Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,267
- 33,870
Awe ni Daudi Albert Bashite ama ni Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaa ndiyo anayeendesha jiji la Dar es salaam na kila kinachofanywa na UKAWA kinavurugwa na Mkuu huyo wa Mkoa.
Inaonekana kama vile UKAWA wamepoteana ama wamekubali yaishe kwani watumishi wa Halmashauri zinazoongozwa na UKAWA wanamsikiliza zaidi Makonda kuliko wanavyowasikiliza mameya wa UKAWA.
Makonda anapanga na kutekeleza mambo mbali mbali na UKAWA hawasikiki kabisa wao ni nini wanafanya Dar. Enzi za Kitwana Kondo na Didas Masaburi (wote marehemu) ilikuwa inajulikana kuna Meya kwa kuwa wakuu wa Mkoa waliokuwepo waliwapa nafasi ya kufanya kazi zao. Isaya Mwita ni kama amefichwa na Makonda.
Jee ni nini kimewasibu UKAWA walioaminiwa na wana Mzizima hata kumwachia Makonda aseme na kufanya atakalo kwenye Halmashauri zao wao wakiwa kimya. Ni rahisi kwa Makonda kuzuia mambo ya UKAWA kuliko UKAWA kukataa mambo ya Makonda!
Inaonekana kama vile UKAWA wamepoteana ama wamekubali yaishe kwani watumishi wa Halmashauri zinazoongozwa na UKAWA wanamsikiliza zaidi Makonda kuliko wanavyowasikiliza mameya wa UKAWA.
Makonda anapanga na kutekeleza mambo mbali mbali na UKAWA hawasikiki kabisa wao ni nini wanafanya Dar. Enzi za Kitwana Kondo na Didas Masaburi (wote marehemu) ilikuwa inajulikana kuna Meya kwa kuwa wakuu wa Mkoa waliokuwepo waliwapa nafasi ya kufanya kazi zao. Isaya Mwita ni kama amefichwa na Makonda.
Jee ni nini kimewasibu UKAWA walioaminiwa na wana Mzizima hata kumwachia Makonda aseme na kufanya atakalo kwenye Halmashauri zao wao wakiwa kimya. Ni rahisi kwa Makonda kuzuia mambo ya UKAWA kuliko UKAWA kukataa mambo ya Makonda!