Dah..Nimekutana na mtu eti kaniambia pole kwa msiba, msiba wa nani? Ruge

Johnny Sack

JF-Expert Member
Jan 21, 2017
8,780
18,747
Ebanae leo nilikutana na jamaa kaniambia pole kwa msiba, nikamuuliza msiba gani? Kaniambia eti wa Ruge,sasa nikajiuliza Ruge ananihusu nini mimi?
Najua kasaidia wengi, wasanii, wafanyakazi wa clouds,viongozi wa CCM n.k, ila mimi kanisaidiaje?

Mwingine nikakutana nae akaniambia kwa nini sikuenda msibani? Nikauliza msiba gani? (Japo nilishajua anamaanisha wa Ruge)

Akanijibu wa Ruge, sasa nikashangaa tena zaidi, nikamuuliza kwani msiba unanihusu nini mimi?

Akaniambia amewasaidia Watanzania wengi na mimi nikiwemo, dah, sikutaka kubishana sana nikajibu tu nilikuwa bize
Wakati nikikubali na kunuheshimu sana marehemu kawasaidia wengi, ila hili jambo limekuzwa sana (sababu ya yeye kuwa mtu wa media)

Hii sio mara ya kwanza, kwa Watanzania kukuza misiba hivi, tuliona Masogange ambaye alikuwa ni video queen na mtu anayetupia picha za kutamanisha kingono mtandaoni msiba wake ukikuzwa sana kiasi kwamba hadi Rais kupeleka salamu za rambirambi

Nikajiuliza sana hivi Watanzania tuna IQ ndogo kiasi hiki?

Yaani propaganda za media zinatuaminisha kirahisi kuwa mtu fulani ni muhimu japo ipo wazi kabisa sio muhimu?
Kuna mtoto mwingine aliitwa Patrick, basi na msiba wake ukageuka kuwa msiba wa taifa, unajiuliza kwani huyu alikuwa ni nani?
Kumbe alikuwa akitupia picha mtandaoni..
 
NASIKIA NA UN WAMETUPA POLE

We join the rest of the country in mourning the loss of Ruge Mutahaba.

We were very happy to have worked with him to spread the message of the #GlobalGoals all over #Tanzania.

R.I.P. Ruge
1f64f-1f3fc.png
@ALVARO_UNTZ
 
Kuna powerful people, wakiamua uwe famous unakua ndani ya siku mbili tu,hadi mnajiuliza "jamaa katoka kimaisha fasta kafanya nini" hata usipate alichofanya,
na wakiamua upotee hata kama umewekeza kiasi gani unapotea in a day!! wao ndo NYOTA wakiamua uwake unawaka na wakiamua uzime unazima mapemaaaaa. so mchizi kupaishwa ni juhudi za hao watu nyuma ya pazia huwa hawaonekani.
 
Ebanae leo nilikutana na jamaa kaniambia pole kwa msiba, nikamuuliza msiba gani? Kaniambia eti wa Ruge,sasa nikajiuliza Ruge ananihusu nini mimi?
Najua kasaidia wengi, wasanii, wafanyakazi wa clouds,viongozi wa CCM n.k, ila mimi kanisaidiaje?

Mwingine nikakutana nae akaniambia kwa nini sikuenda msibani? Nikauliza msiba gani? (Japo nilishajua anamaanisha wa Ruge)

Akanijibu wa Ruge, sasa nikashangaa tena zaidi, nikamuuliza kwani msiba unanihusu nini mimi?

Akaniambia amewasaidia Watanzania wengi na mimi nikiwemo, dah, sikutaka kubishana sana nikajibu tu nilikuwa bize
Wakati nikikubali na kunuheshimu sana marehemu kawasaidia wengi, ila hili jambo limekuzwa sana (sababu ya yeye kuwa mtu wa media)

Hii sio mara ya kwanza, kwa Watanzania kukuza misiba hivi, tuliona Masogange ambaye alikuwa ni video queen na mtu anayetupia picha za kutamanisha kingono mtandaoni msiba wake ukikuzwa sana kiasi kwamba hadi Rais kupeleka salamu za rambirambi

Nikajiuliza sana hivi Watanzania tuna IQ ndogo kiasi hiki?

Yaani propaganda za media zinatuaminisha kirahisi kuwa mtu fulani ni muhimu japo ipo wazi kabisa sio muhimu?
Kuna mtoto mwingine aliitwa Patrick, basi na msiba wake ukageuka kuwa msiba wa taifa, unajiuliza kwani huyu alikuwa ni nani?
Kumbe alikuwa akitupia picha mtandaoni..
Hahahah watasema unamuonea wivu marehemu.
 
Back
Top Bottom