Daktari feki anaswa Mbeya akitibu watu zaidi ya 100,anafanya upasuaji

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Jeshi la Polisi jijini Mbeya linamshikilia Abdallah Bushiri (42) kwa tuhuma za kujifanya daktari wa binadamu wakati hana taaluma hiyo, baada ya kumkuta nyumbani kwake akiwa na wagonjwa zaidi ya 100 wakisubiri kupatiwa matibabu.

Kamanda wa polisi jijini Mbeya Ulrich Matei amethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo Mkazi wa Igodima jijini humo ambaye anafanya kazi hiyo kinyume na sheria za nchi huku akiwataka wananchi kuchukua tahadhari na kuhakikisha wanaenda kupata tiba sehemu rasmi ili kunusuru maisha yao.

Kamanda Matei amesema daktari huyo feki amekuwa akiwafanyia watu upasuaji ambapo wamemkuta akiwa na fomu za maabara, vipimo vya kupima ujauzito, dawa za kusafisha vidonda, chupa za kuongezea wagonjwa maji na mikasi na dawa zimekwisha muda wake wa matumizi.

Kwa upande wa Mganga mkuu wa halmashauri ya jiji la Mbeya, Bwana.Jonas Lurandala amesema mtuhumiwa Abdallah Bushiri hana taaluma ya udaktari na kuwataka wakazi wa jiji la Mbeya kutoa taarifa za wenye tabia kama hiyo ili kuokoa maisha yao.
 
Ningelikua na mamlaka leo, nadhani huyu Dr feki ningemuendeleza baada ya kumfanyia mahojiano ya kutosha.
Na, jambo la ajabu ninalo jiuliza tu nikwamba amewezaje kuwa akitibu watu kwa wingi kiasi hicho pasipo mamlaka kumdhibiti mapema...!!??
Kuna jambo hapa ambalo halipo sawa for sure
 
jiji la Mbeya, Bwana.Jonas Lurandala amesema mtuhumiwa Abdallah Bushiri hana taaluma ya udaktari na kuwataka wakazi wa jiji la Mbeya kutoa taarifa za wenye tabia kama hiyo ili kuokoa maisha yao.


Yawezakana mazingira yasiyo rafiki kwenye hiyo hospitali ya umma ndiyo yamewasukuma wagonjwa kwenda vichochoroni
 
Ningelikua na mamlaka leo, nadhani huyu Dr feki ningemuendeleza baada ya kumfanyia mahojiano ya kutosha.
Na, jambo la ajabu ninalo jiuliza tu nikwamba amewezaje kuwa akitibu watu kwa wingi kiasi hicho pasipo mamlaka kumdhibiti mapema...!!??
Kuna jambo hapa ambalo halipo sawa for sure
Inawezekana ana taaluma ila kakosa Ajira au mizengwe kwenye vibali
 
HUYO JAMAA ATAKUWA ALIACHA KAZI SERIKALINI AKAJIAJIRI SASA WAVIMBA MACHO WANAUMIA...... NAMAANISHA KWAMBA HUDUMA ZA HOSPITALI YA SERIKALI AU ZAHANATI AU KITUO CHA AFYA HAPO MAHALI NI WALA RUSHWA WAKUBWA, WANAFIKI NA WAVIVU SANA. WANA WIVU ULIOPITILIZA NA HUYO JAMAA WANAMUONEA BURE....... siyo haki hii.
 
Yawezakana mazingira yasiyo rafiki kwenye hiyo hospitali ya umma ndiyo yamewasukuma wagonjwa kwenda vichochoroni
Kabisa. Mbona Babu wa Loliondo alikuwa na watu wengi kabisa! Ina maana alikuwa anatibu ukweli? Naona watu wanasahau au hawataki kushughulisha bongo zao. Tena kwa kawaida waganga matapeli ndiyo huwa na wateja wengi kuliko waganga wa kweli. Mganga tapeli huwaambia na kuwafanyia wagonjwa kile masikio na miili yao inachotaka kusikia na kufanyiwa.
 
Kabisa. Mbona Babu wa Loliondo alikuwa na watu wengi kabisa? Ina maana alikuwa anatibu ukweli? Naona watu wanasahau au hawataki kushughulisha bongo zao. Tena kwa kawaida waganga matapeli ndiyo huwa na wateja wengi kuliko waganga wa kweli. Mganga tapeli huwawambia wagonjwa kile masikio yao yanayotaka kusikia...


Yote ni mahangaiko baada ya kweli kutokufanya kweli, endapo kweli ikifanya kweli, watu wataifuata kweli na isipofanya kweli wataendelea kuitafuta.
 
Ningelikua na mamlaka leo, nadhani huyu Dr feki ningemuendeleza baada ya kumfanyia mahojiano ya kutosha.
Na, jambo la ajabu ninalo jiuliza tu nikwamba amewezaje kuwa akitibu watu kwa wingi kiasi hicho pasipo mamlaka kumdhibiti mapema...!!??
Kuna jambo hapa ambalo halipo sawa for sure

Kweli huyu jamaa ni wa kumuendeleza kitaalamu kama wale wajuzijuzi wa kutengeneza umeme waliopewa zawadi na JPM, mkuu umesema ukweli kwani inaelekea jamaa anakub alika kwenye Community sawa tu na mzee wa Loliondo alivyokubalika na yaelekea dawa walizomkuta nazo zote ni "Overcounter Drugs" ambazo ni sawa na kutoa first Aid, pamoja na hivyo kuna baadhi ya nurses na Para medicals kadhaa ambao walikumbwa na hewa chafu ya vyeti lakini ni wazuri kwa kazi hakuna mfano...je wafe njaa?
 
Back
Top Bottom