Uchaguzi 2020 Dakika ya 78: Nyekundu 0, Kijani 0

Ne Mbwitu

JF-Expert Member
Aug 23, 2020
275
801
Dakika ya 78 Kipindi cha pili cha lala salama, makocha hawatulii kwenye bench. Muda huu atakayepigwa goli itakuwa imekula kwake.

Wachezaji wa timu ya kijani wote wamerudi nyuma kuweka ukuta. Wachezaji wa timu Nyekundu wanashambulia kama nyuki.

Faulo na kona zinapigwa kila dakika hapa. Timu ya kijani inakoswa koswa hapa, mpira unagonga mwamba. Kipa amelala chini anagaagaa.

Kocha anataka kufanya mabadiliko ya safu ya ulinzi kwa timu ya kijani hapa. Kipa ameamka, lakini anachechemea.

Mabao bado ni bila kwa bila. Kipa wa timu ya kijani anatoa ishara kwa wachezaji wake waende mbele.

Inapigwa moja ndeefu, inajibiwa kwa kichwa. Wanapasiana hawa wachezaji wa Nyekundu. Wakakwenda kasi kweli kweli. Naona kipa anapiga kelele mabeki warudi haraka. Ooh wamechelewa, inapigwa cross kutoka mashariki ya uwanja huu. Goooooo....aah hapana, kipa ameutoa.

Nyekundu walicheza kama timu ya Brazil hapa. Mpira ulipigwa cross, mshambuliaji wa Nyekundu akatishia kama anataka kupiga kichwa ule mpira, akaupisha. Kwa guu lake la kushoto, akaunganisha shuti maridadi kabisa.

Kona ile inaenda kupigwa kutokea magharibi ya uwanja huu. Wanapasiana hapa Nyekundu, inapigwaa cross mojaa ....hatari hatarii kwenye mlango wa timu ya kijani. Inapiigwaa shuti moja kipa anaipanchi, inapigwa shuti lingine kipa ameruka amegonga kichwa kwenye mwamba.,.......eeh eeh....leo ndio leo, mtoto hatumwi sokoni.

Namwona kipa anagalagala pale golini. Watoa huduma ya kwanza wanaenda na machela. Wanamganga hapaa....kaaazi kweli kweli. Hebu tuwapeleke studio kwa ajili ya matangazo.
 
JamiiForums1556400106.jpg
 
Dakika ya 78 Kipindi cha pili cha lala salama, makocha hawatulii kwenye bench. Muda huu atakayepigwa goli itakuwa imekula kwake.

Wachezaji wa timu ya kijani wote wamerudi nyuma kuweka ukuta. Wachezaji wa timu Nyekundu wanashambulia kama nyuki.

Faulo na kona zinapigwa kila dakika hapa. Timu ya kijani inakoswa koswa hapa, mpira unagonga mwamba. Kipa amelala chini anagaagaa.

Kocha anataka kufanya mabadiliko ya safu ya ulinzi kwa timu ya kijani hapa. Kipa ameamka, lakini anachechemea.

Mabao bado ni bila kwa bila. Kipa wa timu ya kijani anatoa ishara kwa wachezaji wake waende mbele.

Inapigwa moja ndeefu, inajibiwa kwa kichwa. Wanapasiana hawa wachezaji wa Nyekundu. Wakakwenda kasi kweli kweli. Naona kipa anapiga kelele mabeki warudi haraka. Ooh wamechelewa, inapigwa cross kutoka mashariki ya uwanja huu. Goooooo....aah hapana, kipa ameutoa.

Nyekundu walicheza kama timu ya Brazil hapa. Mpira ulipigwa cross, mshambuliaji wa Nyekundu akatishia kama anataka kupiga kichwa ule mpira, akaupisha. Kwa guu lake la kushoto, akaunganisha shuti maridadi kabisa.

Kona ile inaenda kupigwa kutokea magharibi ya uwanja huu. Wanapasiana hapa Nyekundu, inapigwaa cross mojaa ....hatari hatarii kwenye mlango wa timu ya kijani. Inapiigwaa shuti moja kipa anaipanchi, inapigwa shuti lingine kipa ameruka amegonga kichwa kwenye mwamba.,.......eeh eeh....leo ndio leo, mtoto hatumwi sokoni.

Namwona kipa anagalagala pale golini. Watoa huduma ya kwanza wanaenda na machela. Wanamganga hapaa....kaaazi kweli kweli. Hebu tuwapeleke studio kwa ajili ya matangazo.
Safi sana, jiwe yuko hoi bin taabani

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Hadithi nzuri sana inanikumbusha mwaka 2004 kwenye Fainali za Euro kati ya Portugal vs Greece, Portugal ilitawala mchezo kwa kuwa na wachezaji mahiri kama Luis Figo,Cristiano Ronaldo,Nuno Gomez,Bruno na wakali kibao wakiongozwa na Scolari walionekana kuwa tishio lakini ukweli ni kwamba takwimu hazikuwa upande wao..

Nini kilijiri sasa ukweli ni kuwa Greece waliibuka na ushindi wa bao moja na kuwaacha wareno wakilia waliamini wao ndio walilitawala dimba lakini hawakujua mpira pia unahitaji sayansi na mbinu za kimchezo.

October 28th CCM inakwenda kubeba USHINDI WA KISHINDO na hili litakuwa somo kwa vizazi vijavyo kuwa Tanzania ni taifa huru na lina watu wazalendo haliihitaji kuamriwa au kuelekezwa namna ya kujiendesha.

JPM ANATOSHA
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Dakika ya 78 Kipindi cha pili cha lala salama, makocha hawatulii kwenye bench. Muda huu atakayepigwa goli itakuwa imekula kwake.

Wachezaji wa timu ya kijani wote wamerudi nyuma kuweka ukuta. Wachezaji wa timu Nyekundu wanashambulia kama nyuki.

Faulo na kona zinapigwa kila dakika hapa. Timu ya kijani inakoswa koswa hapa, mpira unagonga mwamba. Kipa amelala chini anagaagaa.

Kocha anataka kufanya mabadiliko ya safu ya ulinzi kwa timu ya kijani hapa. Kipa ameamka, lakini anachechemea.

Mabao bado ni bila kwa bila. Kipa wa timu ya kijani anatoa ishara kwa wachezaji wake waende mbele.

Inapigwa moja ndeefu, inajibiwa kwa kichwa. Wanapasiana hawa wachezaji wa Nyekundu. Wakakwenda kasi kweli kweli. Naona kipa anapiga kelele mabeki warudi haraka. Ooh wamechelewa, inapigwa cross kutoka mashariki ya uwanja huu. Goooooo....aah hapana, kipa ameutoa.

Nyekundu walicheza kama timu ya Brazil hapa. Mpira ulipigwa cross, mshambuliaji wa Nyekundu akatishia kama anataka kupiga kichwa ule mpira, akaupisha. Kwa guu lake la kushoto, akaunganisha shuti maridadi kabisa.

Kona ile inaenda kupigwa kutokea magharibi ya uwanja huu. Wanapasiana hapa Nyekundu, inapigwaa cross mojaa ....hatari hatarii kwenye mlango wa timu ya kijani. Inapiigwaa shuti moja kipa anaipanchi, inapigwa shuti lingine kipa ameruka amegonga kichwa kwenye mwamba.,.......eeh eeh....leo ndio leo, mtoto hatumwi sokoni.

Namwona kipa anagalagala pale golini. Watoa huduma ya kwanza wanaenda na machela. Wanamganga hapaa....kaaazi kweli kweli. Hebu tuwapeleke studio kwa ajili ya matangazo.
Kuna goli la mkono limeandaliwa hapa, si bure. Kipindi upo studio refa aliitwa pembeni akanong'onezwa na kamisaa na kuinua kichwa ishara ya kukubali.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom