Dar. darasa la saba wamemaliza mtihani majibu bado harusi zimechukua nafasi.

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
18,657
22,252
Hivi karibuni watoto wa darasa la saba walimaliza kufanya mtihani wa kuingia kidato cha kwanza, kama kawaida maeneo mengi ya Dar. kila baada ya mtihani harusi za watoto hao huanza, ni mavuno mitaani kwetu. Inaelekea serikali huwa hsiwaandai viongozi wa serikali za mitaa kuhusu kuzuia harusi hizo ambazo huenda baadhi ya watoto hao watafaulu kuingia kidato cha kwanza. Tusimpe kazi Mwanri (najua yuko Tabora) ya kuanza kusukuma ndani wachagua mchele, wapiga ngoma, mashangazi, wajomba, waoaji na wanaoolewa, serikali ianze kuzuia sasa ingawa tayari imechelewa.
 
Hivi kuna watu wanaoa watoto wa darasa la 7??
Kweli hii dunia kuna mambo mengi sana siyafahamu😭😭
 
Naomba nikufahamishe kuwa,mtoto (mwanafunzi) anaingia kwenye chumba cha mtihani akiwa tayar ameshapangwa na wazazi wake kuwa "hakikisha unafeli kwenye mitihani yako" so,mwanafunzi ata-shade majibu ya uongo kwenye OMR (Optical Mark Reader)
Kwa hiyo,mpaka wanaandaa harusi wanakuwa na uhakika kuwa huyo mtoto hatafaulu!
 
Muulize Mwanri huko Tabora yeye hukamata na kusukuma ndani kuanzia mchagua Michele mpaka mcheza ngoma na maharusi wao.
 
Back
Top Bottom