Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Ndugu watanganyika wenzangu wana wa JF, Hebu tukae chini na kujadili japo kwa uchache kuhusu moja kati ya madai ya ndugu zetu Wazanzibar wanaowakilishwa na wana wa UAMSHO katika harakati za kudai uhuru wa nchi yao.
Tujadili kwa amani bila jazba wala kuingiza kashfa kutoka dini moja kwenda nyingine. Jambo moja tu, nalo ni dai lao hili hapa chini
(Maili 20 kuingia ndani ya jiji la Dar es salaam ni ardhi ya Zanzibar)
Kwa hesabu za haraka haraka kama unaenda Morogoro, bila shaka ni mpaka maeneo ya Kimara au Kimara Suka hivi.
Maili 20 kutoka fukwe za bahari ya hindi kuingia katikati ya jiji la Dar es salaam ni ardhi ya Zanzibar. Hayo ni madai ya kushangaza kutoka kundi la UAMSHO, Ni dai lenye kila dalili kuwa lina chokochoko zaidi ya lile dai lao la msingi la kutaka kuuvunja muungano. Pamoja na madai mengine kutoka kwa wanajumuia wanaojiita UAMSHO.
Hili ndilo moja kuu ambalo kwa upande wangu naona linatisha zaidi, bila ya shaka hii taarifa ni ngeni sana miongoni mwa watanganyika lukuki ambao wanaijua vizuri historia ya nchi yao. Sijaona sababu ya mamlaka zinazohusika kuyakalia kimya na kuyapuuza madai ya ajabu kama haya.
Kuna kauli za kupuuzwa kutokana na aina ya mtoaji kauli mwenyewe, kwa kuwa kundi hili la UAMSHO limeonyesha kuwa lina dhamira ya dhati ya kudai Zanzibar huru na matokeo ya dhamira yao yameonekana kwa kuteketeza majumba ya ibada ya watu wa imani nyingine, pamoja na kuharibu mali za watu wasio na hatia.
Sioni sababu ya kupuuzwa maneno ya watu hawa hata kidogo. Itakapofikia muda wao wa kuja kudai ardhi yao ambayo wanadai vibali na hati wanazo. Ni mashaka yangu kutakuwa na madhara makubwa hapo baadaye ambayo nina hakika yanaweza kutafutiwa dawa mapema.
UAMSHO ni kundi huru, linalofanya shughuli zake bila uficho likuwa na usajili halali wa serikali. Tofati na makundi kama BOKO HARAM au AL SHABAB. Inashangaza kuona ni kwa nini serikali za jamhuri ya muungano na ile ya mapinduzi Zanzibar wanatoa matamshi mepesi bila ya kuchukua hatua madhubuti za kuwadhibiti watu hawa ambao tayari wameshasababisha madhara makubwa.
Sitarajii kama kutatokea waislamu wa kweli hapa na makini wakatetea aina hii ya makundi na wanaharakati wanaoangamiza bila sababu badala ya kuhubiri amani kama sifa ya mwislamu wa kweli inavyotakiwa iwe.
Tujadili kwa amani bila jazba wala kuingiza kashfa kutoka dini moja kwenda nyingine. Jambo moja tu, nalo ni dai lao hili hapa chini
(Maili 20 kuingia ndani ya jiji la Dar es salaam ni ardhi ya Zanzibar)
Kwa hesabu za haraka haraka kama unaenda Morogoro, bila shaka ni mpaka maeneo ya Kimara au Kimara Suka hivi.
Maili 20 kutoka fukwe za bahari ya hindi kuingia katikati ya jiji la Dar es salaam ni ardhi ya Zanzibar. Hayo ni madai ya kushangaza kutoka kundi la UAMSHO, Ni dai lenye kila dalili kuwa lina chokochoko zaidi ya lile dai lao la msingi la kutaka kuuvunja muungano. Pamoja na madai mengine kutoka kwa wanajumuia wanaojiita UAMSHO.
Hili ndilo moja kuu ambalo kwa upande wangu naona linatisha zaidi, bila ya shaka hii taarifa ni ngeni sana miongoni mwa watanganyika lukuki ambao wanaijua vizuri historia ya nchi yao. Sijaona sababu ya mamlaka zinazohusika kuyakalia kimya na kuyapuuza madai ya ajabu kama haya.
Kuna kauli za kupuuzwa kutokana na aina ya mtoaji kauli mwenyewe, kwa kuwa kundi hili la UAMSHO limeonyesha kuwa lina dhamira ya dhati ya kudai Zanzibar huru na matokeo ya dhamira yao yameonekana kwa kuteketeza majumba ya ibada ya watu wa imani nyingine, pamoja na kuharibu mali za watu wasio na hatia.
Sioni sababu ya kupuuzwa maneno ya watu hawa hata kidogo. Itakapofikia muda wao wa kuja kudai ardhi yao ambayo wanadai vibali na hati wanazo. Ni mashaka yangu kutakuwa na madhara makubwa hapo baadaye ambayo nina hakika yanaweza kutafutiwa dawa mapema.
UAMSHO ni kundi huru, linalofanya shughuli zake bila uficho likuwa na usajili halali wa serikali. Tofati na makundi kama BOKO HARAM au AL SHABAB. Inashangaza kuona ni kwa nini serikali za jamhuri ya muungano na ile ya mapinduzi Zanzibar wanatoa matamshi mepesi bila ya kuchukua hatua madhubuti za kuwadhibiti watu hawa ambao tayari wameshasababisha madhara makubwa.
Sitarajii kama kutatokea waislamu wa kweli hapa na makini wakatetea aina hii ya makundi na wanaharakati wanaoangamiza bila sababu badala ya kuhubiri amani kama sifa ya mwislamu wa kweli inavyotakiwa iwe.