Zifahamu dalili zinazoashiria mwanamke ni mjamzito

niwaellyester1

Senior Member
Sep 7, 2010
123
19
Early-Symptoms-of-Pregnancy.jpg

Eti mimba inaanza kuonekana muda gani baada ya kuingia? yaani kama ikiingia leo, baada ya muda gani ndiyo itaonyesha kuwa ni positive?


MASWALI YA WADAU WENGINE KUHUSU DALILI ZA MIMBA
Helow,

Ni nini kinasababisha matiti kuwasha na chuchu kuuma, je ni dalili za ugonjwa na kuna tiba ya tatizo hili?

Msaada tafadhali
Habari za jioni wana JF,

Naomba kujua ni muda gani mwanamke huweza kuhisi ana mimba tangu siku alipojamiiana na mwanaume akiwa katika siku zake za hatari.

Je, ni siku mbili baadae au wiki kadhaa?

Naomba msaada wenu.
Habari zenu,

Nimefanya mapenzi katika siku za hatari ila jamaa alimwaga nje. Sasa ni wiki imepita naskia tumbo linauma na chuchu zinauma ingawa matiti hayajavimba.

Je, inaweza ikawa ni mimba?
Wakuu, heshima yenu.

Nina mpezi wangu ambaye siku za karibuni alinijulisha kuwa anaujazito wangu lakini umetokea kwenye mazingira ambayo siyaelewi kabisa.

Tulifanya mapenzi tarehe 23/7 alikuwa siku za hatari yani siku ya 12 mzunguko wake ni siku 28 nikamuomba tutumie kinga akagoma akasema yeye mwenyewe anajua hawezi pata mimba anajua anachofanya nikamwini basi tarehe 1/8 akanijulisha anaujazito wangu nikamwambia wewe uliniambiaje?

Nilichokuja kuuliza huku ni kuwa Mimba inachukua siku ngapi mpaka ionekane kwa vile vipimo vya kujipima mwenyewe nyumbani?

> Pia kwa siku hizo ni kweli zinaonyesha dalili kuwa mimba ni yangu au nimebambikiwa


NB: Naomba usinitukane nipe ushauri tu Asante.
Naomba msaada. Nimeona dalili hizi na ningependa kujua endapo ni dalili za ujauzito.

1. Kula kupita kiasi
2. Kuchagua chakula
3. kutopenda harufu ya mafuta
4. Kichefuchefu asubuhi
5. Kuhisi joto

Kama si dalili za ujauzito ni dalili za nini?
Habari ndugu zangu.

Ninaomba kujuzwa. Nina ujauzito wa mwezi mmoja kuna wakati kitovu kinauma na jana wakati naoga ktk harakati zavkujiswafi nimeona dalili za damu kidogo na sometimes nafeel km nataka kuingia Mp. Je, hii ni sawa?

Thanx in advance.


MICHANGO YA WADAU
Mwanamke anapopata ujauzito kwa kawaida huwa anaanza kuona dalili ambazo si za kawaida

Na ni wakati huo ambao ni muafaka kwake kuanza kuuchunguza mwili wake.

Homoni zinazosambaa mwilini mara tu unapopata ujauzito husababisha mabadiliko kadhaa mwili ambayo yanaweza kugundulika kabla hata ya uchunguzi halisi kujua kama una ujauzito au la, anasema Melissa Goist, Profesa na Mtaalamu wa Masuala ya Uzazi wa Chuo Kikuu cha Ohio, Marekani.

Maumivu kwenye matiti
Hii ni dalili ya kawaida ya ujauzito ambapo nguvu za homoni mwilini huongezeka wakati yai linavyopata rutuba jambo ambalo huongeza wingi wa damu na kuyafanya matiti ya mwanamke kuvimba na kuwa makubwa isivyo kawaida.

Maumivu mwilini
Utaanza kusikia maumivu kama vile unataka kuingia katika siku zako. Kwa kawaida hali hii hutokea wakati yai likiwa linasafiri kwenda katika chumba cha mimba. Hivyo, hali hiyo husababisha sehemu hiyo itanuke taratibu na kusababisha maumivu hayo.

Kutokwa damu bila kutegemea
;Wanawake wengi hufikiria kutokwa na damu kidogo ni dalili ya kuwa katika siku zao. Lakini, katika hali halisi, kutokwa damu kusikotegemewa, huwakumba asilimia 25 ya wanawake wakati wa kurutubika kwa yai," anasema Goist. Anaongeza kwamba iwapo utaona hedhi yako inakuwa fupi au inafanyika katika hali ambayo si ya kawaida, unashauriwa kwenda kufanya kipimo cha ujauzito.

Kuchoka
Unapojisikia kuchoka na kukosa raha, au kutaka hata kulala wakati ukiwa kazini, lazima ufahamu kwamba mwili wako unajirekebisha kuingia katika kipindi kipya cha mabadiliko.

Tambua kwamba katika kipindi cha mwanzo cha ujauzito ni muda ambao mtoto tumboni huanza kutumia sehemu ya nguvu zako na hivyo kukuletea uchovu na usingizi," anasema Goist.

Chuchu kuwa nyeusi
Chuchu huanza kubadilika rangi yake kutokana na chembechembe za uhai (seli) kuanza kufanya kazi kwa nguvu zaidi. Hata hivyo, Goist anasema: Wanawake wenye ngozi nyeusi hawawezi kuiona dalili hii mapema hadi muda wa kama wiki kumi zipite."

Kichefuchevu
Hali hii huwapata asilimia 85 ya wanawake wanapopatwa ujauzito, ambapo nyakati za asubuhi ndipo hasa hujionyesha.

Mwili kuvimba
Kuna wakati kupungua kwa nguvu za uyeyushaji chakula kunaweza kukusababishia kuona tumbo limevimba na nguo zikawa zinakubana kutokana na chakula kujaa katika utumbo. Lakini hali hiyo ikiendelea, na ukaona siku zako haziji, basi ni vyema ukatambua kwamba tayari una ujauzito, na kinachokupasa ni kwenda kuhakikisha.

Kwenda haja ndogo mara kwa mara
Kwenda haja ndogo kila mara ni dalili kwamba kibofu chako kimeanza kufanya kazi ya ziada, ambapo huwa kinafanya kazi ya kuondoa maji kwa uthabiti zaidi wakati wa ujauzito. Hali hii pia hujitokeza mwishoni mwa ujauzito, ambapo kibofu kitakapokuwa kinarudia hali yake ya kawaida baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu.

Tamaa ya vitu mbalimbali
Kutokana na mwili kuwa na ;mzigo wa ujauzito na hivyo kuchoka, hali hiyo humfanya mwanamke kutamani vitu mbalimbali ili kukidhi mabadiliko yaliyojitokeza katika mwili wake. Hii ni pamoja na kutaka, kwa mfano, aina fulani ya vyakula, au kufanya mambo ambayo hapo nyuma alikuwa hayapendi.

Kuumwa kichwa
Kuongezeka kwa damu kunaweza kusababisha kichwa kuuma japokuwa si sana, hususan katika wiki za mwanzo za ujauzito. Hata hivyo, hali hii hukoma mwili unapojirekebisha na mzunguko wa homoni unaotokana na ujauzito.

Kufunga choo
Homoni ambazo husababisha mwili kuvimba pia husababisha kufunga choo kutokana na mfumo wa kuyeyusha chakula kutofanya kazi vyema. Hata hivyo, hali hii inaweza kujitokeza zaidi wakati ujauzito unaendelea kukua.

Kuwa na hasira
Kutokana na kuongezeka kwa homoni za utendaji kazi mwilini, hali hiyo itakusababishia uchovu, na kukufanya kuwa na hasira, anasema Goist

Kuongezeka kwa joto mwilini.
Kipimo cha joto la mdomo ni muhimu katika kutambua hali ya ujauzito. Kwa kawaida joto huongezeka kwa nyuzi moja au zaidi wakati yai likiwa linatunga mimba. Hali hiyo ikiendelea kwa zaidi ya wiki mbili, itakuwa inaonyesha dhahiri kwamba kuna mtoto anakuja
Vipimo tunavyotumia ni crude na vinachukua muda mrefu kupata matokeo

Kwa kwetu Tanzania, hatuko that much sophisticated interms of diagnostic facilities, vipimo tunavyotumia ni crude na vinachukua muda mrefu kupata matokeo. Kwetu kipimo tunachotumia cha UPT (urine for pregnancy test) kitakuwa positive siku ya 8 ( kama wiki moja hivi) mpaka ya 11 (roughly 2 weeks) baada ya missed period. Tunatumia pia USS (Ulatrasound), ambayo nayo itaona mimba (intradecidual gestation sac - kifuko cha mimba) wiki ya 4 mpaka ya tano ya ujauzito.

Kama uko Ulaya mimba yaweza kuwa diagnosed 5 days before the first missed period, yaani siku ya 9 since conception [tangu mimba kutunga na sio tangu kukosa siku zako-tofauti na UPT ambayo inakuwa positive siku 8 (roughly one week) baada ya kumiss period na sio baada ya conception, kwa sababu conception hutokea siku 14 kabla ya next menstruation] kabla hata hujakosa siku za mzunguko unaofuata, wanatumia vipimo kama ELISA na vingine.

Jaribu kurudia UPT on the 7th or 8th day since your first day of the last missed menses, na pia kama ni negative rudia siku ya 11, kama itakuwa negativu tena, TRY AGAIN next time you might succeed.
Kujua wakati una mimba

Wanawake wengi hujua wameshika mimba aghalabu wiki 3 baada kushika mimba. Mwili wenyewe utakuonyesha/utakutabiria kama:
  • Hedhi yako itakoma/itakuwa nyepesi
  • Utasikia uchefuchefu/utatapika (ugonjwa wa asubuhi morning sickness na inaweza kutokea wakati wowote wa siku pia).
  • Matiti yako yataanza kuwasha, kufura au yataanza kuwa makubwa.
  • Chuchu (ncha ya titi) na sehemu zilizokaribiana zitaanza kuwa nyeusi na zizizoweza kuvumilia.
  • Itakubidi kwenda haja ndogo mara kwa mara.
  • Utasikia uchovu
  • Kusokotwa na tumbo
Kama umeona baadhi ya dalili hizo, unaweza kuwa na mimba. Pata jaribio/uchunguzi kipimo cha mimba ili kupata yakini! Unaweza pimwa bure katika kliniki iliyokaribu nawe au ununue kifaa vya kujipmia nyumbani kutoka duka la dawa. Daktari wako anaweza kukupima pia au atakuelekeza kwa mtaalamu kama hauna.

Vipimo vya mimba

Vipimo hivi huchunguza kuwepo kwa Human Cherionic Cronadotropin (HCG) kwa mkoja au damu. HCG wakati mwingine hitwa Pregnancy Hormone na huwa kwa mwanamke tu wakati ana mimba. Kuna aina mbili ya vipimo: kipimo cha mkojo na kipimo cha damu.

Kipimo cha Mimba cha Mkojo
Wanawake wengi hutumia kipimo hiki ambacho pia huitwa cha nyumbani (HPT-home pregnancy test) kwa sababu ni rahisi kutumia na bahasa (rahisi kibei) kuna aina nyingi za vipimo hivi. Kwa kimoja, utakwanya mkojo wajo kwa kikombe na kukitumbukiza kijiti huko na kwakingine utaweka kijiti hicho kwenye viungo vya mkojo. Njia iliyobora ni itakayokuonyesha kiwango cha HCG, hivyo tafuta moja katika kiwango cha hCG kutoka 15 hadi 30. Utasaidiwa na mhudumu wako dukani la dawa au kliniki.

Vifaa hivi hufaa kwa asilimia 97-99 kuyakirisha uwepo wa mimba vinapotumiwa ipasavyo. Hivyo kufuata maagizo ni muhimu. Pia angatia wakati wa kuharibika wa kifaa kwani kifaa kilichoharibika hakitakupatia matokeo unayotarajia.

Kama utapata matokeo yasiyofaa/yasiyo hakika
Kama utajipima/utapimwa bado kidogo*, unaweza kuona kwamba hauna mimba ili hali unayo. Aina nyingi ya vipimo vya nyumbani hukushauri ujipime baada ya siku kadha bila kujali matokeo uliyopata awali. Kama unaendelea kupata matokeo yasiyofaa nab ado unashuku una mimba, ongea na daktari/mkaguzi afya waka.

Kama utapata matokeo yafaayo/ya hakika
Kama utapata matokeo ya hakika, fanya miadi na mkaguzi afya wako punde tu. Mkaguzi wa afya yako atayakinisha kama una mimba kupitia kipimo cha damu na ukaguzi mwingine (pelvic exam) na atakwambia chaguzi uliza nazo.

Kipimo cha Damu
Kama wataka kipimo cha damu badala ya kite cha nuymbani, fanya miadi na mkaguzi afya wako/dakatari wako.
Baadhi ya dalili za nje zinazoonyesha uwezekano wa kuwa na mimba
  • Maziwa kujaa na kuwa magumu kidogo.
  • Kunenepa ghafla kutokana na kuongezeka vikoleza mimba mwilini.
  • Mabadiliko kitabia ya ghafla yasiyozoeleka.
Soma hizi dalili 10 za mimba ili ikusaidie kupata uhakika

Hutokea mara nyingi kina mama na wasichana kuwa na kipindi cha msongo wa mawazo pale wanapokosa siku zao na hasa kama hawakutumia njia ya uzazi wa mpango au kinga nyingine ya kushika mimba.

Kukosa siku zako sio dalili pekee ya kushika mimba, bali kuna dalili zingine utalazoziona. Kuna sababu nyingine nyingi zinazoweza kukufanya ukose siku zako, hivyo soma dalili za mimba ili ikusaidie kupata uhakika.

Moja, ni mabadiliko katika siku zako. Hii kitaalamu tunaita spotting. Unaweza kushika mimba ukaendelea kuona damu mwezi huo. Hii hutokea yai lililorutubishwa linapojipandikiza kwenye kizazi. Mishipa ya damu iliyojaa kwenye ukuta huu tayari kulisha kiumbe huachia damu kidogo amabazo mwanamke anaweza kufikiri ni hedhi yake ya kawaida. Hata hivyo mabadiliko yataonekana kwani kiwango na siku za damu hubadilika.

Pili, ni kuongezeka ukubwa na kupata maumivu kwenye maziwa. Hii inasababishwa na ongezeko la homoni za istrogen pale unapokuwa umeshika mimba. Hali hii huisha katika kipindi cha miezi mitatu ya kwanza.

Tatu, ni kichefuchefu na kutapika. Hali hii huwa mbaya zaidi wakati wa asubuhi unapoToka kulala. Hii ni kwa sababu ya homoni ya projestroni ambayo husababisha kupungua nguvu kwa misuli ya mrija wa chakula au koromeo.

Nne, ni uchovu usiokuwa na usingizi usiokuwa na sababu. Hii hutokea kwa sababu ya ongezeko la homoni ya projestroni na mama utajikuta unasinzia mara kwa mara. Hali hii huisha unapoanza mwezi wa nne wa mimba ila hata kipindi cha mwisho wa mimba hujisikia uchovu.

Tano, kusumbuliwa na harufu mbalimbali. Hasa kama unapata mimba kwa mara ya kwanza, utachukia harufu za vyukula na vinywaji mabalimbali. Wakati mwingine hata harufu za watu walio karibu nawe zinaweza kukukera.

Sita, ni kujaa gesi tumboni. Utaona baadhi ya nguo zako zinakubana zaidi hasa sehemu ya tumbo. Hii ni kwa sababu ya homoni nyingi mwilini zinazokufanya kijisikia tumbo kujaa.

Saba, Kukojoa mara kwa mara. Hii kwanza hutokana na kuwa na damu nyingi mwilini ambayo huongezwa na homoni za ujauzito makusudi kutoa rishe ya kutosha kwako na kwa kiumbe tumboni. Ukiwa na damu nyingi pia utakojoa sana za kikemia mwilini. Pili utajisikia kwenda haja ndogo mara nyingi pale kiumbe kitakapoongezeka na kubana kibofu cha mkojo.

Nane, kuongezeka kwa joto la mwili. Kwa kina mama ambao hupima joto lao kama njia ya uzazi wa mpango, watagundua kuwa joto limepanda kwa muda wa wiki mbili au mbili na nusu mfurulizo.

Tisa, kutoona siku sako kabisa. Kwa wale ambao siku zao hazibadiliki na huenda vizuri yawezekana kugundua pale wanapokose siku nap engine kukimbilia hospitali. Hata hivyo kwa wale ambao siku zao hubadilika sana wataona kawaida ila kama ameshika mimba taona mchanganyiko wa kichefuchefu, uchovu na kusinzia pamoja na kukojoa mara kwa mara.

Kumi, kupima mkojo kwa kutumia kipimo cha karatasi ngumu. Famasi nyingi huuza vipimo ambavyo ikikichovya kwenye mjojo wako huweza kugundua homoni za mimba kwenye mkojo.

Hii unaweza kupima mwenyewe ukiwa nyumbani hata kazini. Kipimo hiki ukisha kichovya kwenye mkoja kama katatsi inavyoelekea utaona mistali baada ya dakika moja inajitokeza upande wa chini.

Ikitokea mistari miwili basi unaweza kuwa na mimba na ukitokea mmoja utakuwa huna mimba. Kilingana na kiwango cha homoni mwilini, kuna kina mama hakionyeshi majibu mpaka upitishe wiki moja bila kuona siku zako.

Pamoja na dalili hapo juu, unatakiwa kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa daktari.
Ukitaka kuziona dalili za awali za mimba ni kama utakuwa mrahisi kunotisi yafuatayo

Kuna muda mwanamke anapata mimba na bado anakuwa anapata siku zake hadi miezi mitatu au zaidi. Hii ni kisomi zaidi.

Mwanamke anapokaribia kujifungua ndio rangi ya chuchu huanza kubadilika na kukua/kuvimba.(maana yake ni kwamba maziwa yapo njiani tayari)

Ukitaka kuziona dalili za awali za mimba ni kama utakuwa mrahisi kunotisi yafuatayo:

* Ugumu wa tumbo la mwanamke
* Kitovu kukua/kuvimba ama kuwa na uchafu mara kwa mara
* Mood swing (atakuwa mkali au affectionate zaidi ya kawaida,kukasirika na kununa bila sababu)
* Uke kuwa na ute flani hv mwembamba (yani pako lubricated mda wote)
* Joto kupanda kiasi flani
* Uchovu/uvivu
* Appetite changes

Ila kubwa zaidi ni ww mhusika kujua kalenda ya mwanamke wako na kujua siku mnazokutana. Hapo kama ni ulitaraji mtoto utaanza kufatilia changes na kupima mkojo ila kama ilikuwa ni unexpected utaweza tambua baada ya wiki tatu ambapo dalili za hapo juu huanza kuonekana kwa mbali (mwanamke ambaye ana kaujauzito huwa mnapokutana kimwili utaona mood yake inakuwa kubwa zaidi tofauti na kawaida).

Wanawake hutofautiana hvo hamna direct formula ya kuziona dalili za awali.


ZAIDI, SOMA:

Dalili za kwanza za mimba
Je, nina mimba?

Kuna baina ya wanawake wenye huonyesha dalili za mimba punde tu katika wiki kadhaa baada ya kushika mimba. kuna maswala mengi Kuhusu upataji mimba na ni siku gani mwanamke anaweza kupata mimba. Hebu tujadiliane kwa ufupi. Hedhi yaani mensturation period, ni wakati mwanamke anaweza kujua ya kuwa hana mimba.

Damu inayotoka wakati huu huwa nyekundu. Damu hii hutoka kila mwezi kwa wanawake walio na mzunguko wa kawaida. Pia damu hii huchukua siku tatu hadi tano kwa wale wenye mzunguko wa kawaida. Unapokosa hedhi, haswaa wakati umeshirikiana ngono, Kuna chanzo kubwa ya kuwa umeshika mimba.

“Kukosa Hedhi ni chanzo cha maisha”
Ni vyema kujua jinsi ya kujichunga ili wewe na mwanawe muwe salama. Hata kabla ukose hedhi (mensturation/period) Unaweza kudhani au kutumai una mimba. Tumaini Ni kwa wale waliooleka au wanaopenda kupata watoto. Wakati mwingine, Mimba huja na hofu, haswaa ukiwa umefanya ngono kando ya ndoa. Lakini usitie shaka, mtoto ni baraka na ni lazima na wajibu wa kila mzazi kujua wanapotarajia mwana.

Dalili za mimba kwa wanawake wengi huonyesha katika wiki za kwanza wanapopata mimba. Hizi dalili ni tofauti kwa kila mwanamke. Kuna wale ambao huwa na machungu na magonjwa zaidi ya wengine na kuna wale wanaopitia hali hii kwa njia rahisi mno.

SWALA NYETI!
Swali ambalo kila mwanamke anaweza kuwa nalo ni, Je ninaweza kushika mimba wakati nina hedhi?
Jibu la hakika ni Ndiyo! Ingawaje wanawake wengi hawawezi kushika mimba wakati wana hedhi, Kuna baina ya wengine wanaoweza kushika mimba wakati wanashirikiana ngono wkati wana hedhi. Hii si kawaida kwa wengi lakini kulingana na dakitari Jeannnette Lager, M.D, MPH aliyesomea maumbile ya wanawake, anatuelea jinsi mwanamke anaweza kushika mimba wakati ana hedhi sana sana kwa wale walio na mzunguko fupi zaidi yaishirini na nane au zaidi.
Haya basi hebu tufafanue zaidi juu ya ugunduzi ya kuwa umeshika mimba.

Dalili zifuatazo ya mimba ni maagizo tu ya kuelewa jinsi unavyoweza kukumbatia hali yako ukiwa na mimba.
  • Kukosa Hedhi (Missed Period)
  • Utoaji damu mwepesi (light spotting/implantation bleeding)
  • Kufura kwa Matiti (swollen Breasts)
  • Mhemko wa hisia (Mood swings)
  • Kutoa hewa ( lots of gas)
  • Kutapika au kuhisi kutapika (Nausea and vomiting)
  • Kufura tumbo (bloating)
  • Kukojoa kila wakati (frequent urination)
  • Constipation (Kuvimbika)
  • Mgongo kuuma Upande wa chini (lower back pain)
  • Kuumwa kwa kichwa (headache)
  • Kuzidi joto (increase of basal temperature)
  • Uchovu (fatigue)
  • Kutamani aina ya vyakula (food cravings)
  • Kulia (crying)
  • Kulala muda kwa muda (sleepiness)
Urahisi na kufura Matiti
Matiti yako yanaweza kuonyesha dalili za kwanza ya mimba. Wiki mbili baada ya kupata mimba, mabadiliko ya homoni yanaweza kufanya matiti yako kuwa makubwa kuliko kawaida, unaweza kuhisi kujikunakuna na uchungu kiasi, pia unaweza kuhisi kama matiti yako yamejaa au nzito.

Uchovu
Uchovu umekuwa hali na dalili ya kwanza mno kwa wanawake wajawazito. Homoni inayoitwa Progesterone huongezeka kwa wingi na inaweza kukufanya kuhisi usingizi kila wakati. Pia upunguzaji wa sukari katika damu, upunguzaji wa shinikizo la damu (blood pressure) na uzidishaji wa damu unaweza kukufanya uwe mchovu wakati wa mimba.

Utoaji damu mwepesi na machungu kwa tumbo ya uzazi
Kuna wakati, damu mwepesi (spotting) huwa dalili ya mimba mapema. Damu hii huwa nyepesi mno na haiwezi kulinganishwa na ule wa hedhi. Rangi ya damu hii ni waridi au kahawia kulingana na hali ya mwanamke. Wakati mbegu ya mwanamume na ule wa mwanamke yamekutana kumtengeneza mtoto, mwanamke anaweza kutoa damu nyepesi kuonyesha ya kwamba mwana amelazwa vyema katika tumbo la uzazi wa mwanamke.

Damu hii huchukua siku chache sana kutoka kulinganishwa na ule wa hedhi. Kuna wanawake wengine wenye hukosa kuonyesha damu hii mwepesi wanapopata mimba. sio lazima wanawake kutokwa damu wanaposhika mimba. ni muhimu kuelewa ya kuwa mwili ya kila mwanamke ni tofauti. Pia, machungu katika tumbo la uzazi wakati mimba hutengenezeka, unaweza kufanana na ule wa hedhi.

Damu [ni damu] si kitarasa”
Kuhisi kutapika au Kutapika
lazy_placeholder.gif
Ugonjwa wa asubuhi (morning sickness) unaweza kufanyika wakati wowote wa siku. Kuna wanawake waliosemekana kubebaa mimba ambao huwa na ugonjwa huu hivi punde wanapoamka, kuna wengine wanaopata ugonjwa huu wakati wa mchana na wengine wakati wa usiku. Kila mwanamke ana utofauti kulingana na maumbile ya mwili wake.
Wanawake wengi kwa jumla hupata (morning sickness) wiki mbili wanaposhika mimba. Kutapika huwa matokeo ya homoni inayoitwa estrogen inapoongezeka mwilini. Kuna wanawake wengi ambao hunusa harufu za aina mbali mbali, kama vile marashi, vyakula mbali mbali kama mayai, kwa haraka na pia harufu zingine huwafanya kuhisi kutapika au huenda kutapika.

Ukiwa unahisi kutapika, unaweza kula au kunusa ndimu au kukula matunda kama ndimu, Mizizi kama tangawizi na pia kuhakikisha una kunywa maji mengi kwa wakati huu. Kuna wanawake wengine husema wanaweza kuhisi ladha ya chuma ulimini mwao. Haya yote ni kwa sababu homoni estrogen imeongezeka mwilini juu ya kushika mimba.

Kutamani Vyakula vya aina aina au Kukataa hivi vyakula
lazy_placeholder.gif
Ukiwa umeshika mimba, unaweza kujipata una hisia ya vyakula fulani, ilhali kuna vyakula mbali mbali ulivyopenda sasa hutaki kuviona au kuvinusa.

Kuna wanawake wengi waliopenda mayai na sasa hata harufu ya mayai huwafanya kutapika. Na kuna wale wanaoanza kupenda matunda au vyakula vya aina mbali mbali wanapokuwa wajawazito.

Haya yote ni kwa sababu ya mabadiliko ya homoni mwilini, haswa kwa muhula wa kwanza (Mwezi moja hadi tatu) ya mimba. Pia unaweza kuhisi njaa wakati wowote wa siku. wanawake wengi ulimwenguni huanza kukula zaidi ya kawaida na hii ni ishara kubwa ya kwamba mwanamke amepata uja uzito.

Kuumwa kwa kichwa
lazy_placeholder.gif
Wakati unapopata mimba, uongezaji wa damu ni haswaa. Ndipo Kichwa kuuma muda kwa muda. Ni muhimu kupumua hewa safi na kupunguza kazi ya kimwili ili uweze kupumzika kila wakati.

Kuvimbiwa (constipation)
lazy_placeholder.gif
Hali ya kutoenda haja kubwa ni kawaida kwa mwanamke yeyote aliye na mimba. Dalili hii ni ile kati ya kwanza wakati mwanamke amepata ujauzito. Homoni Progesterone hufanya chakula kuenea polepole kwenya matumbo na hii husababisha ugumu wa kuenda haja kubwa.

Mhemko wa hisia
lazy_placeholder.gif
Katika Muhula wa kwanza wa mimba, utaweza kupata mhemko wa hisia. Unaweza kuhisi furaha halafu baada ya muda chache wahisi huzuni. Kuna wakati mwingine unaweza kujipata unalia kwa mambo madogo sana. Haya yote ni kwa sababu mwili wako unapitia mabadiliko kuweza kumtengeneza mtoto.

Kuhisi Kizunguzungu
lazy_placeholder.gif
Wakati damu linaongezeka na shinikizo la damu kupunguza, unaweza kusikia kichwa chepesi au kizunguzungu wakati wa kwanza kama dalili ya mimba. Wakati mwingine, ukosefu wa sukari kwa damu unaweza kufanya mwanamke mja mzito kuzirai.

Ni muhimu wakati unaposikia uwepesi wa mwili, kuketi chini au kujilaza na kuuweka miguu juu ya mto ili damu literemke kichwani. pia kuhakikisha unakula kila wakati unahisi njaa husaidia kupunguza hali hii.

Kuzidi kwa Kuhisi Joto
lazy_placeholder.gif
Unapoamka, joto la mwili wako huwa la kawaida kila siku. Unapopata mimba joto hili hugeuka na kuwa nyingi kushinda kawaida. Baada ya kuwa na hedhi, kuna wakati mwanamke huwa tayari kupata mimba wakati huu, joto la mwili huongezeka halafu hurudi kuwa la kawaida baada ya wiki mbili.
Ukigundua kuwa joto hili halijapungua baada ya wiki mbili, basi una chanzo kubwa cha kuwa na mimba haswa kama umeshirikaina ngono bila kinga.

Kukosa Hedhi
lazy_placeholder.gif
Baadhi ya dalili nyingi mwilini mwa mwanamke aliye na mimba, Kukosa hedhi ni ule wa kwanza mno haswaa kama (Period) yako ni ya kila mwezi. Utaweza kugundua umekosa mwezi wakati unapojua vyema umefanya ngono bila kujikinga.

Kujawa na hewa
lazy_placeholder.gif
Ni kawaida kwa mwanamke aliye na mimba kuhisi kana kwamba amejaa hewa tumboni na pia kutoa hewa hapa na pale. Hii ni kwa sababu tumbo la uzazi linapanuka kuhakikisha mtoto yuko na mahali pa kukua na kuzunguka.

Kuongezeka kwa hamu ya chakula
lazy_placeholder.gif
Wanawake wengi wanapopata mimba, ingawaje wengi wao huwa wagonjwa na wanahisi wasile vyakula kila wakati, Mwanamke akifikisha muhula wa pili, Hamu ya kula huongezeka.
Sababu ya hamu kuongezeka ni, mtoto aliye tumboni anahitaji chakula pia. Unaweza kuona mama aliyekula chakula sahani moja, anaanza kukula sahani moja na nusu na baada ya muda si mrefu anahisi njaa tena.
Homoni zilizo mwilini hubadilika na kumfanya mwanamke aliye na mimba kuwa na hamu ya kula kila wakati ili mtoto aweze kupata nguvu na kukua vema.

Kulala Muda kwa muda
lazy_placeholder.gif
Wakati mwanamke amekuwa mja mzito, Homoni (progesterone) huongezeka zaidi mwilini. Tulivyonena hapo mbeleni, Homoni hii hufanya kazi mwilini kuzembea.
Hii ndio sababu ya wanawake wengi walio na mimba kuhisi usingizi kila wakati. Tukumbuke kuwa, Mwana anayetengenezwa chupani mwa mamake, anahitaji nguvu zote ili kujistahimili.
Akina mama wanaochukua muda wa kupumzika huwasaidia wanawe kukua kwa njia bora. Pia, afya ya mama huongezeka anapochukua muda wa kulala wakati ana mimba.

Kuhisi una mimba kama matokeo ya ngono
Kuna wanawake wengi wanaojua tu wameshika mimba baada ya ngono. Hisia hizi huwa pembe ya kila mwanamke anayejua mwili wake vizuri.

Unapotazama enzi za kale, mamake msichana aliye na mimba angejua kwa haraka kuwa mwanake ana mimba bila kutizama dalili zote. Hisia kama hizi huwa ya ukweli na zilitumiwa na mababu zetu kujulisha wanawake wanaotarajia wana. Mila hii ilipitishwa kwa kizazi kimoja hadi kingine.

“Kulea mimba si kazi, kazi kulea mwana”
Kuchukua kipimo cha mimba (pregnancy test)
Njia iliyo sahihi kabisa na wa kisayansi na imeaminika kuwa ya haki ni kwa kupima mimba kutumia (pregnancy test).
Kipimo hiki huwa kimetengenezwa kitechnologia. Mwanamke aliyedhani kuwa ana mimba huikojolea kisha kutizama matokeo ya alama ngapi kipo kwenye kipimo hiki cha mimba. Kukiwa na alama mbili hapo basi mwanamke anatarajia mwana.

“Kuzaliwa kumoja, maisha mengi”
Kuna aina mbali mbali toka hapo jadi ya kueleza kama mwanamke ni mja mzito kama vile:-
  • Wanawake wa Misri walikuwa wanapima mimba kwa kukojolea mbegu za ngano siku kadhaa. Mbegu hizo zikianza kuonyesha hali ya kumea, mwanamke alisemekana kuwa na mimba
  • Njia nyingine ilikuwa ya kitunguu. Mwanamke aliweka kipande cha kitunguu kwa uke wake wakati wa usiku alipoenda kulala. Asubuhi ya kuamka, harufu ya kitunguu isipotokea mdomoni alisemekana kuwa na mimba.
  • Kwa wengine, Mwanamke alikuwa akojoe ndani ya beseni kisha kuweka kofuli au kifunguu ndani ya mkojo uliyo ndani ya beseni kwa muda wa masaa matatu au manne.Iliaminiwa kuwa ukisha mwaga hayo makojo na alama ya kofuli au kifunguu kibaki kwa beseni basi una mimba.
  • Mwanamke aliye na mimba ana mkojo wa rangi tofauti. Haswaa ya kijani. Rangi hii huendelea hadi mwisho wa mimba.
Unawezaje kujua haswaa una mimba?
Baada ya kufanya ngono bila kinga, na wakati mwanamke amefikisha umri wa kupata mtoto, (wakati msichana huanza mzunguko wa hedhi), ukiwa na dalili zote zilizotajwa hapo awali, jaribu kuenda na kuhakikisha na Daktari ili isiwe ni alama ya chanzo cha ugonjwa fulani na wala si mimba.
Ni muhimu kuhakikisha una mimba wakati unapofikiria u mjamzito. Pia ukisha pata uhakikisho, unaweza kuchukua vipimo bora vya kujitunza wewe na mwanawe.
Mwanamke yeyote aliyegundua yuko na mimba anahitajika kutibiwa vyema na wale walio karibu naye. Kila mwanamke anastahili kuonyeshwa heshima haswaa wale wanaobeba maisha ndani yao.
Imeaminika mwanamke aliye na furaha kila wakati anapokuwa na mimba huweza kuzaa vizuri na watoto wao pia huwa na furaha.

Upenyo wa Haraka
  • Uja uzito ni baraka na ni lazima kila mtu ajue kwamba maisha hupewa na Mola ili kuendeleza vizazi.
  • Aibu na laana kwa wanawake unastahili kukomeshwa haswa wakati ni wajawazito. Upendo na hali ya amani ni chanzo kubwa cha hawa wanaweke kujiwezesha kupitia muda huu kwa urahisi.
  • Kukula vyakula vizuri kama mboga iliyo na Iron (Chuma) na kalsiamu huwasaidia wanawake kuongeza damu. Pia kukunywa maji mengi wakati huu ni muhimu sana kwa kusaidia viungo vya mwili kujimudu.
  • Kufanya mazoezi kama kutembea kila siku ni muhimu kwa sababu wakati wa kujifungua unapokaribia huwa rahisi na machungu ya kuzaa mwana hupungua.
Kila la heri na ufanikio unapoanza safari hii ya uzazi. Pongezi mama


Chanzo: The African Parent
 
Baada ya week 2 ndio inaweza kuonekana hapo ni kwa uwakika zaidi, ila kwenye maduka kuna vipimo vya kujipa ile asubuhi tu ukiamka na ule mkojo wa kwanza kinaweza kuonyesha.
 
Baada ya week 2 ndio inaweza kuonekana hapo ni kwa uwakika zaidi...ila kwenye maduka kuna vipimo vya kujipa ile asubuhi tu ukiamka na ule mkojo wa kwanza kinaweza kuonyesha.
Nimejipima jana na hiyo UPT ila imeonyesha negative, hapa ni baada ya cku kama 5 hivi zimepita, so niendelee kusubiri?
 
nimejipima jana na hiyo UPT ila imeonyesha negative, hapa ni baada ya cku kama 5 hivi zimepita, so niendelee kusubiri

Basi hauna mimba maana hiyo UPT huwa inaonyesha kama unayo au labda wait mpaka baada ya week 2......
 
Mimba inakuwadetected na upt baada ya wk2, na inaanza kuonekana baada ya wk20 yaan baada ya miezi mitano. Lakin ultrasound inaweza ona hata chini ya hapo.
 
Ukipima na kifaa - pregnancy test, hata mimba iliyoingia jana inaonekana. So jaribu hiyo itakupa ukweli zaidi.
 
Kwa kwetu Tanzania, hatuko that much sophisticated interms of diagnostic facilities, vipimo tunavyotumia ni crude na vinachukua muda mrefu kupata matokeo. Kwetu kipimo tunachotumia cha UPT (urine for pregnancy test) kitakuwa positive siku ya 8 ( kama wiki moja hivi) mpaka ya 11 (roughly 2 weeks) baada ya missed period. Tunatumia pia USS (Ulatrasound), ambayo nayo itaona mimba (intradecidual gestation sac - kifuko cha mimba) wiki ya 4 mpaka ya tano ya ujauzito.

Kama uko Ulaya mimba yaweza kuwa diagnosed 5 days before the first missed period, yaani siku ya 9 since conception [tangu mimba kutunga na sio tangu kukosa siku zako-tofauti na UPT ambayo inakuwa positive siku 8 (roughly one week) baada ya kumiss period na sio baada ya conception, kwa sababu conception hutokea siku 14 kabla ya next menstruation] kabla hata hujakosa siku za mzunguko unaofuata, wanatumia vipimo kama ELISA na vingine.

Jaribu kurudia UPT on the 7th or 8th day since your first day of the last missed menses, na pia kama ni negative rudia siku ya 11, kama itakuwa negativu tena, TRY AGAIN next time you might succeed.
 
Mimba inakuwadetected na upt baada ya wk2, na inaanza kuonekana baada ya wk20 yaan baada ya miezi mitano. Lakin ultrasound inaweza ona hata chini ya hapo.
Nimekuelewa docta, ila kwa sasa nishaanza kuingia period inamaana mimba haikuingia, vp, naweza kukuPM kwa maswali zaidi?
 
niwaellyester1, u seem to be so worried, kama ipo itakuwepo tu, dont worry.

Kwa kwetu Tanzania, hatuko that much sophisticated interms of diagnostic facilities, vipimo tunavyotumia ni crude na vinachukua muda mrefu kupata matokeo. Kwetu kipimo tunachotumia cha UPT (urine for pregnancy test) kitakuwa positive siku ya 8 ( kama wiki moja hivi) mpaka ya 11 (roughly 2 weeks) baada ya missed period. Tunatumia pia USS (Ulatrasound), ambayo nayo itaona mimba (intradecidual gestation sac - kifuko cha mimba) wiki ya 4 mpaka ya tano ya ujauzito.

Kama uko Ulaya mimba yaweza kuwa diagnosed 5 days before the first missed period, yaani siku ya 9 since conception [tangu mimba kutunga na sio tangu kukosa siku zako-tofauti na UPT ambayo inakuwa positive siku 8 (roughly one week) baada ya kumiss period na sio baada ya conception, kwa sababu conception hutokea siku 14 kabla ya next menstruation] kabla hata hujakosa siku za mzunguko unaofuata, wanatumia vipimo kama ELISA na vingine.

Jaribu kurudia UPT on the 7th or 8th day since your first day of the last missed menses, na pia kama ni negative rudia siku ya 11, kama itakuwa negativu tena, TRY AGAIN next time you might succeed.
Me niko hapa hapa TZ , nimeanza period leo so inamaana mimba imeingia, dhumuni langu ilikuwa nipate mimba ila ndio hvyo tena, vp can i PM u 4 more questions?
 
me niko hapa hapa TZ , nimeanza period leo so inamaana mimba imeingia, dhumuni langu ilikuwa nipate mimba ila ndio hvyo tena, vp can i PM u 4 more questions?

Pole but dont worry, ur welcome niwaellyester1, u can PM me if I can help
 
Kujua wakati una mimba


Wanawake wengi hujua wameshika mimba aghalabu wiki 3 baada kushika mimba. Mwili wenyewe utakuonyesha/utakutabiria kama:
  • Hedhi yako itakoma/itakuwa nyepesi
  • Utasikia uchefuchefu/utatapika (ugonjwa wa asubuhi morning sickness na inaweza kutokea wakati wowote wa siku pia).
  • Matiti yako yataanza kuwasha, kufura au yataanza kuwa makubwa.
  • Chuchu (ncha ya titi) na sehemu zilizokaribiana zitaanza kuwa nyeusi na zizizoweza kuvumilia.
  • Itakubidi kwenda haja ndogo mara kwa mara.
  • Utasikia uchovu
  • Kusokotwa na tumbo
Kama umeona baadhi ya dalili hizo, unaweza kuwa na mimba. Pata jaribio/uchunguzi kipimo cha mimba ili kupata yakini! Unaweza pimwa bure katika kliniki iliyokaribu nawe au ununue kifaa vya kujipmia nyumbani kutoka duka la dawa. Daktari wako anaweza kukupima pia au atakuelekeza kwa mtaalamu kama hauna.

Vipimo vya mimba

Vipimo hivi huchunguza kuwepo kwa Human Cherionic Cronadotropin (HCG) kwa mkoja au damu. HCG wakati mwingine hitwa Pregnancy Hormone na huwa kwa mwanamke tu wakati ana mimba. Kuna aina mbili ya vipimo: kipimo cha mkojo na kipimo cha damu.

Kipimo cha Mimba cha Mkojo
Wanawake wengi hutumia kipimo hiki ambacho pia huitwa cha nyumbani (HPT-home pregnancy test) kwa sababu ni rahisi kutumia na bahasa (rahisi kibei) kuna aina nyingi za vipimo hivi. Kwa kimoja, utakwanya mkojo wajo kwa kikombe na kukitumbukiza kijiti huko na kwakingine utaweka kijiti hicho kwenye viungo vya mkojo. Njia iliyobora ni itakayokuonyesha kiwango cha HCG, hivyo tafuta moja katika kiwango cha hCG kutoka 15 hadi 30. Utasaidiwa na mhudumu wako dukani la dawa au kliniki.

Vifaa hivi hufaa kwa asilimia 97-99 kuyakirisha uwepo wa mimba vinapotumiwa ipasavyo. Hivyo kufuata maagizo ni muhimu. Pia angatia wakati wa kuharibika wa kifaa kwani kifaa kilichoharibika hakitakupatia matokeo unayotarajia.

Kama utapata matokeo yasiyofaa/yasiyo hakika
Kama utajipima/utapimwa bado kidogo*, unaweza kuona kwamba hauna mimba ili hali unayo. Aina nyingi ya vipimo vya nyumbani hukushauri ujipime baada ya siku kadha bila kujali matokeo uliyopata awali. Kama unaendelea kupata matokeo yasiyofaa nab ado unashuku una mimba, ongea na daktari/mkaguzi afya waka.

Kama utapata matokeo yafaayo/ya hakika
Kama utapata matokeo ya hakika, fanya miadi na mkaguzi afya wako punde tu. Mkaguzi wa afya yako atayakinisha kama una mimba kupitia kipimo cha damu na ukaguzi mwingine (pelvic exam) na atakwambia chaguzi uliza nazo.

Kipimo cha Damu
Kama wataka kipimo cha damu badala ya kite cha nuymbani, fanya miadi na mkaguzi afya wako/dakatari wako.
 
Mke wangu ananiambia anahisi anaweza kuwa mjamzito na tokea tukutane nae hazijapita hata siku tano je dalili zinaweza kujitokeza.mana ananiambia mala kichefuchefu mala mate yanajaa mdoni hata hamu ya kula hana.

Je, inawezekana? Naomba msada wenu.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom