Daddy change the World: Baadhi ya Watanzania waomba wazazi wao wauawe kikatili ili wanufaike

TODAYS

JF-Expert Member
Apr 30, 2014
13,740
21,183
Mapema leo kaka yake marehemu Goerge Flyode ameliomba shirika la umoja wa mataifa kuangalia jinsi gani watu/waamerika weusi wanakuwa salama ili kulinda usalama wa wao duniani.

20200617_185921.png


Gianna Flyod pichani juu, akiwa amevaa t-shirt ikionyesha picha ya marehemu baba yake kilichotokana na kuuliwa na askali wa kizungu kwa kukandamizwa shingoni kwa takribani dakika 8 na 46 sekunde, ameendelea kupata misaada mbalimbali kutoka kwa watu na taasisi mbalimbali.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya taarifa, maisha ya binti huyo mdogo yanaendelea kuwagusa watu na makampuni tofauti ambayo yamejitokeza na kutoa sapoti mbalimbali, sapoti kubwa imetolewa mwanahisa na mmilili wa kampuni kubwa ya utengenezaji wa filamu ijulikanayo kwa jina la Disney Studio.

Babra Streisand ni mwanahisa ambaye amejitolea kumpa sehemu ya hisa za kampuni hiyo ili kuonyesha hisia zake kutokana na kifo cha baba yake.

👇Pichani Gianna akiwa na cheti cha hisa cha umiliki wa kampuni ya Disney huku akimshukuru Babra.
20200617_181353.png


Kufuatia kuneemeka kwa binti huyo baadhi ya watanzania kupitia mitandao ya kijamii wamejaribu kuwa na hisia zao kama huyu hapa: 👇
20200617_203414.png
 
😃😃😃 wa tz bwana

wamesahau kuwa wanaomba baba zao wafe kikatili katika ardhi ya tz...

huku wataishia kuchezea kichapo tu na hakuna hata watakaye muona akiwapa michango
 
Back
Top Bottom