Dalili za kushindwa mradi wa BRT ziko wazi

rosemarie

JF-Expert Member
Mar 22, 2011
6,887
3,412
Tumekaa kituo cha kimara in dk 50 sasa sioni kinachoendelea,watu ni wengi anaingia mmoja mmoja kwa taratibu sana huku machine zikishindwa kusoma ticket,hapa wafanyakazi kila mmoja yupo busy na simu anachati,je ni kweli tutaweza kuendesha viwanda??
 
IMG_20170628_083850.jpg
 
Tumekaa kituo cha kimara in dk 50 sasa sioni kinachoendelea,watu ni wengi anaingia mmoja mmoja kwa taratibu sana huku machine zikishindwa kusoma ticket,hapa wafanyakazi kila mmoja yupo busy na simu anachati,je ni kweli tutaweza kuendesha viwanda??

Inabidi uwe unawahi mapema, kwani ukifika kituoni saa 1245 kunakuwa afadhali vinginevyo ni mieleka kila mahali
 
Ukweli huo mradi una makwazo mengi sana kwa abiria, wakati mwingine bora wangetuachia ma daladala yetu ila waongezee barabara yawe mengi lakini kwa hayo ma mwendokasi yana makwazo mengi sana sana.
 
Majanga, hadi system imezidiwa...Poleni sana ndugu... DART inabid waboreshe mfumo wao, uendane na mahitaji ya watu
 
Tumekaa kituo cha kimara in dk 50 sasa sioni kinachoendelea,watu ni wengi anaingia mmoja mmoja kwa taratibu sana huku machine zikishindwa kusoma ticket,hapa wafanyakazi kila mmoja yupo busy na simu anachati,je ni kweli tutaweza kuendesha viwanda??
ungetupia picha za hao wanaochat ingesaidia sana pia huo umati wa watu na foleni unayosema ingekuwa msaada mbona siku hizi smartphone hata za 30 elfu zina camera mkuu
 
Huu mradi una ufisadi mkubwa sana,hata Rais anafahamu kuwa Simon Kisena ambaye ndiyo mmiliki wa huu mradi ni tapeli na fisadi mkubwa.

Rais alipokuwa Mwanza kwenye uwanja wa Furahisha aliagiza mali za Nyanza Cooperative Union(NCU) zilizochukuliwa kifisadi na Kisena zirudishwe na TAKUKURU wachunguze uwizi huo.Ile New Era Ginnery ni ya huyuhyu tapeli Kisena.

Alipomaliza kutapeli kanda ya ziwa,akahamia Dsm...Akamuingiza mjini yule muhindi wa magari ya HEICHER,akampa lundo la magari kwa utapeli,mpaka leo Muhindi anaramba cha moto.

Kwa sasa anatoa magari machache ili kuepuka ghalama za mafuta na kulipa madereva,Rais anajua uwizi huu kuanzia kwa rafiki yake Marehemu Didas Masaburi,Mama Firts Lady and Co.

Anchoogopa na kufukua makaburi,lakini hakuna ufisadi mkubwa kama uliopo DART,tatizo ni kwamba ufisadi huu ulishupaliwa na UKAWA na kina KUBENEA,Mzee anaona akiukomalia,basi kuna watu watapata sifa kuwa wao ndio waanzilishi,na yeye kuwapa sifa watu wengine hataki kabisa
 
DART leteni wawekezaji wa ukweli, Simon Group na genge lake wamanacheza na maisha yetu.

UDA-RT ni kampuni ya kitapeli , wote tunajua, sijui wametoa pesa kiasi gani kupata vigezo kwa serikali ya awamu ya tano...
 
Ukitaka kujua kwamba tunakurupuka jiukize
Mwendo kasi
Frayover ubungo
Frayover tazara
Teni mwendo kasi kwenda Moro

Hakuna tunachofanya kwa mafanikio
 
Back
Top Bottom