Dar es Salaam: RC Makalla azuia utekelezaji wa amri ya kuzuia bodaboda na bajaji kuingia city center

... ajabu sana mkuu! Unakataza Hiace (abiria 15) na Coaster (abiria 28) kufika maeneo kama Feri ila unaruhusu utitiri wa bajaji (abiria 3) na bodaboda (abiria 1) kuhanikiza mjini! Hawa wapuuzi mahali popote wanasimama na wanageuza; abiria yuko upande wa pili wa barabara wanageuza wanamfuata kisha wanageuza tena hapo hapo katikati ya barabara wanaendelea na safari!

Kuruhusu hivi vyombo mjini na highway kama Nyerere Rd; Morogoro Rd; A. Mwinyi Rd; Kawawa Rd; Mandela Rd; Sam Nujoma Rd; Shekilango Rd; etc. ni ukosefu wa busara na maarifa. Sio kila chombo kiruhusiwe kupita kila mahali kwa kisingizio cha "riziki" au eti "watanzania ni maskini". Riziki kwako isiwe kero kwa wengine.
You nail it!! Ulichokiongea Nathan kama wanatusikiliza na kutusoma ndio iwe ajenda yao kesho!! Mipango yoyote inatakiwa kusimamiwa na utaratibu na sheria, huwezi kuruhusu vitu kiholela ukategemea ndio kugawa riziki!! Na katika taifa lolote huwezi kuweka kila MTU akajiajiri mwenyewe
 
Hapa Makalla alichukua uamuzi kwa kukariri, akadhani kwasababu machinga imewezekana kuondolewa basi na bodaboda it will be the same, hapana haitakuwa, bodaboda na bajaji wana umuhimu zaidi kwa personal needs in case of emergency zaidi ya machinga.
 
Wakizuia boda wake kwa waume wataota vigimbi kwa kutembea kwa miguu nyakati za foleni. Ukweli ni kwamba si wote ila kuna baadhi ya madereva wa boda hawaendeshi kistaarabu wakiwa katikati ya jiji wao mda wote mi mbio tu kama vile wanawahi namba.
 
MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam, Amos Makalla, amezuia utekelezaji wa zuio la Bodaboda na Bajaji kuingia katikati ya mji hadi atakapotoa tamko jipya baada ya kikao alichoitisha na uongozi wa Bodaboda, Kikosi cha Usalama Barabarani na Uongozi wa Jiji la Dar es Salaam.

Kikao hicho kimepangwa kufanyika Jumatatu ijayo Novemba Mosi.

Zuio la Makalla limekuja saa chache baada ya Kamishna Msaidizi wa Polisi, Mkuu wa Usalama Barabarani Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Abdi Issango, kunukuliwa akipiga marufuku Bodaboda na Bajaji wote kutoingia mjini na wale walioko mjini watoke isipokuwa bajaji za walemavu. Marufuku hiyo ilikuwa ianze rasmi utekelezaji wake Novemba Mosi.

Hata hivyo, Makalla amesitisha zuio hilo kwa muda hadi hapo atakapokutana na wadau hao Novemba Mosi kabla ya kutoa maamuzi.

Pikipiki na Bajaji ambazo miaka ya nyuma ilikuwa ni marufuku kufika maeneo ya katikati ya mji, ziliruhusiwa rasmi Aprili Mosi mwaka jana na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa wakati huo, Paul Makonda, kuingia katikati ya mji ili kupunguza changamoto ya usafiri katika kipindi ambacho nchi ilikabiliwa na mlipuko wa ugonjwa wa Corona.
Yesu ashaondosha Korona, Bodaboda na Bajaji ndio zinaongoza kwa kuchubua magari ya wanyonge.
Bajaji wanasimama popote na ndio chanzo cha foleni,
Bajaji kutoka Ferry njia ya kati mpaka Darajani- kigamboni ile barabara imekuwa hovyo kabisa, wanaenda taratibu wakitafuta abiria huku wakikwamisha magari, waondolewe kabisa, .

Pikipiki na bajaji zimesababisha kuongezeka kwa magonjwa ya kisukari, kiriba tumbo na presha maana sasa mtu hatembei tena, kila pahala ni usafiri tu ambapo serikali inaingia hasara kubwa kuwahudumia hawa watu
 
Mwendokasi umekaa vizuri sana siku hizi, ingawa hawaendi maeneo yote. Na wenyewe wanasema hawatumii basi zote zilizopo. Tuondoe boda boda tupange mji.
 
Hapa mtoa zuia na mkaataa zuio wote wanajuana........Rc kaona huu upepo wa bodaboda na bajaj huenda ukamtoa nje ya reli,
 
Back
Top Bottom