Wana JF last week nilikuwa natoka job na kusimama na sista du mmoja pale posta kituoni tukisubiri gari ya mbezi ya kimara, ilipokuja watu waligombea kinoma mie mwenyewe ilibidi nikae pembeni ili kunusuru afya, usalama na ustaarabu wangu. Lakini kutahamaki nilimuona yule sister du amepata siti tena ya dirishani, duh niliishiwa nguvu na kushangaa kuona aliwezaje kuingia pale mlangoni angali alionekana very soft and civilized. Ilibidi tu nitembee hadi akiba ili nizunguke na bus. Toka siku hiyo niko radhi hata nikope lakini nihakikishe anytime my car is working. Kweli ukitaka uone usumbufu wa daladala dar subiri siku uharibikiwe na gari.