Daktari na Engineer nani analipwa zaidi

anayelipwa zaidi ni injinia, lakini daktari ana wigo mpana zaidi kupata hela kuliko injinia. daktari akianzisha hospitali hata chumba kimoja tu, wateja huwa hawaishi.
kima cha chini cha kila mmoja hapo je kikoje ?
 
kima cha chini cha kila mmoja hapo je kikoje ?
usiwaze kulipwa mshahara, tunaangalia fursa za kujiajiri ndiko kunakoingiza hela. daktari anaweza kuacha kuajiriwa akaanzisha dispensary ikamwingizia faida ya milioni kumi kila mwezi au zaidi. icho ni kima cha chini. injinia anaweza kupata tenda moja tu kwa miezi sita au kwa mwaka, ikamfuta machozi yote. nasikitika kutosomea udaktari, nilisoma sheria kwa kulazimishwa, na ninaifanya kazi ya sheria pasipokutoka moyoni, pamoja na kwamba katika law firm yangu naweza ingiza hela nyingi sana kwa mwezi kuwapita wote madoctor na mainjinia. kesi moja au tatu tu inanifuta machozi, bado wateja wa kudumu wanaoingiza kwenye account kila mwezi hata kama hakuna kilichofanyika.
 
anayelipwa zaidi ni injinia, lakini daktari ana wigo mpana zaidi kupata hela kuliko injinia. daktari akianzisha hospitali hata chumba kimoja tu, wateja huwa hawaishi.

Umefikaje kwenye hiyo conclusion? Analipwa zaidi katika terms zipi? Mshahara wa Kitanzania? Tutajie scale zao wakiajiriwa hapa serikalini.
 
Nan analipwa zaidi kati ya daktari na injinia
Kibongo bongo hawatofautiani sana lakini Eng ana nafasi nzuri kutengeneza pesa nzuri nje ya mshahara...anaweza kuwa consultant wa mradi na akaendelea kazi bila kuathiri upande wa ajira yake.
 
iko poa sana,uwanja mpana na kazi hazipungui.....
hasa ukisomea maswala ya viwanda, then ukajitahidi kusomea na kichina.....nakuahidi hutojuta utafanya kazi na wachina hadi utakimbia....
Mkuu environmental engineer je ? Naye anaingiza sana pesa?
 
Kibongo bongo hawatofautiani sana lakini Eng ana nafasi nzuri kutengeneza pesa nzuri nje ya mshahara...anaweza kuwa consultant wa mradi na akaendelea kazi bila kuathiri upande wa ajira yake.
kuna kaka yangu ni daktari, alikodi tu nyumba akaweka dispensary ndogo tu, ndani ya mwaka mmoja aliacha ajira kwa masaaa, sasaivi, ana dispensary kubwa sana na ameshajenga na chuo cha mafunzo ya afya hapohapo. anaingiza mamia ya mamilioni. ni kazi inayoheshimika. nilikua na mimi nikisoma niwe doctor, lakini kilichotokea secondary school ndicho kikanifanya nikaishia kwenye sheria. hata hivyo, pesa ambayo ningeipata kwenye udoctor naipata kwenye sheria pamoja na kwamba sifurahii kuwa mwanasheria kwasababu short cut na umafia ni mwingi.
 
Back
Top Bottom