Frustration
JF-Expert Member
- Jan 30, 2018
- 3,095
- 4,059
Habari wanajukwaa hili la Afya.
Nina dada ambaye anasumbuliwa sana na hali ya kubanwa na pumzi na kushindwa kuongea. Mara ya kwanza alinitumia sms kuwa halu yake ni mbaya anashindwa kupumua na anahisi kunakitu kinatembea toka kifuani hadi mgongoni.
Hali hii ilikuja kutulia baada ya nusu saa.
Leo amenipigia tena simu ila nilisikia tu akihema kwa sauti ya juu bila ya kuongea chochote. Nimewahi na nimekuta analia kwa sauti ya chini,huku akilalama mbavu zinambana. Alikuwa hawezi kuinuka ila nilifankisha kumpandisha kwenye pikipiki hadi hospitali ya Rufaa ya Songea mjini.
Tumeenda kwa daktari na akashauri tukachukue kipimo cha X ray ila kwa ushauri wa mgonjwa kasema amewahi kupimwa mbavu na maumivu ya uti wa mgongo kwa X ray ila hakukuwa na injury yoyote.
Anasema awali alipimwa aliambiwa ana UTI sugu na kuna dawa aliambiwa atumie. Vipimo hivi walivichukua Tanga na aliandikiwa dawa na sindano. Gynazol tb ni dawa aliyoandikiwa ila sindano hatujui Kwa kuwa kadi yake ameiacha Tanga kwa kuisahau.
Hali hii inamtokea wakati hata akisukumwa kidogo tu.
Naomba msaada wenu
Ahsanteni
Nina dada ambaye anasumbuliwa sana na hali ya kubanwa na pumzi na kushindwa kuongea. Mara ya kwanza alinitumia sms kuwa halu yake ni mbaya anashindwa kupumua na anahisi kunakitu kinatembea toka kifuani hadi mgongoni.
Hali hii ilikuja kutulia baada ya nusu saa.
Leo amenipigia tena simu ila nilisikia tu akihema kwa sauti ya juu bila ya kuongea chochote. Nimewahi na nimekuta analia kwa sauti ya chini,huku akilalama mbavu zinambana. Alikuwa hawezi kuinuka ila nilifankisha kumpandisha kwenye pikipiki hadi hospitali ya Rufaa ya Songea mjini.
Tumeenda kwa daktari na akashauri tukachukue kipimo cha X ray ila kwa ushauri wa mgonjwa kasema amewahi kupimwa mbavu na maumivu ya uti wa mgongo kwa X ray ila hakukuwa na injury yoyote.
Anasema awali alipimwa aliambiwa ana UTI sugu na kuna dawa aliambiwa atumie. Vipimo hivi walivichukua Tanga na aliandikiwa dawa na sindano. Gynazol tb ni dawa aliyoandikiwa ila sindano hatujui Kwa kuwa kadi yake ameiacha Tanga kwa kuisahau.
Hali hii inamtokea wakati hata akisukumwa kidogo tu.
Naomba msaada wenu
Ahsanteni