Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,919
- 31,161
UWEZEKANO wa kupatikana kwa chanjo dhidi ya ugonjwa hatari wa ukimwi unazidi kuongezeka baada ya matokeo ya awali ya chanjo ya majaribio kuthibitisha kuwa ni salama kutokana na watu waliohusika kwenye utafiti unaofanywa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (Muhas), kuonekana kuwa na ongezeko la vichocheo vya kinga dhidi ya ukimwi.
Habari hiyo njema imekuja wakati dunia bado ikihaha kutafuta dawa ya kutibu ugonjwa huo unaodhoofisha kinga ya mwili ambao umekuwa ukichukua maisha ya watu wengi, hasa walio barani Afrika.
Chanjo hiyo ya majaribio ilianza kutolewa Februari 20 mwaka jana, wakati mtu mmoja alipojitolea kupatiwa chanjo hiyo kwenye Kliniki ya Elimu ya Chanjo ya Kinga ya Maradhi ya Ukimwi (HIVIS).
Akizungumza kwenye mahafali ya pili ya chuo hicho, makamu mkuu wa chuo, Prof Kisali Pallangyo alisema matokeo hayo yameleta msisimko kwa watafiti wa masuala ya chanjo ya VVU duniani kote.
Hata hivyo, pamoja na matokeo hayo mazuri ya chanjo hiyo, Prof Pallangyo alisisitiza kuwa bado hakuna chanjo dhidi ya virusi vya ukimwi, hivyo ni lazima kila mtu azingatie njia zote sahihi za kujikinga na maambukizi ya virusi hivyo.
"Napenda kusisitiza kuwa bado hakuna chanjo dhidi ya virusi vya ukimwi na ni lazima kila mtu azingatie njia zote sahihi za kujikinga na maambukizi ya virusi vya ukimwi," alisema Prof Pallangyo.
Mkurugenzi wa mipango wa HIVIS, Dk Muhammad Bakari alisema mafanikio ya chanjo hiyo katika hatua ya awali yamethibitishwa na kwamba majibu ya chanjo hiyo kutoka Sweden yanaonyesha kuwa dawa hiyo ya chanjo ina uwezo wa kutengeneza kinga imara zaidi kuliko matokeo ya chanjo zilizowahi kufanywa awali duniani.
Dk Bakari alisema tatizo kubwa ni kasumba ambazo baadhi ya watu wanazo juu ya uhakika ambao watafiti wa chanjo hiyo wanao kuhusu nguvu ya chanjo hiyo.
"Kuna watu wanaofikiria kuwa ili kutambua nguvu ya chanjo hii ni kuwapatia chanjo watu wenye virusi vya ukimwi. Hii ni njia chafu na isiyo na maadili na haiwezi kwa njia yoyote ile kutumika," alisema Dk Bakari.
Alisema: "Chanjo hii ni kwa ajili ya kutambua usalama na matokeo ya chanjo dhidi ya virusi vya ukimwi kwa watu waliojitolea kupatiwa chanjo hiyo. Na itachukua majaribio mengi zaidi kabla ya kuanza kutumika ili tumika kutambua nguvu yake ya kukinga virusi vya ukimwi."
Aliongeza kuwa muda huo ukifika watatumia kundi la wanaofungamana ikiwa ni hatua ya juu na ya hatari ya kupata uhakika wa chanjo hiyo. Alisema watatumia njia zote kuwakinga wahusika na virusi hivyo.
Dk Bakari aliongeza kuwa kikubwa kinachowavunja moyo watafiti wa chanjo hiyo ni baadhi ya madaktari ambao kwa kukosa elimu ya kutosha juu ya chanjo, wanatoa taarifa za uongo kwa umma. Alisema hii ni kutokana na msukosuko na mkanganyiko walionao watu hao.
Alitoa mfano, uvumi ulio mitaani kwamba chanjo hiyo hutumika kusambaza virusi vya ukimwi kwa watu waliojitolea, jambo ambalo alisema halina ukweli wowote na kutokana na uvumi huo wameongeza elimu kwa wanaojitolea juu ya hatua husika katika majaribio hayo.
Source: Mwananchi
Habari hiyo njema imekuja wakati dunia bado ikihaha kutafuta dawa ya kutibu ugonjwa huo unaodhoofisha kinga ya mwili ambao umekuwa ukichukua maisha ya watu wengi, hasa walio barani Afrika.
Chanjo hiyo ya majaribio ilianza kutolewa Februari 20 mwaka jana, wakati mtu mmoja alipojitolea kupatiwa chanjo hiyo kwenye Kliniki ya Elimu ya Chanjo ya Kinga ya Maradhi ya Ukimwi (HIVIS).
Akizungumza kwenye mahafali ya pili ya chuo hicho, makamu mkuu wa chuo, Prof Kisali Pallangyo alisema matokeo hayo yameleta msisimko kwa watafiti wa masuala ya chanjo ya VVU duniani kote.
Hata hivyo, pamoja na matokeo hayo mazuri ya chanjo hiyo, Prof Pallangyo alisisitiza kuwa bado hakuna chanjo dhidi ya virusi vya ukimwi, hivyo ni lazima kila mtu azingatie njia zote sahihi za kujikinga na maambukizi ya virusi hivyo.
"Napenda kusisitiza kuwa bado hakuna chanjo dhidi ya virusi vya ukimwi na ni lazima kila mtu azingatie njia zote sahihi za kujikinga na maambukizi ya virusi vya ukimwi," alisema Prof Pallangyo.
Mkurugenzi wa mipango wa HIVIS, Dk Muhammad Bakari alisema mafanikio ya chanjo hiyo katika hatua ya awali yamethibitishwa na kwamba majibu ya chanjo hiyo kutoka Sweden yanaonyesha kuwa dawa hiyo ya chanjo ina uwezo wa kutengeneza kinga imara zaidi kuliko matokeo ya chanjo zilizowahi kufanywa awali duniani.
Dk Bakari alisema tatizo kubwa ni kasumba ambazo baadhi ya watu wanazo juu ya uhakika ambao watafiti wa chanjo hiyo wanao kuhusu nguvu ya chanjo hiyo.
"Kuna watu wanaofikiria kuwa ili kutambua nguvu ya chanjo hii ni kuwapatia chanjo watu wenye virusi vya ukimwi. Hii ni njia chafu na isiyo na maadili na haiwezi kwa njia yoyote ile kutumika," alisema Dk Bakari.
Alisema: "Chanjo hii ni kwa ajili ya kutambua usalama na matokeo ya chanjo dhidi ya virusi vya ukimwi kwa watu waliojitolea kupatiwa chanjo hiyo. Na itachukua majaribio mengi zaidi kabla ya kuanza kutumika ili tumika kutambua nguvu yake ya kukinga virusi vya ukimwi."
Aliongeza kuwa muda huo ukifika watatumia kundi la wanaofungamana ikiwa ni hatua ya juu na ya hatari ya kupata uhakika wa chanjo hiyo. Alisema watatumia njia zote kuwakinga wahusika na virusi hivyo.
Dk Bakari aliongeza kuwa kikubwa kinachowavunja moyo watafiti wa chanjo hiyo ni baadhi ya madaktari ambao kwa kukosa elimu ya kutosha juu ya chanjo, wanatoa taarifa za uongo kwa umma. Alisema hii ni kutokana na msukosuko na mkanganyiko walionao watu hao.
Alitoa mfano, uvumi ulio mitaani kwamba chanjo hiyo hutumika kusambaza virusi vya ukimwi kwa watu waliojitolea, jambo ambalo alisema halina ukweli wowote na kutokana na uvumi huo wameongeza elimu kwa wanaojitolea juu ya hatua husika katika majaribio hayo.
Source: Mwananchi