Ooh yes
Senior Member
- Jul 31, 2020
- 174
- 116
Napenda siku moja kushuhudia uchaguzi huru na wa hakiCHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA
Ratiba ya mikutano 5 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mhe. Tundu Lissu, iliyopangwa kufanyika leo mkoani Pwani, imevurugika baada ya helkopta aliyokuwa aitumie kufika katika maeneo hayo, kuzuiliwa kwa kunyimwa kibali na Mamlaka ya Anga nchini, muda mfupi kabla ya kuruka.
Taarifa za kukataliwa kwa helkopta hiyo kuruka zilitolewa kwa Ofisa Mnadhimu wa Kampeni, Amani Golugwa, wakati msafara wa Mhe. Lissu ukielekea kupanda ndege baada ya kumaliza taratibu zote za ukaguzi wa kiusalama Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) terminal I.
Ofisa wa Mamlaka ya Anga aliyewasilisha taarifa hiyo wakati msafara wa Mhe. Lissu umeshatoka nje ya jengo la abiria, ametoa sababu zisizoeleweka kuzuia helkopta hiyo kuruka kutoka Uwanja wa JNIA kuelekea Bagamoyo, Chalinze, Mlandizi na Kibaha, wakati kibali chake kiliombwa tangu jana.
Kutokana na hatua hiyo, Chadema imelazimika kutafuta njia mbadala ili Mgombea Urais Mhe. Lissu na msafara wake, aweze kuendelea na ratiba ya mikutano kwa kadri inavyowezekana. Mbali ya Mhe. Lissu, abiria wengine waliokuwa watumie usafiri huo ni watu 3, akiwemo Ofisa Mnadhimu wa Msafara Amani Golugwa, Katibu wa Mgombea, David Jumbe, msaidizi wa masuala ya ulinzi pamoja na rubani wa ndege hiyo.
Imetolewa leo, Alhamis, Septemba 10, 2020 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
TCAA yawajibu CHADEMA; Yasikitishwa na upotoshaji wao