Dalili gani zinakujulisha kuwa umri umesogea?

Kuna mama niliongea nae, aliniambia ukikutana na traffic ukawaona ni vijana wadogo au daktari hospitali ukamuona ni kama mjukuu wako. Hapo hakuna ubishi wa chumvi uliyoila duniani.
Na vipi kuhusu kichwa kujaa mvi na kuanza kupoteza kumbu kumbu?!
 
Hizi ni dalili za umri kwisha, sio kusogea.
  1. Unapoenda haja ndogo huku ukiamini kua umefungua zipu na kumbe hujaifungua,
  2. Unapoanza kuisahau njia ya kurudi nyumbani,
  3. Unapoanza kuwachanganya watoto wako kwa sura zao na majina yao.
  4. Unapoanza kula vidonge kama chakula chako badala ya chakula,
  5. Unapokua na appointment za Hospitali kila mara,
  6. Unapoanza kulala mapema na kuamka mapema,
  7. Unapoanza kuutambua umuhimu wa majirani zako,
  8. Unapoanza kuwakumbuka rafiki zako wa zamani na kuwathamini zaidi,
  9. Unapoanza kuachiwa Nyumba na watoto ili ukae nao pindi wahusika wanapotoka out,
  10. Unapoanza kuachiwa funguo na majirani.....
 
Mie kuna siku mwendokasi inaanza nikapanda kuona likoje. Nimeingia nimekosa siti kuna mtu mzima akanipisha akaniambia kaa mzee. Nilijitathmini njia nzima na ndio ilikuwa mwisho wa kupanda mwendokasi
Daah nimecheka sana,
Naona mzee ulisononeka mnoo, ukaanza kukumbuka ujana wako ulivyoutumia leo hii unapishwa siti na kuitwa Mzee!
Kweli dunia njia.
 
Nilienda kucheza Moira jumamos/jumapili mazoezi nashangaa watu wanamuita mzee nipasie huku,mshua kwangu,dingo niwekee halafu nikiwaangalia nawaona ni wakubwa

Nimeshtuka nishaanza kuwa muhenga pro max
Mbavu zangu jamaniiii
Mshua nipasie hukuuuuu
 
Kuanza kuchanganya thamani za hela, mfano 5000 unatamka mia tano, elfu kumi unaiita elfu moja, mia tano yenyewe unaiita hamsini, na elfu moja unaiita mia. Ndugu yangu jua umr unapunga mkono😅😅😅
 
_Unapoanza kulimalima vibustani vya mboga mboga nyumbani.

_unapoanza kusuluhisha watu uonapo wanagombana/kupigana maana dalili ya ujana nikufurahia mabifu na kusema acha wanyooshane.

_kuanza kuvaa mabagi mkanda unavalia tumboni.

_kuanza kumind hata vitu vidogo mf mtu asipokusalimia shughuli anayo anaanza kusema hana nidhamu.

_kuanza kujali hata vitu visivyoeleweka mara ukiona kauchafu tu uwanja au kajani unakaokota na kwenda kutupa shimoni

Kuanza kupenda kuhudhulia kila sherehe na kupenda kupewa kauongozi hata kakugawa soda katika sherehe.

Kuanza kusahau mambo ya fashion ukienda kununua kitu mfano nguo hauangalii fashion ww unaangalia ugumu wa bidhaa. View attachment 1690708

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
Kuna moja umenigusa, bustani nashangaa hata hobby hii imetokea wapi!
 
Kuna mama niliongea nae, aliniambia ukikutana na traffic ukawaona ni vijana wadogo au daktari hospitali ukamuona ni kama mjukuu wako. Hapo hakuna ubishi wa chumvi uliyoila duniani.
Kuna siku moja nilienda shule moja ya chekechea aliyokuwa anafundisha rafiki wa kike wa mdogo wangu. Baada tu ya kufika na kukaa kama dakika tano wale watoto wakawa wananong'onezana "wewe Frank baba yako amekuja" hahahahaaaa nilicheka sana nikajisemea kimoyomoyo kumbe sasa ninalazimika kuwa na familia ya watoto kadhaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom