Dar es Salaam Mpya: NSSF kuanzisha miradi mikubwa jijini; Mwisho wa malori kuingia jijini wawadia

Mabadiliko muhimu,tusonge mbele mtu anpokuja na idea nzuri ya kuboresha jambo tumpe sapoti.nchi nyingine wanasonga mbele so let us!
 
Kwanini NCCF WASINGEWAJENGEA WANACHAMA wao kwanza nyumba za bei nafuu kuliko kuwaacha wakihangaika huku pesa zao ya makato yakitumika kunufaisha wengine. Ni vizuri kama wangejenga nyumba kwa wanachama halafu wakawauzia au kuwapangishia kwa gharama nafuu. Mwanachama angepata unafuu na kunufaika na chama kwa upande wangu nilidhani watu muhimu kwanza ni wenye chama halafu unaelekeza mikakati mingine kwa kwingine. Utaachaje nyumba yako ikiungua na kukikimbilia kuuzima wa jirani.
 
Imagine huyu ni Mkurugenzi mkuu wa NSSF,wazo hili lilitakiwa kutolewa na kusimamiwa na PM ama BOss wake ila hao wote wamekaa kimya kama vile hawaoni nchi hii ina vituko sana..
 
Dar! Dar! Dar! Dar! Why not Kigoma?

Kigoma na Mwanza ipo kwenye mipango ya miaka mitano (2010 to 2015) ya JK. Kigoma ataijenga kama Dubai na Mwanza kama California.

Anyway, kama hii kitu ni kweli basi NSSF wapewe serikali na serikali wakaongoze NSSF...............!!!! $0 % ya badget inategemea Umatonya halafu hawa jamaa wanakuja na ndoto zao za kufikirika?? mpaka inaudhi.................KUDADADADADEKI!!!
 
Kigoma na Mwanza ipo kwenye mipango ya miaka mitano (2010 to 2015) ya JK. Kigoma ataijenga kama Dubai na Mwanza kama California.

Anyway, kama hii kitu ni kweli basi NSSF wapewe serikali na serikali wakaongoze NSSF...............!!!! $0 % ya badget inategemea Umatonya halafu hawa jamaa wanakuja na ndoto zao za kufikirika?? mpaka inaudhi.................KUDADADADADEKI!!!

jK alikuwa kashikwa pabaya na Dr. Slaa akaanza kuropoka oovyo
 
Mwakani lazima Nikombe pesa yangu yote, make kwa hizo project haziwezi fanikiwa bila kwanza kuondoa fao la kujitoa
 
Nilimsikia Lowasa Bunge lililoisha akipendekeza hata balozi zetu zijengwe kwa pesa ya NSSF. Hawa jamaa ni balaa na huyu DAU ni dau kweli.
 
Ukisikia ushe..i wa tabia wa ndio huu, kwanza serikali itetehe hoja ya kusema bandari ya Bagamoyo inayotaka jenga hipo kwa mantiki ya kupunguza msongamano wa mjini na kwa sababu za kupunguza unnecessary traffic at city centre. Hapohapo serikali imejizatiti katika kujenga an economic zone to justify the project at the expense of tax payers money and outside investment.

Halafu anakuja mpuuzi kama huyu anasema anataka jenga reli na kubomoa nyumba za watu (assuming with the government blessings) whilst the same government has promised to reduce the inflow of traffic in the city by building another port.

Sasa basi hiwapo bandari ya bagamoyo itajengwa wouldn't that solve that same traffic problem assuming residential areas are restricted and all other plans are considered and the priority is the inflow of goods.

In short Dr. Dau kaishiwa and apparently he has got too much money on his hands na hajui pa kuzipeleka ndio sababu wengine tunasema kuna watu wengi wapo kwenye position ambazo si haki zao sio kwa sababu ya elimu zao bali they're just not creative enough for the posts they hold.
mkuu unaweza ukawa upo sahihi, lakini hebu nitajie tu mkurugenzi mmoja katika shirika la nssf aliyemtangulia Dr. Ramadhani Dau aliyewahi kufikia mafanikio haya? na shauri ushabiki na udini tuweke pembeni.
 
Hivi Mkurugenzi wa NSSF huteuliwa na rais?

Je, rais ni mwanachama wa NSSF pia?.?

Kama sio mwanachama kwa nini wakurugenzi wanajipendekeza kwake na sio kwa wanachama??

Wewe huna akili kabisa, Hiyo miundombinu na uboereshaji wa makazi ni kujipendekeza kwa Rais? Ulitaka nae awe na kashfa za kuficha pesa nje ili uone hajipendekezi? Kichwa chako kimeumbwa kuhifadhi Mapunye kwenye bongo yako!
 
Kwanini NCCF WASINGEWAJENGEA WANACHAMA wao kwanza nyumba za bei nafuu kuliko kuwaacha wakihangaika huku pesa zao ya makato yakitumika kunufaisha wengine. Ni vizuri kama wangejenga nyumba kwa wanachama halafu wakawauzia au kuwapangishia kwa gharama nafuu. Mwanachama angepata unafuu na kunufaika na chama kwa upande wangu nilidhani watu muhimu kwanza ni wenye chama halafu unaelekeza mikakati mingine kwa kwingine. Utaachaje nyumba yako ikiungua na kukikimbilia kuuzima wa jirani.
mkuu ni nani hasa mwanachama wa nssf? mimi nilikuwa mwanachama, nikatoka, nikarudi na sasa natarajia kutoka. kwa kifupi kila mtu either ni mwanachama wa nssf either mstaafu, mtarajiwa au active. think wide, hili ni jukwaa la maGT
 
Mwakani lazima Nikombe pesa yangu yote, make kwa hizo project haziwezi fanikiwa bila kwanza kuondoa fao la kujitoa
sishangai wewe ukawa graduate wa UDOM au umeishi mabibo hostel, chuo cha hombolo et al. ambazo zimejengwa na NSSF. utafikiri ana kichwa kumbe ni kifuu cha nazi kipo juu ya shingo.
 
Hivi wadau kwa kutumia akili ya kawaida ni kweli uwepo wa bandari na shughuli ndiyo chanzo kimojawapo kinachohusika na msongamano Dar??? bandari inatumia njia zipi kwa ajili ya shughuli zake??? Hizo fedha kwanini zisitumike angalau kuhamishia baadhi ya ofisi za serikali kwenda Dodoma?? Tutatapanya fedha nyingi sana kwenye ujenzi wa njia za juu. .... mabasi ya kwenda kasi.....na siasa nyinginezo za ujenzi lakini mwisho wa siku tutajikuta tunaongeza matatizo mengine......
ujinga unakusumbua. NSSF inawekeza. sasa kuhamisha makao/ofisi kwenda dodoma kutarudisha vipi hizo hela. ukimwona utafikiri anakichwa kumbe ni kifuu cha nazi.
 
Hivi hii NSSF wanachama wake wako DSM tu! Daraja la Kigamboni DSM, Nyumba za bei nafuu DSM, Reli DSM, Bandari kavu DSM Ooops Kisarawe? Je wanachama wa mikoa mingine hutataki hizo nyumba za bei nafuu?

Halafu nani amempatia mamlaka hayo ya kutumia pesa zetu atakavyo? Wanachama tunachotaka ni kuboresha formulae ya kukokotoa mafao ya uzeeni yafanane fanane na ya PSPF.

Sijui hili suala tunaweza kuli solve vipi kwenye katiba mpya? Mkurugenzi wa NSSF na mifuko mingine ya jamii achaguliwe na wanachama wenyewe badala ya kuteuliwa na RAIS ambaye yeye ni mwanachama wa PSPF.

Hivi hela zetu (NSSF) tulizotumia kujenga UDOM serikali imeshaanza kuturudishia?, Maana report ya CAG ya 20012 inaonesha Serikali imeshindwa kurudisha hiyo pesa na mifuko hiyo (NSSF, PPF) iko taabani kifedha na ndiyo ulikuwa mwanzo wa muswaada ule wa kuzuia FAO LA KUJITOA.

Kama ni hivyo kwanini Dr. Dau aendelea kuifadhili serikali ambayo it is a bad DEBTOR. Huyu Dr. Dau kwanini anajipendekeza sana kwa serikali at the expense ya michango ya wanachama?
unaongea as if wewe peke yako ndo unachangia pale NSSF. na si shangai wewe ukawa graduate wa udom. kwa kweli mimi kwa haya wayafanyao nakubaliana kabisa nao, japokuwa najua watendaji wa nssf hasa hawa wa chini ni wasumbufu sana. tanzania tuko nyuma sana kimaendeleo, kwa hiyo hatuna budi kutumia kila opportunity tuipatayo. otherwise we are finished.
 
..serikali imeamua kujenga bandari BAGAMOYO.

..mradi wa bandari ya nchi kavu Kisarawe ni wa nini?
 
Watu wanaoishi MANZESE na VINGUNGUTI wataenda WAPI? Isije Ikatokea kama SLAMs za NAIROBI kwa Wananchi kufukuzwa kwenye VIWANJA halali...

Kwanini kila kitu KISARAWE??? BANDARI MPYA ITAKUWA HUKO as WELL
Kwanini wasingesogea CHINI KULIA kwa BANDARI yetu IPO LINDI inahitaji MAENDELEO Oh LINDI ni kwa MAMA; Kisarawe kwa BABA... Mmmmmmmmmm
 
ujinga unakusumbua. NSSF inawekeza. sasa kuhamisha makao/ofisi kwenda dodoma kutarudisha vipi hizo hela. ukimwona utafikiri anakichwa kumbe ni kifuu cha nazi.
Naona uliamka vibaya leo mkuu....msongamano Dar ni tatizo...kiuchumi ,kijamii. Kikwazo cha serikali kuhamia Dodoma tunaambiwa ni gharama. NSSF pia ina wajibu wa kutoa huduma hasa pale kwenye tatizo. Nilichotaka kusema kama imeweza kuikopesha serikali katika miradi kadhaa...haiwezekani pia kufanya hivyo kupunguza hili tatizo???.........
 
Naipongeza NSSF kwa mpango mzuri wa kuboresha jiji, lakini huu mpango wa kuboresha uswahilini unatia mashaka kwa sababu fidia watakazolipa zitakua ndogo sidhani kwa nyumba ya kawaida itafika hata 50M wakati NSSF ikishajenga itakwambia nyumba ya gharama nafuu wanauza 100M kama wanavyotufanyia sasa NHC wanasema wamejenga appartment za gharama nafuu ukiuliza bei unaambiwa 100M Je mtanzania gani ataweza nunua hizo nyumba km sio wafanyabiashara halafu watupangishe kwa USD.

Mtanzania aliyefidiwa 50M leo baada ya miaka 2 mradi ukikamilika atakua amebakiza pesa kidogo hataweza kunua hizo nyumba hata akiambiwa alipie nusu bei.

Watumishi wa umma wengi hatutaweza hata tukikopa kwa sababu zaidi ya 80% ya mafao yataishia kulipa deni la nyumba tutastaafu tukiwa na pesa kiduchu!
 
Gazeti la mwananchi leo: NYUMBA ZA BEI NAFUU NSSF NI SH200 MILIONI. Zimejengwa ili kuwauzia wanachama wake kwa bei nafuu eneo la Kijichi Dar. Je kuna huwino wa haya yaliyosemwa ZNZ?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom