Pre GE2025 Daftari la wapiga kura na kitambulisho kimoja tu cha kura ni urasimu unaopunguza wapiga kura na kufifisha demokrasia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
46,820
67,193
Hiki kinachoitwa kujiandikisha katika daftari la wapiga kura kwa raia wote waliokidhi vigezo na wanaohitaji kupiga kura ni aina fulani ya kituko na jambo lisilo na tija yoyote katika demokrasia zaidi ya kupunguza ushiriki wa raia katika uchaguzi kwa urasimu wa ajabu ajabu tu.

Pia ni upotezaji wa pesa za walipa kodi tu kwa gharama zisizo na mashiko yoyote.

Watanzania walio na vitambulisho kama NIDA, Passport na leseni ya udereva walitakiwa waweze kupiga kura kwa hivi vitambulisho vyao, hakuna haja ya kwenda kupanga mstari tena sijui kujiandikisha au kuboresha daftari la wapiga kura.
 
Hiki kinachoitwa kujiandikisha katika daftari la wapiga kura kwa raia wote waliokidhi vigezo na wanaohitaji kupiga kura ni aina fulani ya kituko na jambo lisilo na tija yoyote katika demokrasia zaidi ya kupunguza ushiriki wa raia katika uchaguzi kwa urasimu wa ajabu ajabu tu.

Pia ni upotezaji wa pesa za walipa kodi tu kwa gharama zisizo na mashiko yoyote.

Watanzania walio na vitambulisho kama NIDA, Passport na leseni ya udereva walitakiwa waweze kupiga kura kwa hivi vitambulisho vyao, hakuna haja ya kwenda kupanga mstari tena sijui kujiandikisha au kuboresha daftari la wapiga kura.
Watu wako bize na maokoto!
 
Swala lingine lililo kaa kikanjanja ni kulazimisha MTU apige kura sehem aliyojiandikisha pekee...hii kufanya wale watakao kuwa sehem tofaut na eneo la kujiandikisha kushindwa kupiga kura...hii inafanya CCM iendelee kutawala kirahisi... kwa maana wanakuwa na wapiga kura wa aina moja miaka yote...
 
Swala lingine lililo kaa kikanjanja ni kulazimisha MTU apige kura sehem aliyojiandikisha pekee...hii kufanya wale watakao kuwa sehem tofaut na eneo la kujiandikisha kushindwa kupiga kura...hii inafanya CCM iendelee kutawala kirahisi... kwa maana wanakuwa na wapiga kura wa aina moja miaka yote...

Mkuu upo sahihi sana, sijui kwa nini wanasiasa wa upinzani hawatetei haki za msingi kama hizi

inatakiwa mtu akijiandikisha awe huru kupiga kura ktk kituo chochote maana kadi atakuwa nayo yenye namba inayotambulika ktk mfumo
 
Mkuu upo sahihi sana, sijui kwa nini wanasiasa wa upinzani hawatetei haki za msingi kama hizi
Kwa sababu raia wengi hawajali sana haya mambo pamoja na umuhimu wake mkubwa.
 
Hiki kinachoitwa kujiandikisha katika daftari la wapiga kura kwa raia wote waliokidhi vigezo na wanaohitaji kupiga kura ni aina fulani ya kituko na jambo lisilo na tija yoyote katika demokrasia zaidi ya kupunguza ushiriki wa raia katika uchaguzi kwa urasimu wa ajabu ajabu tu.

Pia ni upotezaji wa pesa za walipa kodi tu kwa gharama zisizo na mashiko yoyote.

Watanzania walio na vitambulisho kama NIDA, Passport na leseni ya udereva walitakiwa waweze kupiga kura kwa hivi vitambulisho vyao, hakuna haja ya kwenda kupanga mstari tena sijui kujiandikisha au kuboresha daftari la wapiga kura.

Suala la kujiandikisha au maboresho la daftari la wapiga kura ni kutambua idadi kamili kwa watakao piga kura, ili kuongeza wapya na kuondoa walio kufa. Ili jambo ni muhimu na hilo daftari lina umuhimu wake

suala la mpiga kura kutumia kitambulisho cha nida, paspoti, leseni ya udereva hilo lifanyiwe tathmin kama litafaa maana vyote hvyo ni vitambulisho vya serikali
 
Watu wako bize na maokoto!

Mwaka huu, watu watajiandikisha wengi ili wapate vitambulisho kwaajiri ya matumizi mengine lakini mwamko wa watu kupiga kura siku ya uchaguzi ni mdogo
  • washindi wameshajulikana
  • raia wengi hawapendi kujihusisha na siasa
  • vyama vya upinzani havina hoja na mwelekeo

wengi watakaopiga kura ni watu wa ccm maana wana hamasa, wanapewa bakshish, hawajitambui, wanaamin wao ndio watawala
 
Suala la kujiandikisha au maboresho la daftari la wapiga kura ni kutambua idadi kamili kwa watakao piga kura, ili kuongeza wapya na kuondoa walio kufa. Ili jambo ni muhimu na hilo daftari lina umuhimu wake
Wale wote weny NIDA, passport ambazo hazija expire na leseni za udereva zilizo hai wanatakiwa wahesabiwe kama ni wapiga kura watarajiwa tayari. Wale wasio na hivi vitambulisho ndio wakajiandikishe katika daftari la wapiga kura na wapatiwe kitambulisho cha kura.
 
Mwaka huu, watu watajiandikisha wengi ili wapate vitambulisho kwaajiri ya matumizi mengine lakini mwamko wa watu kupiga kura siku ya uchaguzi ni mdogo
  • washindi wameshajulikana
  • raia wengi hawapendi kujihusisha na siasa
  • vyama vya upinzani havina hoja na mwelekeo

wengi watakaopiga kura ni watu wa ccm maana wana hamasa, wanapewa bakshish, hawajitambui, wanaamin wao ndio watawala
Kuna mahali nimepita jana nikakuta kuna mkusanyiko mkubwa wa watu wamevaa Tshirts na kofia zimeandikwa majina ya kiongozi fulani wao wakijitapa kuwa mheshimiwa kawapa majiko ya gas na shs 50,000/= kila mmoja. Na amewasafirisha kutoka huko na huko kwa mabasi na malori! Na kweliagari yalijaa pomoni. Hiviiii TAKUKURU wanafanya kazi kwa mfumo upiiii? Au mpaka mtu aseme kuwa mahali fulani kuna harufu ya rushwa ndiyo waende kunusa? Au wananusa wenyewe na kugundua kuwa mahali fulani kuna rushwa kisha kuchukua?Matukio ya jana pale kwa maoni yangu ilikuwa ni rushwa bab kubwa!! Na hasa ukiangalia walengwa/wanufaika inafikirisha!!
 
Swala lingine lililo kaa kikanjanja ni kulazimisha MTU apige kura sehem aliyojiandikisha pekee...hii kufanya wale watakao kuwa sehem tofaut na eneo la kujiandikisha kushindwa kupiga kura...hii inafanya CCM iendelee kutawala kirahisi... kwa maana wanakuwa na wapiga kura wa aina moja miaka yote...
Hili haliwezekan kwa sbb mtu anaweza akachaguliwa na watu wasio wakazi wa eneo husika kwenye serikali za mitaa
 
Hili haliwezekan kwa sbb mtu anaweza akachaguliwa na watu wasio wakazi wa eneo husika kwenye serikali za mitaa
Kwa nini mtu ajisumbue kwenda kumpigia kura mwenyekiti wa mtaa, diwani au mbunge asiyemuhusu huku akiacha kuwapigia kura watu wake wanaomuhusu??
 
Umesema kweli! Mtu una kitambulisho cha NIDA why Vote card?
Ambao walipaswa kutumia Vote cards ni wale ambao hawana vitambulisho vya NIDA kwa sababu yo yote ili mradi wawe watanzania.
 
Back
Top Bottom