Dar Es Salaam tumieni maji ya baharini, maji ni mengi sana yale

Yupo vizuri. Hata mimi ninapenda this kind of life style.
1. Mtungi wa gas wa kupikia as ine Oryx/Mihan gas au gas ipi haswa?

2. Kuhusu maji na umeme solar hata sisi tunafanya hivyo. Ila kuna sehemu niliona wanapiga mikwara/beat kwamba uvunaji wa maji ya mvua sijui ni illegal eti mpaka vibali bla bla blah dah. Guys is harnessing rain-water into your own private rain-water reservoir at home illegal?
illegal ya wapi hiyo,kijijini kwetu huko huwa wanavuna maji ya kutosha maelfu ya Lita,nyumba nyingi Zina chemba za maji Tena ya kutosha kabisa...
 
Leo nimesikia kwenye habari ya kuwa Mikoa ya Dar Es Salaam na Pwani watarajie upungufu wa maji kutokana na kina cha maji ya Mto Ruvu kupungua.

Mwanamuziki Bob Marley kwenye wimbo wake wa 'Rat race' kuna mstari anasema "in the abudance of water the fool is thirty"...na maandiko yanasema "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa".

Nimekuwa najiuliza hili kwa miaka mingi kuhusu yale maji ya baharini, ni maji mengi sana yasiyotarajiwa kuisha milele...Miaka ya nyuma niliwahi kumsikia Mwanasayansi au Mwanasiasa sikumbuki vizuri wa hapa kwetu akisema teknolojia ya kusafisha maji yale ni ghali sana, nikajisemea 'ala' sasa ikiwa ghali ndio tupande vitandani tuchape usingizi tusubiri miujiza?.

Mambo duniani hufanywa kwa mikakati, kama tuna Wanasayansi nchini basi tuwawezeshe washinde maabara usiku na mchana mpaka wapate jibu, waje na teknolojia rahisi ya kuwezesha kutumia maji ya baharini kwa matumizi ya kila siku ya kibinaadamu na kilimo.

Marekani waliweka tu mikakati kuhakikisha Binaadamu anafika kwenye mwezi na ikawa...Hata chanjo ya corona ni mikakati tu baada ya Binaadamu kuwa cornered.

Tusisubiri kila jibu litoke kwa Binaadamu wengine ili hali hata sisi ni Binaadamu.
Mimi naona majibu rahisi ya 'aghali sana' bila kufafanua ughali sana wake ni upi, ni majibu ya 'wabunge vihiyo' wanaojibu bila utafiti ama kwa ghilba za ubinafsi.

Maana kuna nchi, hii teknolojia wanayo kitambo sana.

Wao wameweza wana nini na sisi tumeshindwa tunanini?

Maana ingelikuwa ni ghali kama tunavyopotoshwa, waIsraeli wasingelikuwa na ubavu wa kuyachuja kutosheleza hadi ziada ya kumwagilia mashamba.

WaTz ama waAfrika sijui huwa kwanini tunapenda kubweteka hadi akili, maana zamani ilikuwa kuongelea kwa mfano treni za umeme kwenye nchi kama ya kwetu hii, unaonekana mtu kama unaota, lakini kumbe dhamira chanya ikiwepo hakuna linaloshindikana!
 
Nilimtembelea binamu yangu anaishi kijijini. Nilimkuta ana simtank ya litre 10,000 amezungusha gutters bati lote. Ameweka umeme wa solar na ana mtungi wa gas kwa kupikia. Anasema kabla ya litre 10,000 hazijaisha mvua inakua imenyesha tena.
Mkuu hiyo figures za tarakimu nadhani umekosea!

Mimi nina tanki lita 5000 nalitumia karibia siku8, hivyo lita 10,000 almost 2 weeks only!
 
Hilo nalo ni la kulifikiria. Miji mingi mikubwa ya wenzetu hupata maji toka kwenye reservoirs. Lakini Dar wanategemea yanayoflow mtoni. Na karibu miji yote Bongo wanategemea hivyo. Walau Moro wana Mindu. Dar wangeweza hata kudam Ruvu au Wami na kusahau shida ya maji.
.. Wami ndio tunajenga Daraja jipya kwanza....baada ya Miaka 60 ya Uhuru Mkuu !!
 
Wakati ule ndiyo nakuja mjini kwa mara ya kwanza, nilienda baharini nikashinda huko kutwa nzima, sasa nikawa na kiu na niko ufukweni mwa bahari, nikijua maji yake ni sawa tu na yale ya Ziwa Tanganyika, nikainama ili ninywe,
Loh! kumbe yana chumvi zaidi ya Uvinza.
Hahahaha sio pow
 
Leo nimesikia kwenye habari ya kuwa Mikoa ya Dar Es Salaam na Pwani watarajie upungufu wa maji kutokana na kina cha maji ya Mto Ruvu kupungua.

Mwanamuziki Bob Marley kwenye wimbo wake wa 'Rat race' kuna mstari anasema "in the abudance of water the fool is thirty"...na maandiko yanasema "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa".

Nimekuwa najiuliza hili kwa miaka mingi kuhusu yale maji ya baharini, ni maji mengi sana yasiyotarajiwa kuisha milele...Miaka ya nyuma niliwahi kumsikia Mwanasayansi au Mwanasiasa sikumbuki vizuri wa hapa kwetu akisema teknolojia ya kusafisha maji yale ni ghali sana, nikajisemea 'ala' sasa ikiwa ghali ndio tupande vitandani tuchape usingizi tusubiri miujiza?.

Mambo duniani hufanywa kwa mikakati, kama tuna Wanasayansi nchini basi tuwawezeshe washinde maabara usiku na mchana mpaka wapate jibu, waje na teknolojia rahisi ya kuwezesha kutumia maji ya baharini kwa matumizi ya kila siku ya kibinaadamu na kilimo.

Marekani waliweka tu mikakati kuhakikisha Binaadamu anafika kwenye mwezi na ikawa...Hata chanjo ya corona ni mikakati tu baada ya Binaadamu kuwa cornered.

Tusisubiri kila jibu litoke kwa Binaadamu wengine ili hali hata sisi ni Binaadamu.
Hili suala ni linawezekana kutumia Yale maji, ishu juu ndiyo hiyo uthbutu wa kuanza hatuna, tunatishika na gharama za uendeshaji
 
Hata tusihangaike na maji ya bahari kwa sababu ni gharama kuyafanya yawe safi...

Tunaweza tukafanya vitu viwili vya uhakika...
1. Kuvuna maji ya mvua na kuyatumia wakati kunapotokea uhaba wa maji ya mto

2. Matumizi ya visima virefu sababu mikoa ya Dar na Pwani yana maji chini ya ardhi
 
Mimi naona majibu rahisi ya 'aghali sana' bila kufafanua ughali sana wake ni upi, ni majibu ya 'wabunge vihiyo' wanaojibu bila utafiti ama kwa ghilba za ubinafsi.

Maana kuna nchi, hii teknolojia wanayo kitambo sana.

Wao wameweza wana nini na sisi tumeshindwa tunanini?

Maana ingelikuwa ni ghali kama tunavyopotoshwa, waIsraeli wasingelikuwa na ubavu wa kuyachuja kutosheleza hadi ziada ya kumwagilia mashamba.

WaTz ama waAfrika sijui huwa kwanini tunapenda kubweteka hadi akili, maana zamani ilikuwa kuongelea kwa mfano treni za umeme kwenye nchi kama ya kwetu hii, unaonekana mtu kama unaota, lakini kumbe dhamira chanya ikiwepo hakuna linaloshindikana!
Kwa mvua tunazopata Tanzania, hatuhitaji kuingia gharama hizo, kwanza wananchi wahamasishwe kupanda miti hata mijini, moja ya faida za miti ni kuleta mvua.

Water reservoirs kujengwa zikusanye maji ya kutosha hata miaka miwili mvua ikikosekana.
 
Yule dada alietoa ushuhuda wa Hamza alienda kujisaidia baharini, nikukumbushe
 
Ruvu na Wami ni mbali, yale maji ya Jangwani yanoyozuia watu kwenda makazini yale yangekwenda kwenye reservoir mbona yangeleta mabadiliko chanya.
Jumlisha na Bonde la mto Mzinga ambalo maji yake hupotea baharini kupitia kijichi
 

Similar Discussions

16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom