Dalili kuu za kufeli kwa Rais Magufuli

Tukwazane Taratibu

Senior Member
Dec 20, 2012
195
537
Wasalamu wana JF.

Kwanza kabisa nianze kwa kujifuta machozi na kuionea huruma nchi yangu ya Tanzania kwa kufika huku ilipofika kwa sababu ya ukosefu wa umakini katika chaguzi na teuzi za viongozi. Tumekuwa ni nchi yenye mfumo mbaya na wa kijinga wa uchaguzi wa viongozi na hata mfumo ya kiuteuzi umekuwa hivyo hivyo enzi na enzi sasa. Nchi yetu imejengwa katika misingi ya kinafiki na kujipendekeza ambayo imepelekea viongozi wengi kuwa watu wasiokuwa "REAL" katika mifumo yao ya kuongoza.


Mwaka 2015 ulikuwa ni mwaka wa kihistoria katika nchi yetu, ni mwaka amao tuliwashuhudia wavivu, wazembe na wanafiki wakiibuka kuyasaka madaraka kwa hila na mali. Ni mwaka ambao msululu wa wasaka tonge waijitokeza kuchukua fomu za kugombania nafasi kubwa ya Urais wa nchi yetu. Mathalani ndani ya chama tawala walijitokeza wagombea 42, lakini ukiwatazama hawa 42 wengi wao walikuwa hawajui kwa nini wamechukua fomu za kuomba kuiongoza nchi yetu. Wengi walijitokeza kwa kushitukiza, mashinikizo na hata kwa tamaa ya kutaka kukwea katika kiti kikubwa kuiko vyote ndani ya nchi na kiuongozi. Hawakuwa na nia wala malengo ya muda mrefu na nchi yetu. Kiufupi walijipeleka kwa mihemko.



Katika pilika pilika hizo chama cha Mapinduzi nach kiliingia kwenye mtego wao aidha kwa makusudi au kwa kujua na kufanikisha kuwachuja wagombea hadi watano na mwishowe watatu waliofanikiwa kuingia hatua ya mwisho ya mchujo wa kura. Ukiwatazama hawa wanafainali watatu hakuna hata mmoja aliyekuwa na ndoto ya Tanzania moyoni wala mawazoni mwake, walibeba fomu kwa mashinikizo ya wakubwa wao kipindi hicho.


KWA NINI UTAWALA WA MAGUFULI UTAFELI.


1. Kwa sababu alikuwa hajajiandaa kuwa Rais kisaikolojia au kimbinu. Magufuli hakujiandaa na wala hakuwahi kujua kama kuna siku anagekuja kubeba bendera ya kwanza ya nchi hii, hata uchukuaji wake wa fomu ya kugombea Urais unasemekana alishinikwa na Rais mmoja wa zamani. Kwamba chama kilimkosa mtu hivyo bwana mkubwa akalazimishwa abebe kijiti hiki. Kitaalamu ni kwmaba kama ulikuwa hujajiandaa kukifanya kitu na ukapewa dhamana ya kukifanya na kukisimamia kuna uwezekano mkubwa sana wa kushindwa.


Dalii ni nyingi sana za Magufuli kushindwa na kuonyesha kwamba alikuwa hajajiandaa kuwa Rais, mfano nyingi ya teuzi zake zimekosa weledi na nyingi zimeonyesha mahaba , mfano alipoingia madarakani tu aiwateua DASs, DEDs, DCs, RASs, RCs na hata Mawaziri na Mananibu wao. Kwenye teuzi zilizopo chini ya TAMISEMI kwa maana ya DCS, DEDs, na DAS, mkuu huyu alionyesh kuchemka mapema sana mana majina ya wateuliwa ylikuwa yakijirudia mara kwa mara katika teuzi tofauti tofauti, hii inaashiria kuwa mkuu hakuwa makini katika uteuzi wake au alikuwa anafanya kazi mwenyewe bila ushauri wa vyombo husika na wasaidizi wake. Hii ni daili kuu ya kushindwa.



2. Dalili ya pili ya kushindwa kwa Magufuli ni kukosekana kwa uthabiti na ubunifu kwa utawala wake. Wengi wa watawala na wateuliwa wa Rais wamekuwa siyo wabunifu, wamekuwa ni watu wa kusikiliza maagizo na kuendeshwa kwa mihemko. Mfano kitu kikiibuka Dar kesho yake utasikia kimegeuka na kuwa kampeni kwa viongozi wote nchini, kana kwamba think tank ya nchi hii iko kichwani mwa mtu mmoja Dar es salaam. Leo akiibuka mtu Dar na kusema naanza zoezi la kuzibua mitaro ,basi kila kiongozi mikoani ataifanya hiyo ni ajenda na kampeni ya nchi nzima. Hizi ni dalili za kushindwa na kukkosa umakini na ubunifu kwa viongozi.



3. Sera ya Viwanda .

Watanzania wengi haswa wa kipato cha chini walimpa kura Magufuli kwa kuwa alijinadi kuwa Tanzania aliyotaka kuiongoza ilikuwa Tanzania ya viwanda na kwamba angehakikisha katika utawala wake viwanda vingi vinpatikan kadri iwezekanavyo lakini ni miaka miili sasa nchi na wananchi wake hawajaona sera, wala dira wala mpango wowote ukianzishwa na serikali ili kuwezesha kupatika kwa nchi ya viwanda. Serikali imekuwa ni wapiga domo na nadiriki kusema kuwa Magufuli na wenzake wanatupigia domo katika ishu hii ya viwanda, hakuna uhalisia wowote. Wangekuwa ni watu makini, wenye nia ya dhati ya viwanda basi wangekuwa wameishafikisha mpango mkakati bungeni ili ujadiiwe na kupelekea kufanikisha nchi njema ya viwanda. Huwezi kusema utavipata viwanda kutoka mawinguni bila ya kuwa na mpango mkakati wa kuviwezesha kupatikana.



4. Uongozi wa visasi na chuki.


Uongozi wa Magufuli umetawaliwa na visasi na chuki kwa baadhi ya watu katika nchi hii, kwa sasa ukiwa mpinzani wa kiitikadi na watawala unakuwa umegeuka kuwa adui wao moja kwa moja. Hii siyo dalili njema hata kidogo kwa mstakabali wa taifa, leo mawazo mazuri ya kujenga kutoka kwa wapinzani wa kiitikadi hayapokelewi, wapinzani wamegeuzwa punching boxes za vyombo vya dola na usalama, hawana amani, hawako huru. Linatengenezwa bomu litakalokuja kulipuka na kuilipua Tanzania vipande vipande... oooh god forbid maana hata Rwanda ilianza hvi hivi.



5. Usalama hafiifu wa raia.

Nchi kwa sasa inalalama, wananchi hawana usalama wa maisha yao, mauwaji yasiyojulikana kila kuchapo, watu kupotea bila kuonekana na kujulikana walipo. Vyombo vya dola havina majibu ya kuridhisha juu ya matukio haya, haya yanaongeza chuki na kupunguza imani na ushirikiano wa raia kwa serikali yao. Kwa sasa ukanda wa Pwani ni ukanda hatari sana wa kuishi kwa Mtanzania yeyote mwenye hofu na maisha yake, vyombo vya usalama vikiongozwa na Polisi, TISS na wengine hawana majibu ya kutia moyo juu ya haya. Unategemea wananchi wa ukanda huo waamke wakazalishe huku hawajui kama watafika kesho? No, they can't,matokeo yake ni kuwa na wananchi wasioweza kuzalisha na kubakia kutegemea serikali yao hafifu isiyoweza kuwalinda iwape chakula na mambo mengine ya muhimu kwao.


Ninayo mengi ya kusema juu ya utawala huu wa Magufuli kwa leo hayo yanatosha, ila naomba itoshe tu kusema sioni PROGRESS yoyote tutakayopata kama nchi kutoka kwa utawala huu wa awamu ya tano.
 
Wasalamu wana JF.

Kwanza kabisa nianze kwa kujifuta machozi na kuionea huruma nchi yangu ya Tanzania kwa kufika huku ilipofika kwa sababu ya ukosefu wa umakini katika chaguzi na teuzi za viongozi. Tumekuwa ni nchi yenye mfumo mbaya na wa kijinga wa uchaguzi wa viongozi na hata mfumo ya kiuteuzi umekuwa hivyo hivyo enzi na enzi sasa. Nchi yetu imejengwa katika misingi ya kinafiki na kujipendekeza ambayo imepelekea viongozi wengi kuwa watu wasiokuwa "REAL" katika mifumo yao ya kuongoza.


Mwaka 2015 ulikuwa ni mwaka wa kihistoria katika nchi yetu, ni mwaka amao tuliwashuhudia wavivu, wazembe na wanafiki wakiibuka kuyasaka madaraka kwa hila na mali. Ni mwaka ambao msululu wa wasaka tonge waijitokeza kuchukua fomu za kugombania nafasi kubwa ya Urais wa nchi yetu. Mathalani ndani ya chama tawala walijitokeza wagombea 42, lakini ukiwatazama hawa 42 wengi wao walikuwa hawajui kwa nini wamechukua fomu za kuomba kuiongoza nchi yetu. Wengi walijitokeza kwa kushitukiza, mashinikizo na hata kwa tamaa ya kutaka kukwea katika kiti kikubwa kuiko vyote ndani ya nchi na kiuongozi. Hawakuwa na nia wala malengo ya muda mrefu na nchi yetu. Kiufupi walijipeleka kwa mihemko.



Katika pilika pilika hizo chama cha Mapinduzi nach kiliingia kwenye mtego wao aidha kwa makusudi au kwa kujua na kufanikisha kuwachuja wagombea hadi watano na mwishowe watatu waliofanikiwa kuingia hatua ya mwisho ya mchujo wa kura. Ukiwatazama hawa wanafainali watatu hakuna hata mmoja aliyekuwa na ndoto ya Tanzania moyoni wala mawazoni mwake, walibeba fomu kwa mashinikizo ya wakubwa wao kipindi hicho.


KWA NINI UTAWALA WA MAGUFULI UTAFELI.


1. Kwa sababu alikuwa hajajiandaa kuwa Rais kisaikolojia au kimbinu. Magufuli hakujiandaa na wala hakuwahi kujua kama kuna siku anagekuja kubeba bendera ya kwanza ya nchi hii, hata uchukuaji wake wa fomu ya kugombea Urais unasemekana alishinikwa na Rais mmoja wa zamani. Kwamba chama kilimkosa mtu hivyo bwana mkubwa akalazimishwa abebe kijiti hiki. Kitaalamu ni kwmaba kama ulikuwa hujajiandaa kukifanya kitu na ukapewa dhamana ya kukifanya na kukisimamia kuna uwezekano mkubwa sana wa kushindwa.


Dalii ni nyingi sana za Magufuli kushindwa na kuonyesha kwamba alikuwa hajajiandaa kuwa Rais, mfano nyingi ya teuzi zake zimekosa weledi na nyingi zimeonyesha mahaba , mfano alipoingia madarakani tu aiwateua DASs, DEDs, DCs, RASs, RCs na hata Mawaziri na Mananibu wao. Kwenye teuzi zilizopo chini ya TAMISEMI kwa maana ya DCS, DEDs, na DAS, mkuu huyu alionyesh kuchemka mapema sana mana majina ya wateuliwa ylikuwa yakijirudia mara kwa mara katika teuzi tofauti tofauti, hii inaashiria kuwa mkuu hakuwa makini katika uteuzi wake au alikuwa anafanya kazi mwenyewe bila ushauri wa vyombo husika na wasaidizi wake. Hii ni daili kuu ya kushindwa.



2. Dalili ya pili ya kushindwa kwa Magufuli ni kukosekana kwa uthabiti na ubunifu kwa utawala wake. Wengi wa watawala na wateuliwa wa Rais wamekuwa siyo wabunifu, wamekuwa ni watu wa kusikiliza maagizo na kuendeshwa kwa mihemko. Mfano kitu kikiibuka Dar kesho yake utasikia kimegeuka na kuwa kampeni kwa viongozi wote nchini, kana kwamba think tank ya nchi hii iko kichwani mwa mtu mmoja Dar es salaam. Leo akiibuka mtu Dar na kusema naanza zoezi la kuzibua mitaro ,basi kila kiongozi mikoani ataifanya hiyo ni ajenda na kampeni ya nchi nzima. Hizi ni dalili za kushindwa na kukkosa umakini na ubunifu kwa viongozi.



3. Sera ya Viwanda .

Watanzania wengi haswa wa kipato cha chini walimpa kura Magufuli kwa kuwa alijinadi kuwa Tanzania aliyotaka kuiongoza ilikuwa Tanzania ya viwanda na kwamba angehakikisha katika utawala wake viwanda vingi vinpatikan kadri iwezekanavyo lakini ni miaka miili sasa nchi na wananchi wake hawajaona sera, wala dira wala mpango wowote ukianzishwa na serikali ili kuwezesha kupatika kwa nchi ya viwanda. Serikali imekuwa ni wapiga domo na nadiriki kusema kuwa Magufuli na wenzake wanatupigia domo katika ishu hii ya viwanda, hakuna uhalisia wowote. Wangekuwa ni watu makini, wenye nia ya dhati ya viwanda basi wangekuwa wameishafikisha mpango mkakati bungeni ili ujadiiwe na kupelekea kufanikisha nchi njema ya viwanda. Huwezi kusema utavipata viwanda kutoka mawinguni bila ya kuwa na mpango mkakati wa kuviwezesha kupatikana.



4. Uongozi wa visasi na chuki.


Uongozi wa Magufuli umetawaliwa na visasi na chuki kwa baadhi ya watu katika nchi hii, kwa sasa ukiwa mpinzani wa kiitikadi na watawala unakuwa umegeuka kuwa adui wao moja kwa moja. Hii siyo dalili njema hata kidogo kwa mstakabali wa taifa, leo mawazo mazuri ya kujenga kutoka kwa wapinzani wa kiitikadi hayapokelewi, wapinzani wamegeuzwa punching boxes za vyombo vya dola na usalama, hawana amani, hawako huru. Linatengenezwa bomu litakalokuja kulipuka na kuilipua Tanzania vipande vipande... oooh god forbid maana hata Rwanda ilianza hvi hivi.



5. Usalama hafiifu wa raia.

Nchi kwa sasa inalalama, wananchi hawana usalama wa maisha yao, mauwaji yasiyojulikana kila kuchapo, watu kupotea bila kuonekana na kujulikana walipo. Vyombo vya dola havina majibu ya kuridhisha juu ya matukio haya, haya yanaongeza chuki na kupunguza imani na ushirikiano wa raia kwa serikali yao. Kwa sasa ukanda wa Pwani ni ukanda hatari sana wa kuishi kwa Mtanzania yeyote mwenye hofu na maisha yake, vyombo vya usalama vikiongozwa na Polisi, TISS na wengine hawana majibu ya kutia moyo juu ya haya. Unategemea wananchi wa ukanda huo waamke wakazalishe huku hawajui kama watafika kesho? No, they can't,matokeo yake ni kuwa na wananchi wasioweza kuzalisha na kubakia kutegemea serikali yao hafifu isiyoweza kuwalinda iwape chakula na mambo mengine ya muhimu kwao.


Ninayo mengi ya kusema juu ya utawala huu wa Magufuli kwa leo hayo yanatosha, ila naomba itoshe tu kusema sioni PROGRESS yoyote tutakayopata kama nchi kutoka kwa utawala huu wa awamu ya tano.
Uwa mnakosa la kusema
 
Wasalamu wana JF.

Kwanza kabisa nianze kwa kujifuta machozi na kuionea huruma nchi yangu ya Tanzania kwa kufika huku ilipofika kwa sababu ya ukosefu wa umakini katika chaguzi na teuzi za viongozi. Tumekuwa ni nchi yenye mfumo mbaya na wa kijinga wa uchaguzi wa viongozi na hata mfumo ya kiuteuzi umekuwa hivyo hivyo enzi na enzi sasa. Nchi yetu imejengwa katika misingi ya kinafiki na kujipendekeza ambayo imepelekea viongozi wengi kuwa watu wasiokuwa "REAL" katika mifumo yao ya kuongoza.


Mwaka 2015 ulikuwa ni mwaka wa kihistoria katika nchi yetu, ni mwaka amao tuliwashuhudia wavivu, wazembe na wanafiki wakiibuka kuyasaka madaraka kwa hila na mali. Ni mwaka ambao msululu wa wasaka tonge waijitokeza kuchukua fomu za kugombania nafasi kubwa ya Urais wa nchi yetu. Mathalani ndani ya chama tawala walijitokeza wagombea 42, lakini ukiwatazama hawa 42 wengi wao walikuwa hawajui kwa nini wamechukua fomu za kuomba kuiongoza nchi yetu. Wengi walijitokeza kwa kushitukiza, mashinikizo na hata kwa tamaa ya kutaka kukwea katika kiti kikubwa kuiko vyote ndani ya nchi na kiuongozi. Hawakuwa na nia wala malengo ya muda mrefu na nchi yetu. Kiufupi walijipeleka kwa mihemko.



Katika pilika pilika hizo chama cha Mapinduzi nach kiliingia kwenye mtego wao aidha kwa makusudi au kwa kujua na kufanikisha kuwachuja wagombea hadi watano na mwishowe watatu waliofanikiwa kuingia hatua ya mwisho ya mchujo wa kura. Ukiwatazama hawa wanafainali watatu hakuna hata mmoja aliyekuwa na ndoto ya Tanzania moyoni wala mawazoni mwake, walibeba fomu kwa mashinikizo ya wakubwa wao kipindi hicho.


KWA NINI UTAWALA WA MAGUFULI UTAFELI.


1. Kwa sababu alikuwa hajajiandaa kuwa Rais kisaikolojia au kimbinu. Magufuli hakujiandaa na wala hakuwahi kujua kama kuna siku anagekuja kubeba bendera ya kwanza ya nchi hii, hata uchukuaji wake wa fomu ya kugombea Urais unasemekana alishinikwa na Rais mmoja wa zamani. Kwamba chama kilimkosa mtu hivyo bwana mkubwa akalazimishwa abebe kijiti hiki. Kitaalamu ni kwmaba kama ulikuwa hujajiandaa kukifanya kitu na ukapewa dhamana ya kukifanya na kukisimamia kuna uwezekano mkubwa sana wa kushindwa.


Dalii ni nyingi sana za Magufuli kushindwa na kuonyesha kwamba alikuwa hajajiandaa kuwa Rais, mfano nyingi ya teuzi zake zimekosa weledi na nyingi zimeonyesha mahaba , mfano alipoingia madarakani tu aiwateua DASs, DEDs, DCs, RASs, RCs na hata Mawaziri na Mananibu wao. Kwenye teuzi zilizopo chini ya TAMISEMI kwa maana ya DCS, DEDs, na DAS, mkuu huyu alionyesh kuchemka mapema sana mana majina ya wateuliwa ylikuwa yakijirudia mara kwa mara katika teuzi tofauti tofauti, hii inaashiria kuwa mkuu hakuwa makini katika uteuzi wake au alikuwa anafanya kazi mwenyewe bila ushauri wa vyombo husika na wasaidizi wake. Hii ni daili kuu ya kushindwa.



2. Dalili ya pili ya kushindwa kwa Magufuli ni kukosekana kwa uthabiti na ubunifu kwa utawala wake. Wengi wa watawala na wateuliwa wa Rais wamekuwa siyo wabunifu, wamekuwa ni watu wa kusikiliza maagizo na kuendeshwa kwa mihemko. Mfano kitu kikiibuka Dar kesho yake utasikia kimegeuka na kuwa kampeni kwa viongozi wote nchini, kana kwamba think tank ya nchi hii iko kichwani mwa mtu mmoja Dar es salaam. Leo akiibuka mtu Dar na kusema naanza zoezi la kuzibua mitaro ,basi kila kiongozi mikoani ataifanya hiyo ni ajenda na kampeni ya nchi nzima. Hizi ni dalili za kushindwa na kukkosa umakini na ubunifu kwa viongozi.



3. Sera ya Viwanda .

Watanzania wengi haswa wa kipato cha chini walimpa kura Magufuli kwa kuwa alijinadi kuwa Tanzania aliyotaka kuiongoza ilikuwa Tanzania ya viwanda na kwamba angehakikisha katika utawala wake viwanda vingi vinpatikan kadri iwezekanavyo lakini ni miaka miili sasa nchi na wananchi wake hawajaona sera, wala dira wala mpango wowote ukianzishwa na serikali ili kuwezesha kupatika kwa nchi ya viwanda. Serikali imekuwa ni wapiga domo na nadiriki kusema kuwa Magufuli na wenzake wanatupigia domo katika ishu hii ya viwanda, hakuna uhalisia wowote. Wangekuwa ni watu makini, wenye nia ya dhati ya viwanda basi wangekuwa wameishafikisha mpango mkakati bungeni ili ujadiiwe na kupelekea kufanikisha nchi njema ya viwanda. Huwezi kusema utavipata viwanda kutoka mawinguni bila ya kuwa na mpango mkakati wa kuviwezesha kupatikana.



4. Uongozi wa visasi na chuki.


Uongozi wa Magufuli umetawaliwa na visasi na chuki kwa baadhi ya watu katika nchi hii, kwa sasa ukiwa mpinzani wa kiitikadi na watawala unakuwa umegeuka kuwa adui wao moja kwa moja. Hii siyo dalili njema hata kidogo kwa mstakabali wa taifa, leo mawazo mazuri ya kujenga kutoka kwa wapinzani wa kiitikadi hayapokelewi, wapinzani wamegeuzwa punching boxes za vyombo vya dola na usalama, hawana amani, hawako huru. Linatengenezwa bomu litakalokuja kulipuka na kuilipua Tanzania vipande vipande... oooh god forbid maana hata Rwanda ilianza hvi hivi.



5. Usalama hafiifu wa raia.

Nchi kwa sasa inalalama, wananchi hawana usalama wa maisha yao, mauwaji yasiyojulikana kila kuchapo, watu kupotea bila kuonekana na kujulikana walipo. Vyombo vya dola havina majibu ya kuridhisha juu ya matukio haya, haya yanaongeza chuki na kupunguza imani na ushirikiano wa raia kwa serikali yao. Kwa sasa ukanda wa Pwani ni ukanda hatari sana wa kuishi kwa Mtanzania yeyote mwenye hofu na maisha yake, vyombo vya usalama vikiongozwa na Polisi, TISS na wengine hawana majibu ya kutia moyo juu ya haya. Unategemea wananchi wa ukanda huo waamke wakazalishe huku hawajui kama watafika kesho? No, they can't,matokeo yake ni kuwa na wananchi wasioweza kuzalisha na kubakia kutegemea serikali yao hafifu isiyoweza kuwalinda iwape chakula na mambo mengine ya muhimu kwao.


Ninayo mengi ya kusema juu ya utawala huu wa Magufuli kwa leo hayo yanatosha, ila naomba itoshe tu kusema sioni PROGRESS yoyote tutakayopata kama nchi kutoka kwa utawala huu wa awamu ya tano.
Porojo tu, hakuna cha maana ulichoandika
 
Tunatawaliwa na binadamu kama wewe, tathmini shughuli zako za kila siku - tukikufahamu kisha ukatupatia fursa ya kukuchambuwa utahisi ulikosea njia kumbe uko sawa.

Utakosea sawa sawa na binadamu wengine lkn kwa issues za JPM sioni kama ana matatizo kiasi cha kumfanya afeli kufikia malengo yake.
 
31 Reactions
Reply
Back
Top Bottom