Dalili Mbaya Kiuchumi, Hata Maonyesho ya Sabasaba yamedoda!

Watu wanajiandaa kwa panga la 18% nk nk.hapo bado ukiuza kitu toa risiti,ukinunua kitu dai risiti.Tunaisoma namba wote mwaka huu.
 
Yale majina ya makampuni maarufu hapo77 bado wapo? kwa nini umaarufu umepotea ghafla.

Mh JPM wakati unaendelea kuwaomba wananchi wakuombee kwa Mungu ni vizuri sana na wewe ukaongeza kumuomba Mungu akuzidishie hekima ya kutuongoza. Kuna watu wanamkakati wa kukukatisha tamaa na kukurudisha nyuma usitimize anzama yako ya kuwatumikia Watanzania bila kuwaangusha.

Ni kama vile wanajibidisha kuhakikisha unawaangusha Watanzania ili uaibike. Ila ukitegemea hekima itikayo kwa Mungu na amini utashinda.

Hii dunia imegeuka kweli mtu mwenye nia njema ya kusaidia wananchi wa hali ya chini na wasioweza kujisaidia ndiye anapigwa vita, na wakati mwingine maskini haohao ndio wanatumiwa katika vita hiyo.
 
Sasa hivi wenye pesa ni wale waliyoipata kihalali kwa jasho ambao huwa wabahili kuitumia hovyo hovyo.

Waliokuwa wanajazana huko sabasaba wengi wao wlikuwa ni wale waliopata mapesa kwa njia za madili haramu yakiwamo ya kuuza unga. Hawa mwaka huu wanaisoma namba.
 
Miaka ya nyuma maonyesho ya Sabasaba Kilwa Road yalikuwa yanashamiri na kuleta picha Fulani hivi kuhusu uchumi wa mtu mmoja mmoja na makampuni yanayoshiriki.
Lakini mwaka huu kwa karibia ya wiki sasa yamedorora na mbanda mengi hayajafungukiwa na hata wananchi hawana furaha ya kufuatili kwa nini?
Kuna dalili mbaya sana ya mwenendo wa nchi kiuchumi wa watu wake, kila mtu kapigika au tuseme wengi wamepigika na hakuna jitihada ya wazi kulikabili hilo.
Nina banda la kampuni yangu mle ndani , pamoja na kuweka vifaa vya kisasa na wahudumu bomba lakini naomba nikwambie kitu , mwaka huu ninaziona dalili za kupata hasara kubwa sana na Kiukweli hali ya uchumi kama itakuwa hivi kwa miaka miwili ijayo MAONYESHO YA SABASABA YATAFUNGWA MOJA KWA MOJA , maana hakuna tunachokifanya kule , ni bora kufanya matangazo ya biashara kwa njia nyingine .
 
Sasa hivi wenye pesa ni wale waliyoipata kihalali kwa jasho ambao huwa wabahili kuitumia hovyo hovyo.

Waliokuwa wanajazana huko sabasaba wengi wao wlikuwa ni wale waliopata mapesa kwa njia za madili haramu yakiwamo ya kuuza unga. Hawa mwaka huu wanaisoma namba.
Unauhakika waliokuwa wanajaa Kule walikuwa watu wa dili? Mbona wanafunzi, wamama wa nyumbani na wananchi wa kawaida wanaoenda nunua bidhaa ndio walikuwa wengi? Hivi hao nao ni wa dili?
Tukubali tuu kuwa nchi iko kwenye mkwamo na matumaini yanapotea kwa kasi
 
Maonyesho kawaida sawa na siku zote.Watu wapo wengi tu.Ukute mleta mada hakuwahi kwenda kwenye hayo maonyesha na pengine hayupo hata Dar.Mtajikuta mnakuwa wachawi mwisho wa siku.
 
Tusubiri tu mkuu mbona trh 7 July haijafika!
Nina uzoefu sana na haya maonyesho mkuu , tarehe 7 ni siku ya kuhitimisha shughuli tu , manunuzi , mauzo pamoja na matangazo yote yanafanyika siku kama hizi , ngoja nikuulize kitu , hivi safari hii umesikia tena hata yale matangazo ya NUNUA MOJA PATA TATU BURE ? si kizota wala heineken wala wale wala mdudu kule mole bar , kote kimyaaaaa !!!!
 
Maonyesho kawaida sawa na siku zote.Watu wapo wengi tu.Ukute mleta mada hakuwahi kwenda kwenye hayo maonyesha na pengine hayupo hata Dar.Mtajikuta mnakuwa wachawi mwisho wa siku.
Kama ni uzushi basi magazeti ya Leo nayo yamezusha kwa kiwango kikubwa.
 
Na ukinunua kitu ndani hata pensel ukitoka lazima uwe na risiti kama huna unanyanganywa. Vitu vinauzwa bei sana
 
Mzunguko wa pesa Kwa watu wa kawaida Kwa sasa ni mgumu sana , wenye pesa wengi wameficha pesa zao Kwa hofu hivyo ni vigumu wananchi wa kawaida kwenda kujazana huko 77 .
 
To be sincere, mwaka huu 77 hali ngumu sana... wananchi wachache sana wanaokwenda.. hata magari ktk parking nje ya 77 grounds machache..!! Naona uchumi wa wananchi umeyumba kidogo..!! Hali si nzuri, lazima niseme ukweli, hali ni tofauti na miaka ya nyuma.. labda tuvumiliane uchumi utakuwa mzuri MUNGU AKIPENDA, maana Rais wetu Magufuli anajitahidi sana, pia anamwomba Mungu sana, tuvumiliane tu..
 
Tarehe saba urudi hapa na thread mpya.

wangejaa leo ungesema hawana kazi
 
Back
Top Bottom