JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,458
Bunaza Doto Manyanda (34) anadaiwa kumuua mpenzi wake, Happiness Mzalile Zakaria (23) kwa kumchoma na kitu chenye ncha kali tumboni kisha naye kujiua, marehemu wote wakiwa ni Wakazi wa Charambe kwa Mbiku Wilayani Temeke, Dar es Salaam.
Tukio hilo limetokea jana Jumatano Juni 8, 2022 ambapo Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar, Muliro Jumanne amesema baada ya mauaji, ndipo Bunaza akaamua kujiua kwa kunywa dawa ya kuulia wadudu wa mazao ya DUDU CRON, vidonge vya flagyl na kuchanganya na pombe.
“Bado tunachunguza chanzo, miili ya marehemu imehifadhiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,” - anasema Muliro.
Tukio hilo limetokea jana Jumatano Juni 8, 2022 ambapo Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar, Muliro Jumanne amesema baada ya mauaji, ndipo Bunaza akaamua kujiua kwa kunywa dawa ya kuulia wadudu wa mazao ya DUDU CRON, vidonge vya flagyl na kuchanganya na pombe.
“Bado tunachunguza chanzo, miili ya marehemu imehifadhiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,” - anasema Muliro.