Dar: Meli yenye magari 3,743 yawasili bandarini ikitokea Japan

Nchi ilipitia kipindi kigumu sana.
Mbaya zaidi, wananchi wakakubali kuwa manipulated...

Na tatizo zaidi, watu huwa hatutaki kutafuta ukweli kutoka kwenye vyanzo tofauti!! Tunasikiliza sana wanasiasa, bila kujali credibility ya kile ambacho kimesemwa!!
 
Mama Samia anaupiga mwingi sana. Hizi takwimu zimetolewa na Bank kuu ya Uganda na zinaonesha ni jinsi gani sasa tunafanya vizuri kiuchumi kwenye ukanda huu.

Ninachompendea huyu Mama pamoja na mafanikio yote hakuna majivuno Hakuna makelele ya kujisifu wala nini. Anapiga show kimya kimya.

Huyu Mama yupo vizuri hakika.
 
Raisi fulani aliyepita angepata wazo la kuwafungia wapinzani wa siasa wote humu ndani awapeleke Kisiwa cha Wagagagigikoko na nafasi bado ikabaki !

1628671430274.png
 
Bado sana, Meli kubwa ya container 5000 ndio ilifika mpaka ikaonyeshwa AZAM TV meli kubwa ya mizigo kutia nanga bandari ya Dsm. .



Huko Duniani kuna meli zinabeba container zaidi ya 20,000 kwa mara moja

Ku
Bado sana, Meli kubwa ya container 5000 ndio ilifika mpaka ikaonyeshwa AZAM TV meli kubwa ya mizigo kutia nanga bandari ya Dsm. .



Huko Duniani kuna meli zinabeba container zaidi ya 20,000 kwa mara moja

Kuna watu mkuu inabidi ujishushe ili uendane na akili zao.
 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Eric Hamissi amesema kuwa meli hiyo imeandika historia mpya kutokana na kubeba shehena kubwa ya magari.

"Leo ni siku nzuri sana katika historia ya TPA kwa kuweka rekodi mpya kwa kupokea meli kubwa na iliyobeba shehena kubwa zaidi kuja nchini. Hii haijawahi kutokea katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na kubwa zaidi meli hii imetoka moja kwa moja Japan kuja nchini bila kupitia bandari
1628671913642.png

Kwa hiyo ni uongo tunaambiwa hii meli haijaja Tanzania moja kwa moja toka Japan, kumbe imepitia Mombasa kwanza.

Kwa nini viongozi wanasema uongo siku zote?
 
Mama Samia anaupiga mwingi sana. Hizi takwimu zimetolewa na Bank kuu ya Uganda na zinaonesha ni jinsi gani sasa tunafanya vizuri kiuchumi kwenye ukanda huu.

Ninachompendea huyu Mama pamoja na mafanikio yote hakuna majivuno Hakuna makelele ya kujisifu wala nini. Anapiga show kimya kimya.

Huyu Mama yupo vizuri hakika.
Kwa hiyo kwa miezi 6 ya kubadili uongozi matokeo yake ndio haya.
 
View attachment 1887764

View attachment 1887765

Bandari ya Dar es Salaam imeendelea kuzivutia kampuni kubwa za usafirishaji duniani, baada ya meli kubwa ya kisasa ikiwa na shehena kubwa zaidi ya magari kuwahi kutia nanga bandarini hapo.

Meli hiyo ya TRANQUAIL ACE (IMO: 9561253) inayomilikiwa na Kampuni ya Mitsui ikitokea moja kwa moja nchini Japan, imetia nanga ikiwa na magari 3,743 ambayo ni mengi zaidi kuwahi kusafirishwa kuja nchini kwa mara moja.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Eric Hamissi amesema kuwa meli hiyo imeandika historia mpya kutokana na kubeba shehena kubwa ya magari.

Meli hiyo iliyotengenezwa mwaka 2009 ina urefu wa mita 199.9 na upana mita 32.2 kwenda chini, ambapo imetia nanga chini ya nahodha, Diardado Garate.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 10, 2021 katika Bandari ya Dar es Salaam, Hamissi amesema kuwa meli hiyo imetia nanga Agosti 9, 2021 na kuanza shughuli ya ushushaji ambao unatarajiwa kumalizika kesho jioni.

Meli kubwa kuwahi kutia nanga nchini na ailiyokuwa imebeba shehena kubwa ya magari ilitia nanga bandarini hapo mwaka 2018 ikiwa na magari 2600.

"Leo ni siku nzuri sana katika historia ya TPA kwa kuweka rekodi mpya kwa kupokea meli kubwa na iliyobeba shehena kubwa zaidi kuja nchini. Hii haijawahi kutokea katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na kubwa zaidi meli hii imetoka moja kwa moja Japan kuja nchini bila kupitia bandari nyingine.

View attachment 1887766

"Kwa hiyo ni jambo jema dunia inakafahamu kwamba, Tanzania tuna bandari bora na ya kisasa yenye uwezo wa kupokea meli zote na ikazihudumia kwa wakati,” amesema Hamissi na kuongeza: “Katika inayoendelea kushushwa, magari yatasafirishwa kwa njia ya barabara kwenda nchi jirani na mengine 798 yanabaki hapa nchini.

"Mtaona ni jinsi gani sasa nchi zetu za jirani zinazotuzunguuka zimeenza kutuamini, kati ya magari yaliyoingia asilimia 65 yanakwenda kwenye nchi hizo."

Meneja Kampuni ya Inchcape Shipping Services, John Massawe amesema meli hiyo ina uwezo wa kubeba magari 5,200 na kwamba imetumia siku 20 ikiwa safari hadi kuwasili.

"Tumekuwa tukihudumia kampuni ya magari kwa miaka zaidi ya 20, na hii ni meli ya kwanza hivyo tunatarajia huu ni mwanzo wa kuleta meli nyingine kubwa zaidi," amesema Massawe.
hii inasaidia nini watanzania? au sifa za kijinga tuu maaammae.
 
Watetezi wa bandari ya Bagamoyo waone aibu. Maana tulikuwa tunaambiwa kuwa bandari ya Dar haiwezi kushindana na bandari ya Mombasa hivyo tukitaka kushindana basi tujenge bandari ya Bagamoyo; leo wamesutwa.

Narudia hakuna haja ya bandari ya Bagamoyo.
Kwahiyo kuja kwa hiyo meli ndo inaonesha Bandari ya Dar ina uwezo wa kushindana na Bandari ya Mombasa, au?!!

Au kwavile umeambiwa bandari imepokea "bonge la mmeli" ndo maana umefikia kusema hayo!!!

FYI, ile meli wamesema ina urefu wa almost 200M, wakati Megaships zinafikia hadi 400M; and it's matter of time kabla hazijitengenezwa zenye urefu wa hata 500M!!

Meli kama hizo nilizotaja hapo juu haziwezi kuingia Dar Port!!

Na kama unadhani kuingia meli yenye urefu wa 200M ndo inaonesha mbavu zetu dhidi ya Mombasa, hebu soma hapa chini:-
The Panama flagged vessel has a length overall of 300 m, a breadth of 48m, height of 62 m and deadweight of 110629 tonnes and a gross tonnage of 94469.
Hiyo ndo meli ambayo ilifunga gati Mombasa way back in 2018!!

Na hapa chini, ni idadi ya meli zilizofunga gati, na zinazotarajiwa kuingia kwenye bandari hizo mbili kama inavyoripitiwa na Marine Traffic---
Dar.png


Mombasa.png

Sasa endeleeni kuleta mizaa kwenye mambo serious, lakini nikukumbushe tu kwamba, Firs Phase ya Lamu Port imeshakamilika!!
 
Kwahiyo kuja kwa hiyo meli ndo inaonesha Bandari ya Dar ina uwezo wa kushindana na Bandari ya Mombasa, au?!!

Au kwavile umeambiwa bandari imepokea "bonge la mmeli" ndo maana umefikia kusema hayo!!!

FYI, ile meli wamesema ina urefu wa almost 200M, wakati Megaships zinafikia hadi 400M; and it's matter of time kabla hazijitengenezwa zenye urefu wa hata 500M!!

Meli kama hizo nilizotaja hapo juu haziwezi kuingia Dar Port!!

Na kama unadhani kuingia meli yenye urefu wa 200M ndo inaonesha mbavu zetu dhidi ya Mombasa, hebu soma hapa chini:-

Hiyo ndo meli ambayo ilifunga gati Mombasa way back in 2018!!

Na hapa chini, ni idadi ya meli zilizofunga gati, na zinazotarajiwa kuingia kwenye bandari hizo mbili kama inavyoripitiwa na Marine Traffic---
Sasa endeleeni kuleta mizaa kwenye mambo serious, lakini nikukumbushe tu kwamba, Firs Phase ya Lamu Port imeshakamilika!!
Huwa tunashangaaga sana Kenya wanapotunyoosha kwenye mapato wakati utalii hata sisi tunao tena kuwazidi. Kenya watu 52m kama sijakosea bajeti TZS 78 trillions. Tanzania watu 60m bajeti TZS 36 trillions . Nimecheka tu lakini sio mazuri
 
Kiongozi Mkuu anaweza kuwa misinformed kwenye suala la Bandari kama alivyokuwa misinformed kwenye suala la Covid-19.

Sina utaalamu sana kwenye masusla ya kodi lakini niliangalia faida za ziada na kodi vyanzo vya mapato vitavyotengenezwa na mradi.

Tukumbuke fedha ya mradi huu sio mkopo, bali nu fedha karibia trillions 23 mtu anakuja kuwekeza hivyo anahitaji muda kurudisha fedha yake na faida juu.

Pia suala la kijiografia, tumezungukwa na nchi 8 ambazo 6 hazina bandari zimekuwa zikitegemea bandari yetu ya Dsm. Ambayo pia imekuwa ikipata ushindani wa kibiashara kutoka kwenye bandari za Lamu, Beira na Durban kutokana na ufanisi wa hizo bandari.

Pia bandari yetu kuu bado ni ndogo kwa Dunia ya sasa na technology ilivyokuwa ndio maana tumeshangaa meli kubeba gari 3700 wakati kuna bandari zinauwezo wa kupokea meli za kubeba gari 8000 kwa wakati mmoja. Tulipokea meli ya kontena 5000 na yenyewe ikawekwa kwenye font fod wakati huko Duniani Kuna meli zinabeba kontena 20000.

Pia hatukujenga SGR kwa ajili ya kutumia Kama tunavyotumia MGR. Uwezo wa SGR ni kubeba mzigo mkubwa na kwa haraka zaidi. Tunaboresha reli kwa matrilion lakini Mlango (Bandari) wa kupokea na kutolea Mzigo bado na mwembamba moja moja utaweza ona faida ya SGR ni bora tubaki na MGR kulilo kuteketeza Kodi za watanzania hapo kwe SGR.

Pia mradi ulikuwa unakuja na viwanda karibia 190 kwenye eneo la Bagamoyo na Pwani, sijajua vingetoa ajira kiasi gani na mapato kiasi gani kwa serikali ya mkoa na serikali kuu.

Mkuu umeongea mambo ya msingi sana, nami acha niseme kidogo kuhusu masuala ya kodi!!!

Pale Bandarini kuna kodi kuu za aina tatu...

1. Import/Export Tax
2. Value Added tax (VAT),
3. Excise Duty, na
4. Income Tax.

Hizo kodi #1 hadi #3 ni MALI YA SERIKALI.

Sasa kama kodi zote 3 ni mali ya serikali, Mchina atapata nini?!

Mchina kazi yake pale ni kutoa huduma!! Atapokea meli zinazoleta na kufuata mizigo!! Hapa atalipwa Mapato (Income)!

Atakuwa na eneo la kuhifadhi mizido... hapa tena atakuwa analipwa na wenye mizigo yao

Atakuwa pia anatoa huduma ya meli kufunga gati hapo bandarini... hapa napo Mchina atakuwa analipwa na wenye meli zao!

Zipo pia shughuli/huduma nyingine atakazotoa Mchina, na atakuwa analipwa!!!

Sasa hayo mapato hapo juu kisheria anatakiwa alipie kodi niliyotaja kama #4, yaani Income Tax!!

Sasa basi, kawaida ya Mchina, na hata Investors wengine hususani kwenye BOT Projects, huwa anaomba asamehewe hiyo Income Tax!!

Sasa Mamlaka husika badala ya kuwa wakweli ni kodi ipi Mchina anaomba kusamehewa, wao wanaongea kijumla jumla tu kwamba "Mchina anataka kusamehewa kodi"!

Lakini kama ulivyosema hapo juu, faida za mradi kwa ujumla ni kubwa kuzidi hata hiyo Income Tax!!!

Watu hatuangalii ni ajira ngapi zitatolewa kupitia Bagamoyo Port na mradi pacha wake, Yaani Industrial City!!

Watu hatuangalii multiplier effect itakayotokea hapo bandarini na kwenye mradi pacha wake!!

Kwa faida ya wengine, na kwa mujibu wa Investopedia...
The multiplier effect refers to the proportional amount of increase, or decrease, in final income that results from an injection, or withdrawal, of spending.

Generally, economists are usually the most interested in how capital infusions positively affect income. Most economists believe that capital infusions of any kind—whether it be at the governmental or corporate level—will have a broad snowball effect on various aspects of economic activity.

As its name suggests, the multiplier effect provides a numerical value or estimate of a magnified expected increase in income per dollar of investment.

Yaani, ndo hivyo imefanyika investment kubwa ya bandari ya Bagamoyo... what next?

The next is: Mosi kutakuwa na ajira itakayohakikisha kipato kwa waajiriwa!!! Huyu mwajiriwa akipata mshahara wake, sehemu ya mshahara atanunua mama nitilie, atanunua maji ya kunywa, atanunua nguo, atalipa nauli, n.k!!!

Yule Mama Ntilie aliyepokea pesa ya Mfanyakazi wa Bandari, nae sehemu ya hiyo pesa ataenda gengeni kununua nyanya, vitunguu, mchele, n.k! Hao waliolipwa na Mama Ntilie nao pesa hiyo itaenda kwa wengine!!

Sasa unakuta pesa iliyowekezwa Bandarini Bagamoyo, imenyambulika kidogo kidogo hadi imemfikia Mkulima wa Nyanya aliyepo Lushoto... yaani ime-multiply!!

Kwenye Decision Making, hususani serikalini, Multiplier Effect ni jambo la msingi kuliko hata hiyo direct tax kwa sababu, unaweza kukosa kodi bandarini lakini pesa iliyotoka hapo bandarini imeenda kuboresha sekta zingine za kiuchumi zinazoweza kukuletea kodi uliyoikosa bandarini!!
 
Ishu ni idadi kubwa ya magari iliyobebwa kwenye hiyo Meli na yakashuka Dar Port.

Meli hiyo aina ukubwa wowote mita 199.9, waandishi wa habari wameikuza Sana hii taarifa mpaka DG anatokea kwenye ishu ndogo kama hii.

Mwezi uliopita Dar es Salaam Port Kuna Meli ilikuja (Ship Carrier) ilileta meli za wachina wanaotanua bandari hakuna media au waandishi walioenda kupiga picha Wala kutangaza.

Kwa Sasa vyombo vya habari vingekuwa vinaweka mambo kama meli fulani ya Container au Bulk Cargo(Mzigo wa shehena) imekuja na mzigo kiasi Fulani na umeshuka ndani ya muda mfupi (Ship turn around) habari za uzalishaji bandari Ndio mpango.
 
Huwa tunashangaaga sana Kenya wanapotunyoosha kwenye mapato wakati utalii hata sisi tunao tena kuwazidi. Kenya watu 52m kama sijakosea bajeti TZS 78 trillions. Tanzania watu 60m bajeti TZS 36 trillions [emoji13]. Nimecheka tu lakini sio mazuri
Hapo nilipo-bold ndo umemaliza kila kitu!!

Nishawahi kusema hapa JF mara kadhaa kwamba wakati mwingine watu tunaingia Jukwaa la Kenya na kuamua tu kujitoa ufahamu ili kuitetea nchi yetu lakini ukweli ni kwamba, jamaa wametuzidi kwenye idara nyingi sana za kiuchumi!!!

Ni kutokana na hilo, ndo maana binafsi huwa nakwepa sana mijadala ya kule Jukwaa la Kenya kwa sababu nafahamu ili kuitetea nchi yangu nitatakiwa ama niwe na-twist mada zinazotolewa na Wakenya, au niamue kujitoa ufahamu!!
 
Siku moja nitaenda kutalii bandarini, nione hizo meli zinavyofanana, kwa kweli sikuwahi kufikiri kama meli inaweza kubeba magari mengi kiasi hicho
Kwani wanaruhusu mkuu kuingia mule ndani na kufanya utalii mi mwenyew napenda sana kuona mule ndani shughuli zinavofanywa.
 
Hapo nilipo-bold ndo umemaliza kila kitu!!

Nishawahi kusema hapa JF mara kadhaa kwamba wakati mwingine watu tunaingia Jukwaa la Kenya na kuamua tu kujitoa ufahamu ili kuitetea nchi yetu lakini ukweli ni kwamba, jamaa wametuzidi kwenye idara nyingi sana za kiuchumi!!!

Ni kutokana na hilo, ndo maana binafsi huwa nakwepa sana mijadala ya kule Jukwaa la Kenya kwa sababu nafahamu ili kuitetea nchi yangu nitatakiwa ama niwe na-twist mada zinazotolewa na Wakenya, au niamue kujitoa ufahamu!!
Ukweli mchungu, jamaa wametuacha inabidi tupambane.
 
View attachment 1887764

View attachment 1887765

Bandari ya Dar es Salaam imeendelea kuzivutia kampuni kubwa za usafirishaji duniani, baada ya meli kubwa ya kisasa ikiwa na shehena kubwa zaidi ya magari kuwahi kutia nanga bandarini hapo.

Meli hiyo ya TRANQUAIL ACE (IMO: 9561253) inayomilikiwa na Kampuni ya Mitsui ikitokea moja kwa moja nchini Japan, imetia nanga ikiwa na magari 3,743 ambayo ni mengi zaidi kuwahi kusafirishwa kuja nchini kwa mara moja.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Eric Hamissi amesema kuwa meli hiyo imeandika historia mpya kutokana na kubeba shehena kubwa ya magari.

Meli hiyo iliyotengenezwa mwaka 2009 ina urefu wa mita 199.9 na upana mita 32.2 kwenda chini, ambapo imetia nanga chini ya nahodha, Diardado Garate.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 10, 2021 katika Bandari ya Dar es Salaam, Hamissi amesema kuwa meli hiyo imetia nanga Agosti 9, 2021 na kuanza shughuli ya ushushaji ambao unatarajiwa kumalizika kesho jioni.

Meli kubwa kuwahi kutia nanga nchini na ailiyokuwa imebeba shehena kubwa ya magari ilitia nanga bandarini hapo mwaka 2018 ikiwa na magari 2600.

"Leo ni siku nzuri sana katika historia ya TPA kwa kuweka rekodi mpya kwa kupokea meli kubwa na iliyobeba shehena kubwa zaidi kuja nchini. Hii haijawahi kutokea katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na kubwa zaidi meli hii imetoka moja kwa moja Japan kuja nchini bila kupitia bandari nyingine.

View attachment 1887766

"Kwa hiyo ni jambo jema dunia inakafahamu kwamba, Tanzania tuna bandari bora na ya kisasa yenye uwezo wa kupokea meli zote na ikazihudumia kwa wakati,” amesema Hamissi na kuongeza: “Katika inayoendelea kushushwa, magari yatasafirishwa kwa njia ya barabara kwenda nchi jirani na mengine 798 yanabaki hapa nchini.

"Mtaona ni jinsi gani sasa nchi zetu za jirani zinazotuzunguuka zimeenza kutuamini, kati ya magari yaliyoingia asilimia 65 yanakwenda kwenye nchi hizo."

Meneja Kampuni ya Inchcape Shipping Services, John Massawe amesema meli hiyo ina uwezo wa kubeba magari 5,200 na kwamba imetumia siku 20 ikiwa safari hadi kuwasili.

"Tumekuwa tukihudumia kampuni ya magari kwa miaka zaidi ya 20, na hii ni meli ya kwanza hivyo tunatarajia huu ni mwanzo wa kuleta meli nyingine kubwa zaidi," amesema Massawe.
Let's hope hayo magari asilimia kubwa yawe mapya,sio used,maana itakuwa kama imekuja kufanya dumping ya mikweche iliyochoka
 
Back
Top Bottom