Dalili za CCM kupatia OCAMPO kazi 2015 zinajionyesha wazi

Joblube

JF-Expert Member
Mar 4, 2011
369
151
CCM ilivyo sasa imepungukiwa na upeo wa kuona mambo na kudhani kuwa wao ndio wenye hati miliki ya kuongoza nchi hii na Rais lazima atoke ndani ya CCM ndio maana badala ya kutatua kero za wananchi wao kwa sasa wanaangalia nani rais ndani ya CCM 2015 ikiwa juzi tuu tumetoka kwenye uchaguzi na wao ndio wanaongoza serikali, hii ni dharau kubwa kwa Watanzania na inaonyesha jinsi ambavyo hawako tayari kuachia madaraka kwa amani tena hawana tena uwezo wa kusoma alama za nyakati. Hata ule ushauri wa bure wa Majidi Mjengwa kwenye gazeti la Raia Mwema toleo lililopita hawakuona.Nasisitiza tena CCM isiendelelee kujidanganya kuwa inaweza kuendelea kuwadanganya watanzania kwa kuendelea kuwaibia kura. Kama CCM inadhamira ya kweli ya kulinda amani ya Tanzania lazima kuwe na tume huru chini ya Katiba mpaya 2015 na haki lazima itendeke na ionekane ikitendeka vinginevyo mnamuandalia Ocampo kazi na ofisi yake huenda ikawa Arusha 2016.
 
Bahati mbaya ndugu zangu na wengineo wooooote waliopo vijijini hawajaelewa...................
 
CCM ilivyo sasa imepungukiwa na upeo wa kuona mambo na kudhani kuwa wao ndio wenye hati miliki ya kuongoza nchi hii na Rais lazima atoke ndani ya CCM ndio maana badala ya kutatua kero za wananchi wao kwa sasa wanaangalia nani rais ndani ya CCM 2015 ikiwa juzi tuu tumetoka kwenye uchaguzi na wao ndio wanaongoza serikali, hii ni dharau kubwa kwa Watanzania na inaonyesha jinsi ambavyo hawako tayari kuachia madaraka kwa amani tena hawana tena uwezo wa kusoma alama za nyakati. Hata ule ushauri wa bure wa Majidi Mjengwa kwenye gazeti la Raia Mwema toleo lililopita hawakuona.Nasisitiza tena CCM isiendelelee kujidanganya kuwa inaweza kuendelea kuwadanganya watanzania kwa kuendelea kuwaibia kura. Kama CCM inadhamira ya kweli ya kulinda amani ya Tanzania lazima kuwe na tume huru chini ya Katiba mpaya 2015 na haki lazima itendeke na ionekane ikitendeka vinginevyo mnamuandalia Ocampo kazi na ofisi yake huenda ikawa Arusha 2016.
Nadhani ni ndoto nzuri.
 
Ocampo atapata kazi bila shaka!! Watu wa vijijini wataelewa tu, somo linaingia kupitia wanaelewa wala si ndoto ni kweli kabisa chama chetu chamapinduzi chajenga chuki siku hizi siyo kujenga nchi tena.
 
Bahati mbaya ndugu zangu na wengineo wooooote waliopo vijijini hawajaelewa...................
hao wa igunga waliopigia CDM ni wa mjini? naongelea watu 23,000 walioikataa CCM igunga.
 
Back
Top Bottom