Daktari apoteza maisha kwenye vurugu baada ya mechi ya Nigeria vs Ghana

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,805
4,484
1648639481430.png

Daktari kutoka nchini Zambia Joseph Kabungo ambae jana alikuwa ofisa wa CAF katika mchezo wa kufuzu kombe la Dunia baina ya Nigeria dhidi ya Ghana amepoteza maisha kutokana na vurugu zilizofanywa na mashabiki wa Nigeria mara baada ya mchezo huo kuisha kwa sare ya 1-1 na Ghana kufanikiwa kufuzu kombe la Dunia.

Kutokana na vyanzo mbalimbali vinaripoti kuwa mashabiki wa Nigeria walimpiga wakati wakilazimisha kuvamia ndani ya eneo la kuchezea kitu kilichompelekea apoteze fahamu na baadae kufariki.
===

Chama cha Soka cha Zambia (FAZ) kimethibitisha kifo cha Ofisa wa Afya, Joseph Kabungo ambaye alipoteza maisha katika vurugu zilizotokea katika mchezo wa Nigeria dhidi ya Ghana, jana Machi 29, 2022 kwenye Uwanja wa MKO Abiola Jijini Abuja, Nigeria

Vyanzo mbalimbali vinaripoti kuwa mashabiki wa Nigeria walimpiga wakati wakilazimisha kuvamia ndani ya eneo la kuchezea kitu kilichosababisha apoteze fahamu na baadaye kufariki

Nigeria ilipata sare na hivyo kukosa nafasi ya kucheza Kombe la Dunia 2022, hivyo mashabiki wakawa wanaingia uwanjani kuonyesha hasira zao mara baada ya fiimbi ya mwisho

Source: African Football Greats.
 
Nigeria wapuuzi, niliwaona wana timu nzuri zaidi ya Ghana, na matokeo mazuri yalikuwa upande wao game ya kwanza, lakuni wametolewa nyumbani kwao kwa uzembe wao wenyewe, CAF wawapige rungu tu.
 
Nigeria wapuuzi, niliwaona wana timu nzuri zaidi ya Ghana, na matokeo mazuri yalikuwa upande wao game ya kwanza, lakuni wametolewa nyumbani kwao kwa uzembe wao wenyewe, CAF wawapige rungu tu.
Sasa walikuwa na timu nzuri zaidi ya Ghana maana yake nini wakati wao ndio wametolewa, huo ni ushabiki tu.

Nigeria wanapenda sana kujiamini wakiwa nje ya uwanja lakini hayo ndiyo matokeo ya ndani ya uwanja lazima wayaheshimu tu maanake hamna namna. World Cup nyingine inakuja 2026 wajipange upya.
 
Back
Top Bottom