Dar es Salaam: RC Makalla azuia utekelezaji wa amri ya kuzuia bodaboda na bajaji kuingia city center

Dr Matola PhD

JF-Expert Member
Oct 18, 2010
56,492
92,983
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amezuia utekelezaji wa zuio la Bodaboda na Bajaji kuingia mjini hadi atakapotoa tamko jipya baada ya kikao chake na Uongozi wa Bodaboda, Jeshi la Usalama Barabarani na Uongozi wa Jiji la Dar es salaam.

Mapema leo Mkuu wa Usalama Barabarani Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Abdi Issango alizungumza kupitia Power Breakfast ya Clouds FM na kusema ifikapo November 01, 2021 bodaboda na bajaji zote itakuwa ni marufuku kuingia mjini na kuwataka wale waliokua mjini watoke wote isipokua bajaji za walemavu.

RC Makalla amesema amezipata taarifa hizo na ameelekeza kabla ya utekelezaji wa tamko hilo yeye RC ameitisha kikao hicho Jumatatu November 01 kwa lengo la kutafuta ufumbuzi wa tatizo hilo ambao hautoathiri upande wowote. #MillardAyoUPDATES
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amezuia utekelezaji wa zuio la Bodaboda na Bajaji kuingia mjini hadi atakapotoa tamko jipya baada ya kikao chake na Uongozi wa Bodaboda, Jeshi la Usalama Barabarani na Uongozi wa Jiji la Dar es salaam...
Hii serikali haifai
 
MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam, Amos Makalla, amezuia utekelezaji wa zuio la Bodaboda na Bajaji kuingia katikati ya mji hadi atakapotoa tamko jipya baada ya kikao alichoitisha na uongozi wa Bodaboda, Kikosi cha Usalama Barabarani na Uongozi wa Jiji la Dar es Salaam.

Kikao hicho kimepangwa kufanyika Jumatatu ijayo Novemba Mosi.

Zuio la Makalla limekuja saa chache baada ya Kamishna Msaidizi wa Polisi, Mkuu wa Usalama Barabarani Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Abdi Issango, kunukuliwa akipiga marufuku Bodaboda na Bajaji wote kutoingia mjini na wale walioko mjini watoke isipokuwa bajaji za walemavu. Marufuku hiyo ilikuwa ianze rasmi utekelezaji wake Novemba Mosi.

Hata hivyo, Makalla amesitisha zuio hilo kwa muda hadi hapo atakapokutana na wadau hao Novemba Mosi kabla ya kutoa maamuzi.

Pikipiki na Bajaji ambazo miaka ya nyuma ilikuwa ni marufuku kufika maeneo ya katikati ya mji, ziliruhusiwa rasmi Aprili Mosi mwaka jana na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa wakati huo, Paul Makonda, kuingia katikati ya mji ili kupunguza changamoto ya usafiri katika kipindi ambacho nchi ilikabiliwa na mlipuko wa ugonjwa wa Corona.
 
Zuio ni sawa, ila tunapokosea ni kutoweka utaratibu wa kudumu!! Hapa dar kulikuwa na usafiri wa mabus madogo hiace, au vipanya mjini kukawa hakupitiki na fujo nyingi tukasema kwenye kitovu cha mji hili sio sawa hiace zikahamishwa pembezone, na ikawa ni sawa, sasa baada ya hayo tumeruhusu bajaji na bodaboda, je!?

Tumetumia busara!? Naomba hili lisiamuliwe kisiasa wadau wote washirikishwe Latra na polisi usalama barabarani pamoja na kamati zote ili uamuzi uwe wa kitaalamu zaidi
 
Ulemavu usiwe chambo cha kuvunja utaratibu utakaokuwa umefikiwa, baadae tutakuja na makundi mengine yenye uhitajio nao watataka kupendelewa
 
Wadau wengine Muhimu ni maofisa wa Mipango Miji, wawepo kwenye hicho kikao wawambie viongozi wamepanga nini kwa ajili ya jiji letu!?

Hatuwezi kwenda bila utaratibu, kwa kuwasaidia tu, ningependa kuanzishwe sehemu maalumu na parking ya kutosha ili wahitaji wa huu usafiri waweze kwenda hapo!! Pia kuwe na tozo na wote watakaenda huko wawe na vibali vilivyolipiwa kabisa (wenye vyombo).

Utaratibu ni Muhimu, unakuta ofisa wa Halmashauri ameruhusu watu kujenga vibanda sehemu ya parking na ukisimama barabarani unapigwa faini na ni eneo LA soko!

Ndio maana nasema watu wa Hamashauri ndio tatizo kubwa, Mfano Soko LA Mwananyamala na Solo LA Tegeta Nyuki, na mengineyo mengi!!
 
Zuio ni sawa, ila tunapokosea ni kutoweka utaratibu wa kudumu!! Hapa dar kulikuwa na usafiri wa mabus madogo hiace, au vipanya mjini kukawa hakupitiki na fujo nyingi tukasema kwenye kitovu cha mji hili sio sawa hiace zikahamishwa pembezone, na ikawa ni sawa, sasa baada ya hayo tumeruhusu bajaji na bodaboda, je!? Tumetumia busara!? Naomba hili lisiamuliwe kisiasa wadau wote washirikishwe Latra na polisi usalama barabarani pamoja na kamati zote ili uamuzi uwe wa kitaalamu zaidi
... ajabu sana mkuu! Unakataza Hiace (abiria 15) na Coaster (abiria 28) kufika maeneo kama Feri ila unaruhusu utitiri wa bajaji (abiria 3) na bodaboda (abiria 1) kuhanikiza mjini! Hawa wapuuzi mahali popote wanasimama na wanageuza; abiria yuko upande wa pili wa barabara wanageuza wanamfuata kisha wanageuza tena hapo hapo katikati ya barabara wanaendelea na safari!

Kuruhusu hivi vyombo mjini na highway kama Nyerere Rd; Morogoro Rd; A. Mwinyi Rd; Kawawa Rd; Mandela Rd; Sam Nujoma Rd; Shekilango Rd; etc. ni ukosefu wa busara na maarifa. Sio kila chombo kiruhusiwe kupita kila mahali kwa kisingizio cha "riziki" au eti "watanzania ni maskini". Riziki kwako isiwe kero kwa wengine.
 
... ajabu sana mkuu! Unakataza Hiace (abiria 15) na Coaster (abiria 28) kufika maeneo kama Feri ila unaruhusu utitiri wa bajaji (abiria 3) na bodaboda (abiria 1) kuhanikiza mjini! Hawa wapuuzi mahali popote wanasimama na wanageuza; abiria yuko upande wa pili wa barabara wanageuza wanamfuata kisha wanageuza tena hapo hapo katikati ya barabara wanaendelea na safari!

Kuruhusu hivi vyombo mjini na highway kama Nyerere Rd; Morogoro Rd; A. Mwinyi Rd; Kawawa Rd; Mandela Rd; Sam Nujoma Rd; Shekilango Rd; etc. ni ukosefu wa busara na maarifa. Sio kila chombo kiruhusiwe kupita kila mahali kwa kisingizio cha "riziki" au eti "watanzania ni maskini". Riziki kwako isiwe kero kwa wengine.
hapo feri bodaboda wale waliopak kwenye njia ya wamiguu wale wallahi huwa wanataka kukanyaga watu miguun.wakigombea abiria.inaleta taharruk sana. kwel rizq inatafutwa ila hawana utu wale. wanakupitia miguun walai
 
Back
Top Bottom