Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,811
- 4,533
Rais John Magufuli amemsimamisha kazi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Richard Abwao na mkuu wa upelelezi mkoani humo, John Rwamulema kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili.
Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Novemba 23, 2019 na msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime inaeleza kuwa wawili hao wamesimamishwa kazi wakidaiwa kushirikiana na wamiliki wa kiwanda cha kutengeneza pombe kali cha Canon cha mkoani Shinyanga kukwepa kodi.
“Sababu ya pili ni utovu wa nidhamu kwa kushindwa kutekeleza maelekezo waliyopewa na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Shinyanga ambaye ni mkuu wa Mkoa huo, Zainab Telack,” inaeleza taarifa hiyo.
Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Novemba 23, 2019 na msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime inaeleza kuwa wawili hao wamesimamishwa kazi wakidaiwa kushirikiana na wamiliki wa kiwanda cha kutengeneza pombe kali cha Canon cha mkoani Shinyanga kukwepa kodi.
“Sababu ya pili ni utovu wa nidhamu kwa kushindwa kutekeleza maelekezo waliyopewa na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Shinyanga ambaye ni mkuu wa Mkoa huo, Zainab Telack,” inaeleza taarifa hiyo.