Uzalendo ndio huu, Dar-New York kwa B787-8 gharama ya mafuta ni TZS 267M

🚮🚮🚮🚮 Mnaomchafua mnatumia nguvu kiasi gani?
Tunaomchafua kina nani? kwanza sijawahi kumchafua nimekuwa nasema zuri na kama kuna baya nadhani nasema. Ukiwa kiongozi ni lazima ukubali kukosolewa na kusifiwa pia yote kubali. point yangu kutoka UN kunahitaji mapokezi?
 
Siku mkiacha kumkosoa tutakaa kimya,

Kwanini usiwaambie wanaomdhalilisha waache?
Mimi sijawahi kumkosoa Samia, nipo upande wake since day one na sitobadilika!! Wanaomdhalilisha hawatokosekana, hata afanye nini!! Watu walimtundika Yesu msalabani uchi wa mnyama sembuse yeye Samia kutukanwa? Kama hutaki matusi na kudhalilishwa then usiingie kwenye siasa za ushindani, waliomwambia Lowassa kajinyea leo ni washkaji zake wakubwa, ndiyo siasa hizo jombaa!! Kinachokera ni uchawa uliopitiliza...and sidhani kama Mama anapenda machawa!! Leo naona Diamond kaachia brand new Song ya kumsifia karudisha demokrasia na uhuru wa habari!! Kwani havikuwepo hivyo vitu?
 
Wanazengo mnafahamu ni kwanini Rais Samia aliamua kupanda ndege ya Emirates na kuacha ndege 11 mpya zimepaki?!
_________________________________

Kutoka Dar es salaam kwenda New York Marekani ni Jumla ya Km 12,050 sawa na jumla ya Km 24,100 two ways,ikiwa ni sawa na safari ya masaa 21 na dk 31 Mchana na Usiku nani sawa na masaa 43 kwenda na kurudi,

Boing 787-8 engine inatumia lita 5,400 za mafuta kwa lisaa limoja yaani ( 5,400L/h )

Fanya hivi, chukua lita 5,400 za mafuta zidisha kwa masaa 21.31 utapata jumla ya Lita 115,074 za mafuta ili kufika New York Marekani yaani ( one way)

Tunafahamu,bei ya Lita moja ya mafuta ya ndege (Jet fuel) hapa Tanzania kama trh 24|09|2021 ni $0.501/lita sawa na Tshs 1,162

Ilikupata gharama ya mafuta Dar es salaam to New York ,Chukua lita hizi 115,074 zidisha kwa bei ya lita moja ambayo ni Tsh 1,162 utapata jumla ya Tshs 133,653,240 kwa Safari moja tu ( One way)

Ilikupata gharama ya safari zote mbili yaani kwenda New York na kurudi,Zidisha gharama ya mafuta ya kwenda Tshs 133,653,240 X 2 ilikupata gharama halisi ya mafuta ya Dar es Salaam to New York two ways ,Utapata Jumla ya Tsh267,306,480 hii ni pesa ya mafuta tu yakwenda New York na kurudi Dar es salaam,

Hapa hatujazungumzia rate ya landing fees, Parking fees nanyinginezo watu wa aviation wanafahamu hizi gharama vizuri, kwakuwa Mimi si mtaalum wa mambo Aviation naomba niishie hapa kwenye mathematical calculation ya gharama ya mafuta tu ambayo ni karibu 270M,

Sasa mnaolalamika Rais katumia gharama kubwa sikieni hii,Emirates gharama ya Mtu mmoja kwenda New York na kurudi Dar es salaam kwa Economy Class ni Tsh 2,854,500 kama utakaa huko chini ya Siku 7 ,

Sasa tufanye mama ameenda na watu|deligates 50 japo naamini ameenda na chini ya hawa,
Chukua 2,854,500 7X 50 Utapata jumla ya Tshs 142,725,000 ,

Chukua gharama ya mafuta ya Boing 787-8 ya kwenda New York na kurudi Dar es salaam ambayo ni Tshs 267,306,240 toa 142,725.000 ambayo ni nauli ya watu 50 utapata Salio la Tshs 124,581,240,

Rais Samia anajua umasikini wa watu wake, anajua hakuna madawa, anajua barabara mbovu, anajua watu wanamaisha magumu ndio maana anasafiri na Emirates pamoja na kwamba Tanzania tunazo ndege mpya 11,

Mnaotaka rais aende na dreamliner New York rudieni kusoma uchambuzi huu, Mnaosema rais anatumia gharama kubwa kwenda New York angalieni hii nia ya Rais katika kukwepa gharama zisizo za lazima,

NB, Kitendo cha Rais Samia kwenda na usafiri wa umma amepunguza gharama ya Safari kwa 40% na kwahaki nchi ilimsubiri kiongozi wa aina hii kwa muda mrefu,

_________________________________


View attachment 1952267
Na kama kuna wanaona asingeenda kabisa kuokoa fedha ya umma tupigie hesabu kama kuna hasara gani maana tumeona marais kibao wakishiriki kwa mtandao. Huko kama kawaida ni domo tu.
 
Kaogopa kupanda la kunyumba ,lingeweza 'kuzima' angani na kupelekea kurest in Hell kama yule Hayati..tusimlaumu saa nyingine tuangalie tumetoka wapi?

Tulipigwa!
 
Mimi sijawahi kumkosoa Samia, nipo upande wake since day one na sitobadilika!! Wanaomdhalilisha hawatokosekana, hata afanye nini!! Watu walimtundika Yesu msalabani uchi wa mnyama sembuse yeye Samia kutukanwa? Kama hutaki matusi na kudhalilishwa then usiingie kwenye siasa za ushindani, waliomwambia Lowassa kajinyea leo ni washkaji zake wakubwa, ndiyo siasa hizo jombaa!! Kinachokera ni uchawa uliopitiliza...and sidhani kama Mama anapenda machawa!! Leo naona Diamond kaachia brand new Song ya kumsifia karudisha demokrasia na uhuru wa habari!! Kwani havikuwepo hivyo vitu?
Unataka Machadema yamdhalilishe sisi tukae kimya kwa lipi kwa mfano?

Wewe ni chama gani Mjomba unayezuia mama kutetewa mtandaoni?

Unajua siasa kweli wewe au unadhani mfumo ni ule wa 2020?

Hapa ni bandika bandua mpaka 2025 mjomba watajua hawajui Samia ndio habari yote ,

Kama vipi log off kama unamsapoti halafu unapinga wanaomsapoti huna maana,

Mimi natumia bando langu, natumia muda wangu,Simu yangu,

Nani chawa hapa kwa hoja yako,

Wewe unataka Mama achafuliwe kura 2025 tunapataje acha wakereketwa tujibu mapigo kwa namba ?
 
Kakosea kuacha kwenda na ndege yetu. Ningekuwa mimi ningetinga na dege letu. Yaani linatua Swiss au Uk, then linaunga. Mambo ya kundandia wakati sisi si nchi masikini ni kujiendekeza. So kwangu hiyo siyo sifa.
Daaah,

Mzee siutauza nchi kabisa,
 
mkuu mm ninamashaka.sina utaalam kabisa na mambo ya hayo ysnayoluka juu.

hivi lina injini kubwa kiasigani hadi kula mafuta lita 5400 kwa saa 1?
 
Kakosea kuacha kwenda na ndege yetu. Ningekuwa mimi ningetinga na dege letu. Yaani linatua Swiss au Uk, then linaunga. Mambo ya kundandia wakati sisi si nchi masikini ni kujiendekeza. So kwangu hiyo siyo sifa.
Ila vijana mawazo yenu hahaha
 
CCM NDIO CHAMA,

Asante mwandishi umemaliza utata,
Umewaonesha Watanzania Uzalendo wa mama Samia kwa namba,

Karibu nyumbani mama kesho nitakuwepo,
yote ni kweli mzee
Hapo sawa amewazima waliokuwa wanasema kaenda na Boeng ,heko Madam President
CCM NDIO CHAMA,

Asante mwandishi umemaliza utata,
Umewaonesha Watanzania Uzalendo wa mama Samia kwa namba,

Karibu nyumbani mama kesho nitakuwepo,
Nakubaliana,
 
Back
Top Bottom