MALCOM LUMUMBA
JF-Expert Member
- Jul 26, 2012
- 20,897
- 63,783
Kwanza naomba niseme wazi kabisa
Mimi ni kati ya binadamu wanaochukia uonevu na unyonyaji wa binadamu mmoja dhidi ya mwingine. Ile hali ya kuhisi kwamba wewe ni bora na mtu wa maana kuliko wengine (Grandiosity and Megalomania) huwa inanifanya nichafukwe na nyongo sana. Mambo maovu kama ukoloni na taasisi zake hayatakiwi kabisa kuchekewa wala kufunikwa hata kidogo.
Hayatakiwi kufunikwa na kupuuzwa hata kama yalifanywa na watu mashughuli duniani, makabila yetu au hata kupitia taasisi kubwa za kidini ambazo wengi wetu ni waumini. Kiufupi njia sahihi ya kujenga mahusiano mazuri ni kuwa wawazi juu ya hayo mahusiano mnayotaka kuyajenga. Lazima kila upande ukubali wapi ulikosea na kuwajibika kwa asilimia 100%, bila kutafutiza sababu.
Wasomi wengi wa kiafrika tumekuwa na kasumba kubwa mno ya kuyaonea aibu au kupuuza mambo mengi yaliyofanywa na yanayofanywa na jamii za kigeni hapa barani Afrika (wazungu, waarabu, wachina, wahindi na taasisi zao za kidini). Nakubali kabisa waafrika tuna sehemu kubwa katika hili tatizo, lakini kamwe hatujawahi kuoana uwajibikaji wowote kwa upande wa hawa wenzetu ambao chumi zao hutegemea rasilimali za Afrika.
Nadhani dada huyu kazungumza vizuri sana, mahusiano baina ya Afrika na Ulaya ni jambo zuri sana na muhimu lakini lazima tukubali kwamba mengi yamejengwa juu ya msingi wa unyonyaji na ukoloni. Hivyo kuna kutoaminiana na kujistukia tu. Lakini kubwa zaidi ni lile la kuamini kwamba wenzetu wana wajibu wa kutufundisha sisi kuhusu demokrasia, uungwana na utawala bora ilhali wao hawalifanyi hili katika utekelezaji wa sera zao za mambo ya nje na uwekezaji.
Hata wanaharakati na wanasiasa wengi wa Afrika (watawala na wapinzani) hasa nchini Tanzania, nadhani hili wamelifumbia macho na hawajalizungumzia ipasavyo, aidha wakiamini kabisa kwamba kila kinachofanyika na nchi za Ulaya hapa Afrika kiko sahihi, AU matatizo yote ya Afrika yamesababishwa na watawala mafisadi na madikteta wasio na uchungu na uelewa, AU kwasababu nchi za Ulaya ni wadau wetu wakubwa wa maendeleo wakiunga mkono juhudi za serikali na kumwaga mamilioni ya misaada kwa wanaharakati na wapinzani. Inafikirisha sana!
Mimi ni kati ya binadamu wanaochukia uonevu na unyonyaji wa binadamu mmoja dhidi ya mwingine. Ile hali ya kuhisi kwamba wewe ni bora na mtu wa maana kuliko wengine (Grandiosity and Megalomania) huwa inanifanya nichafukwe na nyongo sana. Mambo maovu kama ukoloni na taasisi zake hayatakiwi kabisa kuchekewa wala kufunikwa hata kidogo.
Hayatakiwi kufunikwa na kupuuzwa hata kama yalifanywa na watu mashughuli duniani, makabila yetu au hata kupitia taasisi kubwa za kidini ambazo wengi wetu ni waumini. Kiufupi njia sahihi ya kujenga mahusiano mazuri ni kuwa wawazi juu ya hayo mahusiano mnayotaka kuyajenga. Lazima kila upande ukubali wapi ulikosea na kuwajibika kwa asilimia 100%, bila kutafutiza sababu.
Wasomi wengi wa kiafrika tumekuwa na kasumba kubwa mno ya kuyaonea aibu au kupuuza mambo mengi yaliyofanywa na yanayofanywa na jamii za kigeni hapa barani Afrika (wazungu, waarabu, wachina, wahindi na taasisi zao za kidini). Nakubali kabisa waafrika tuna sehemu kubwa katika hili tatizo, lakini kamwe hatujawahi kuoana uwajibikaji wowote kwa upande wa hawa wenzetu ambao chumi zao hutegemea rasilimali za Afrika.
Nadhani dada huyu kazungumza vizuri sana, mahusiano baina ya Afrika na Ulaya ni jambo zuri sana na muhimu lakini lazima tukubali kwamba mengi yamejengwa juu ya msingi wa unyonyaji na ukoloni. Hivyo kuna kutoaminiana na kujistukia tu. Lakini kubwa zaidi ni lile la kuamini kwamba wenzetu wana wajibu wa kutufundisha sisi kuhusu demokrasia, uungwana na utawala bora ilhali wao hawalifanyi hili katika utekelezaji wa sera zao za mambo ya nje na uwekezaji.
Hata wanaharakati na wanasiasa wengi wa Afrika (watawala na wapinzani) hasa nchini Tanzania, nadhani hili wamelifumbia macho na hawajalizungumzia ipasavyo, aidha wakiamini kabisa kwamba kila kinachofanyika na nchi za Ulaya hapa Afrika kiko sahihi, AU matatizo yote ya Afrika yamesababishwa na watawala mafisadi na madikteta wasio na uchungu na uelewa, AU kwasababu nchi za Ulaya ni wadau wetu wakubwa wa maendeleo wakiunga mkono juhudi za serikali na kumwaga mamilioni ya misaada kwa wanaharakati na wapinzani. Inafikirisha sana!