejengwa kwa manufaa ya umma na atakayejaribu atakamatwa na mifumo ya kumfikisha kwenye vyombo vya sheria itazingatiwa.

Muliro J. MULIRO – ACP
KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAM.
Ukiacha huyo Mrangi, hao watuhumiwa wengine hawana makabila?
 
Kichwa kilifaa angalau kisomeke:

"Dar: Wanne wakamatwa kwa tuhuma za kuhujumu miundo mbinu ya TANESCO".
Badala ya kutuandikia majina yao katika heading.
 
Upumbavu wa hali ya juu ,hawa ni suspects na bado hawajapelekwa mahakamani why ututajie majina yao?suspects wanatambuliwa wanapokua wameshasimama mahakamani, matokeo ya pithole country.
 
Huku Mzanzi Afrika waiba Nyaya za Copper wanaitwa Izinyoka,Ukikamatwa nazo hizo copper unafia Jela bora hata ukavunje na uibe Kituo cha Polisi utasalimika siyo hizo Nyaya.
 
Upumbavu wa hali ya juu ,hawa ni suspects na bado hawajapelekwa mahakamani why ututajie majina yao?suspects wanatambuliwa wanapokua wameshasimama mahakamani, matokeo ya pithole country.
Mkuu ulisikia mahakama gani mtuhumiwa akitiwa hatiani akaitwa kwa cheo chake mf: mwizi akaitwa "mwizi?

Pale baada ya kutiwa hatiani hubadilika toka mtuhumiwa na kuitwa mfungwa na si mwizi!

Mhalifu nchi hii anabembelezwa na kunyenyekewa sana kuliko mtu anavyobeba kwa unyenyekevu tray la mayai.
 
Back
Top Bottom