Dah...sikuwa najua hili...msamaa wa gharama za matibabu muhimbili

Hhm

Member
Apr 28, 2010
69
14
Kwakweli jambo usilolijua ni kama usiku wa giza...siku zooote tunaposikia misamaha ya kodi tunaelewa na ndivyo ilivyo there is some one who is paying that tax on behalf of the person who is exempted...sasa hili kwa upande wa Hospitali zetu nchini kumbe ni tofauti .... Mgonjwa anapopewa msamaha yaaani anatibiwa bure hakuna mamlaka yoyote serekalini inalipa au kufidia gharama za matibabu kwa Mgonjwa aliyepewa msamaha jambo ambalo Hospitali zetu nchini huduma zinazidi kudorora....chakusikitisha zaidi ni pale niliposikia kuwa hili swala la msamaha hata watu kama viongozi wa kisiasa kama wabunge mawaziri hupewa exemption Hospitali ya taifa Muhimbili.... Hii sidhani kama Ndiyo ilikuwa dhana mzima ya exemption kama ilivyowekwa na serikali....naamini kuwa sababu kubwa ya serikali kuweka utaratibu huu ni ili kusaidia watu wale ambao kwakweli hawana uwezo kabisa lakini kwa Hospitali ya taifa muhimbili ni mpaka mbunge anapewa msamaha jambo ambalo ni mzigo mkubwa kwa Hospitali zetu...gharama za matibabu ziko juu sana na endapo serekali isipokuwa makini itafikia mahali Hospitali zitashindwa kutoa huduma...kuna haja ya serekali kuuangalia utaratibu wa misamaha ya malipo ya tiba kwa upya kwasababu people abuse the system. Mtu kama mbunge au waziri kwanini atibiwe view?? Madawa na reagent za maabara zinazotumika kumpa tiba yanarudishwaje? Hata hao wafadhili wanaotusaidia jamani misaada ina mwisho. Kama mtu akipewa msamaha wa kodi kwa gari alilonunua haimaanishi kuwa ile kodi hailipwi kuna mamlaka inalipa kwa niaba yake...sasa inakuwaje kwa huduma za Hospitali??
 
Ni jambo la kamaida hapa bongo. Misamaha huwahusu zaidi wakubwa tena wenye mauwezo na sio uwezo. Chunguza uone mwenye nacho ndie anaepitisha mizigo bandarini free, haohao ndo wanaopelekana matibabu nje free. Hata akitaka kiwanja mwendo ndo huohuo. Katoto ka mkulima kanaumwa, kanahitaji milioni 2tu kapelekwe India kwa matibabu wizara ya afya itakwambia haina hela. Jioni yake mke wa waziri fulani kakoboka uso kwa mkorogo, anakodishiwa ndege kumwahisha ujerumani kwa matibabu. Hii ndio bongo ndg yangu.ishu sio kuingia tu uwanja wa mpira bali ishu ni je umekalia viti vya rangi gani?
 
Hii sasa watanzania lazima ifikie mahali tuseme basi....ukifika Hospitali ya taifa Muhimbili kibasila mwaisela na ukajionea hali ilivyo ukiuliza wimbo ni serekali haina hela...na hapo hapo kuna wafadhili wanafadhili maeneo ambayo ni muhimu kwa uzalishaji hospitalini kama maabara....yaani eti wanapewa reagent za mashine za uchunguzi wa magonjwa bure spea za mashine hizo bure, preventive maintenance service ya facilities karibu zote wanalipiwa na wafadhili .... Jambo la ajabu ni kwamba pesa zinazopatikana siyo kwamba zinarudi kwenye mzunguko wa kusuport hizo services No!! Zinaingia kwenye mfuko wa Hospitali na zitatumika kwa matumizi ya Hospitali yaani maeneo mengine ambayo mfadhili hasuport...na cha ajabu zaidi eti serikali haipeleki pesa kulingana na mahitaji ya Hospitali na hapo hapo waziri au mbunge au memo inatoka wizara ya afya mkubwa flani anakuja atibiwe bure...ikumbukwe kuwa kipimo kimoja tu cha maabara kinaweza kufikia 60000/- na hapo bado mri sijui nini yani mpaka Mgonjwa anatoka gharama alizoipa Hospitali siyo chini ya 2 milion...halafu BURE...Tutafika kweli??? Yaani kama utaratibu wa msamaha wa matibabu muhimbili usipoangaliwa upo siku huduma zitakwama....
 
Back
Top Bottom