FRANCIS DA DON
JF-Expert Member
- Sep 4, 2013
- 35,835
- 40,430
Hapa Dar es Salaam kila baada ya mita 2 au 3 kuna ndoo ya maji safi yenye koki ya kunawia pamoja na sabuni ya kubonyeza kwa ajili ya kutakasa mikono, na unaweza kuitumia huduma hiyo ya kunawa popote na muda wowote bila hata kumuuliza mwenye eneo husika.
Kwakuwa njia kuu hasa na ya uhakika ya kusambaa kwa virusi vya Corona ni kupitia mikono nadhani hii imesaidia sana hapa Dar watu wasife kwa maelfu kwa siku kama huko Marekani, unless Marekani haina uwezo wa kifedha wa kununua ndoo milioni kadhaa za kunawia ndani ya siku chache, nawashauri waige utaratibu huu wa kuweka ndoo za kunawia mitaani kama tulivyofanya Dar.
Pia jambo lingine linalotusaidia Dar kwa sasa ni hili la kuvaa barakoa kwa lazima, inaonekana kule Marekani barakoa ni ghali sana na kuna hatari ya watumishi wa afya kukosa barakoa endapo itatangazwa lazima kuvaa barakoa kabla ya kutoka nje.
Ndio maana wakasema kuvaa barakoa ni kwa wanaoumwa tu, lengo lao ni ili kuwaokoa watumishi wa afya ili wasikose barakoa, nitoe wito kwa serikali ya Marekani kuruhusu watu wajishonee barakoa zao wenyewe na iwe lazima kuvaa kabla ya kutoka nje.
Ifahamike kwamba unapokohoa ile barakoa inasaidia virusi visiende mbali.
Kwakuwa njia kuu hasa na ya uhakika ya kusambaa kwa virusi vya Corona ni kupitia mikono nadhani hii imesaidia sana hapa Dar watu wasife kwa maelfu kwa siku kama huko Marekani, unless Marekani haina uwezo wa kifedha wa kununua ndoo milioni kadhaa za kunawia ndani ya siku chache, nawashauri waige utaratibu huu wa kuweka ndoo za kunawia mitaani kama tulivyofanya Dar.
Pia jambo lingine linalotusaidia Dar kwa sasa ni hili la kuvaa barakoa kwa lazima, inaonekana kule Marekani barakoa ni ghali sana na kuna hatari ya watumishi wa afya kukosa barakoa endapo itatangazwa lazima kuvaa barakoa kabla ya kutoka nje.
Ndio maana wakasema kuvaa barakoa ni kwa wanaoumwa tu, lengo lao ni ili kuwaokoa watumishi wa afya ili wasikose barakoa, nitoe wito kwa serikali ya Marekani kuruhusu watu wajishonee barakoa zao wenyewe na iwe lazima kuvaa kabla ya kutoka nje.
Ifahamike kwamba unapokohoa ile barakoa inasaidia virusi visiende mbali.