Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,114
- 35,120
Kuna kila dalili kuwa hakuna mwanasiasa kutoka upinzani ambaye alihamia CCM ili kuunga mkono juhudi (maarufu kama wasaliti) mwenye nafasi ya kupenya katika kinyang'anyiro kinachoendelea sasa cha kura za maoni ndani ya CCM kwenye ngazi yoyote ile, iwe ubunge, udiwani au viti maalum. Wasaliti wote huenda wataangukia pua asubuhi na mapema.
Namna pekee ya wasaliti hao kuvuka hicho kikwazo ni kusubiri huruma za mwenyekiti za kuwabeba mezani na kuwateua kibabe, jambo ambalo linaonekana kuwa na nafasi finyu sana katika mazingira yaliyopo sasa.
Namna pekee ya wasaliti hao kuvuka hicho kikwazo ni kusubiri huruma za mwenyekiti za kuwabeba mezani na kuwateua kibabe, jambo ambalo linaonekana kuwa na nafasi finyu sana katika mazingira yaliyopo sasa.