Slave
JF-Expert Member
- Dec 6, 2010
- 5,314
- 2,635
Kuna msukuma mwenzangu huku nilipo,ni tajiri sana wa ng'ombe mzee huyu haja soma hata lile darasa la popo hata kiswahili cha kuombea maji hajui ila humdanganyi kitu katika kujua hesabu ya ng'ombe zake. Cha mno zaidi mzee huyu kahifadhi namba za simu za watu wengi kichwani.juzi nilikutana nae na kumuliza kama anayo namba ya simu ya -- akaniambia anayo na kuanza kunitajia kwa kisukuma akimanisha; ;ya kwanza ipo kama yai(0) ya pili kama fyekeo (7) ya tatu kama mashikio ya mkasi (8) ya nne kama mtu kachuchumaa (4) na....mzee alitaja mpaka namba zote kwa mtindo huo.