Dar: Mahakama ya Kisutu yamfutia kesi na kumwachia huru dereva aliyetuhumia kumteka Mo Dewji

Futeni haraka pia kesi ya ugaidi# Mbowe sio gaidi na walinzi wake pia, mnaliaibisha taifa.Kelele zikizidi tutapata hasara kubwa.
 
- KumbukiziMTAFUTANO.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imemfutia kesi na kumwachia huru dereva taksi Mousa Twaleb aliyekuwa akituhumiwa kuhusika na tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara maarufu, Mohammed Dewji almaarufu ‘Mo Dewji’.

Twaleb alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Mei 28, 2019 akikabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kumteka Mo, tukio lililotokea alfajiri ya Oktoba 11, 2019 wakati mfanyabiashara huyo akielekea mazoezini katika Hoteli ya Colosseum iliyopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Bilionea huyo aliachiliwa huru Oktoba 20, 2019 zikiwa ni siku tisa baada ya kutekwa baada ya watu waliomteka kudaiwa kumtelekeza kwenye viwanja vya Gymkhana.

NANI ALIMTEKA MO au HAKUTEKWA?
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom