Dar Es Salaam tumieni maji ya baharini, maji ni mengi sana yale

Wakati ule ndiyo nakuja mjini kwa mara ya kwanza, nilienda baharini nikashinda huko kutwa nzima, sasa nikawa na kiu na niko ufukweni mwa bahari, nikijua maji yake ni sawa tu na yale ya Ziwa Tanganyika, nikainama ili ninywe,
Loh! kumbe yana chumvi zaidi ya Uvinza.
Muha wewe
 
Nilimtembelea binamu yangu anaishi kijijini. Nilimkuta ana simtank ya litre 10,000 amezungusha gutters bati lote. Ameweka umeme wa solar na ana mtungi wa gas kwa kupikia. Anasema kabla ya litre 10,000 hazijaisha mvua inakua imenyesha tena.
Lita 10,000 msimu mpaka msimu? ni familia ya Watu wangapi?.

Hapa jirani yangu tu Mtu na Mkewe/Girl friend hawamalizi wiki bila kupandisha maji kwenye tanki la lita 2000.

Labda Binamu ana chanzo kingine cha maji, au la ana nidhamu kubwa sana ya matumizi.
 
Umeambiwa yamepungua kwa kiasi kikubwa. Dar ni mji wenye watu wengi na matumizi ya maji ni makubwa.
Waongo hao usiwasikilize enzi za jk zimerudi tuliwahi kuambiwa kuwa kina cha maji mtera kimepungua ndio maana kuna mgao wa umeme,mbona enzi za yule dikteta hizo story zilipotea,jk is back,mgao wa maji na umeme vitarudi
 
Lita 10,000 msimu mpaka msimu? ni familia ya Watu wangapi?.

Hapa jirani yangu tu Mtu na Mkewe/Girl friend hawamalizi wiki bila kupandisha maji kwenye tanki la lita 2000.

Labda Binamu ana chanzo kingine cha maji, au la ana nidhamu kubwa sana ya matumizi.
Lita 2000 kwa wiki wastani wa mapipa nane,so zaidi ya pipa moja kwa siku ,wako vizuri
 
Lita 2000 kwa wiki wastani wa mapipa nane,so zaidi ya pipa moja kwa siku ,wako vizuri
Sio vizuri Ndugu, ni matumizi mabaya...mimi kumwaga hata maji niliyosuuzia nguo huwa roho inaniuma, nitayatunza niyatumie kwa shughuli nyingine.
 
Lita 10,000 msimu mpaka msimu? ni familia ya Watu wangapi?.

Hapa jirani yangu tu Mtu na Mkewe/Girl friend hawamalizi wiki bila kupandisha maji kwenye tanki la lita 2000.

Labda Binamu ana chanzo kingine cha maji, au la ana nidhamu kubwa sana ya matumizi.
No mvua hunyesha kila baada ya miezi mitatu, ukiacha za vuli na masika Kuna zile za rasha rasha. Matumizi makubwa ya maji ni kuoga kwenye shower na tub pamoja na flushing ya chooni.

Kijijini choo cha shimo na kuoga unakinga ndoo unapeleka bafuni.
 
No mvua hunyesha kila baada ya miezi mitatu, ukiacha za vuli na masika Kuna zile za rasha rasha. Matumizi makubwa ya maji ni kuoga kwenye shower na tub pamoja na flushing ya chooni.

Kijijini choo cha shimo na kuoga unakinga ndoo unapeleka bafuni.
Hakika inahitajika pia elimu ya matumizi bora ya maji.

Maji yatumike zaidi ya mara mbili au tatu kutegemea na matumizi...ka mfano maji yakifulia yatumike tena msalani kwa kuflash na kushea choo n.k.
 
Hivi Dar es Salaam na Pwani kuna water reservoirs ngapi? Maji ya mvua huwa kuna jitihada za kuyakusanya na kuyasafisha?
Hakika inahitajika pia elimu ya matumizi bora ya maji.

Maji yatumike zaidi ya mara mbili au tatu kutegemea na matumizi...ka mfano maji yakifulia yatumike tena msalani kwa kuflash na kushea choo n.k.
Matatizo maji ya kuvulia kuoshea choo choo kinakua na rangi ya uchafu flani hivi. Labda u flush kutoa mzigo na umwage ndoo ya pili kusuuza.

Nilimtembelea rafiki yangu Kampala, yeye maji ya choo ameunganisha na simtank. Maji ya idara ni ya jikoni na kufulia. Simtank inakusanya maji ya mvua.
 
Water desalination ni gharama sana ila ina fiada pia na maji yake yanabidi yawe ghari sana kwa ajili ya replac ement za filter..

Dasani nadhani wanatumia Maji ya baharini
 
chukua chumvi robo kilo hapo mkoani,itie kwenye kikombe chenye maji nusu rita changanya,kisha koroga uonje.

chumvi uliyosikia ndio kiwango kilichopo ktk maji ya baharini,huwezi kuyafanyia chochote hayo.

kama uko porini umechoma nyama,na ukawa nayo,unaweza yatumia kama chumvi bila kuhisi kitu chochote kupungua.
Lakini naamini bado ipo namna nzuri tu ya kuyafanya yatumike iwapo tutatumia akili na maarifa aliyotupa Mwenyezi Mungu.

Mungu anataka tutumie akili ndio maana hakuyaacha yawe rahisi tu kuyatumia, kwamba tukachote tu tunywe tuende.
 
Wakati ule ndiyo nakuja mjini kwa mara ya kwanza, nilienda baharini nikashinda huko kutwa nzima, sasa nikawa na kiu na niko ufukweni mwa bahari, nikijua maji yake ni sawa tu na yale ya Ziwa Tanganyika, nikainama ili ninywe,
Loh! kumbe yana chumvi zaidi ya Uvinza.
Kwaiyo ukanywa maji ya chumvini
 
Mkuu hututakiii mema yale maji mabomba yote ya maji taka kitoka magorofa ya wahindi kariakoo posta yote yanamwaga uchafu humo ukiachilia mbali bombaa kuu kutoka hospital ya muhimbili maji yote ya kuoshwa maiti jamani jamani jamani alaf unatushauri nini mkuu SHWAIN kabisa
 
Nilimtembelea binamu yangu anaishi kijijini. Nilimkuta ana simtank ya litre 10,000 amezungusha gutters bati lote. Ameweka umeme wa solar na ana mtungi wa gas kwa kupikia. Anasema kabla ya litre 10,000 hazijaisha mvua inakua imenyesha tena.

Yupo vizuri. Hata mimi ninapenda this kind of life style.
1. Mtungi wa gas wa kupikia as ine Oryx/Mihan gas au gas ipi haswa?

2. Kuhusu maji na umeme solar hata sisi tunafanya hivyo. Ila kuna sehemu niliona wanapiga mikwara/beat kwamba uvunaji wa maji ya mvua sijui ni illegal eti mpaka vibali bla bla blah dah. Guys is harnessing rain-water into your own private rain-water reservoir at home illegal?
 
Yupo vizuri. Hata mimi ninapenda this kind of life style.
1. Mtungi wa gas wa kupikia as ine Oryx/Mihan gas au gas ipi haswa?

2. Kuhusu maji na umeme solar hata sisi tunafanya hivyo. Ila kuna sehemu niliona wanapiga mikwara/beat kwamba uvunaji wa maji ya mvua sijui ni illegal eti mpaka vibali bla bla blah dah. Guys is harnessing rain-water into your own private rain-water reservoir at home illegal?
Mmoja ninamfahamu anaishi Makongo Juu, yeye amechimba kisima cha litre 30,000 na simtank 10,000. Ametega mvua hasa za masika simtank ikijaa yanaingia kisimani. Simtank ikiisha ana pump ya kisimani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom