Dada una miaka 28+ unatoa wapi ujasiri wa kuuliza namba yangu umepata wapi?

Redpanther

JF-Expert Member
Feb 23, 2019
2,813
3,764
Habari gani wadau na wanajamvi wenzangu wa jamvi pendwa la MMU?

Eti mtu nimekuwa napiga naye stori kila mara kwenye ki glosari kimoja hivi. Sasa nikawa nimemuelewa, huyu dada ni mzuri kusema ukweli halafu anakamwili fulani portable sana yaani .

Nikawa namvutia muda tu, basi akawa ananipigisha stori za hapa na pale. Sikumuomba namba, juzi nikaomba namba yake kwa rafiki yake. Daah yule dada bila hiyana hakuninyima maana nikimwambia nimempenda rafiki yako kusema ukweli.

Sasa nimemtafuta huyu dada, nakwambia kakomalia eti nimwambie nani kanipa namba yake. Swali ni kwamba, una miaka 28+ hujaolewa, uko single unapata wapi jeuri ya kumkomalia mwanaume akuambie amepewa na nani namba yake?

Seriously

Kuweni serious basi dada zetu.

1623912014903.png

 
Sio kawaida mtu usiyemfahamu awe na namba yako lazima uulize ameipata wapi? Hata kama ana miaka 40+,na yupo single.Tabia ya kugawa namba za watu bila ruhusa ya muhusika ni mbaya.Je kama wewe ni stalker je?Huyo alokupa namba amefanya makosa!

Kitu kingine yaani wewe umekosa ujasiri hata wa kuomba namba mpaka upewe na mtu mwengine!Tatizo ni nini?
 
Sio kawaida mtu usiyemfahamu awe na namba yako lazima uulize ameipata wapi?Hata kama ana miaka 40+,na yupo single.Tabia ya kugawa namba za watu bila ruhusa ya muhusika ni mbaya.Je kama wewe ni stalker je?Huyo alokupa namba amefanya makosa!

Kitu kingine yaani wewe umekosa ujasiri hata wa kuomba namba mpaka upewe na mtu mwengine!Tatizo ni nini?
Watu tuko tofauti kama mimi nina tabia ya kuongea na mtu siku nyingi bila kumuuliza jina lake wala kuuliza chochote kumuhusu. Sometimes akiniuliza jina namwambia utanijua mbeleni kama tutalazimika kuendelea kufahamiana. Mwisho wa siku najua jina lake kwa kusikia anaitwa, napata namba yake kwa njia yoyote ya utulivu ila sio kwake. Mazingira kama hayo asiponielewa basi kakaza kichwa mwenyewe
 
Sio kawaida mtu usiyemfahamu awe na namba yako lazima uulize ameipata wapi?Hata kama ana miaka 40+,na yupo single.Tabia ya kugawa namba za watu bila ruhusa ya muhusika ni mbaya.Je kama wewe ni stalker je?Huyo alokupa namba amefanya makosa!

Kitu kingine yaani wewe umekosa ujasiri hata wa kuomba namba mpaka upewe na mtu mwengine!Tatizo ni nini?

Sio bhana..! Nimejitambulisha umenikumbuka labda tulikuwa kwenye party sehemu bado unataka kujua nani kanipa namba yako …! Like seriously
 
Watu tuko tofauti kama mimi nina tabia ya kuongea na mtu siku nyingi bila kumuuliza jina lake wala kuuliza chochote kumuhusu. Sometimes akiniuliza jina namwambia utanijua mbeleni kama tutalazimika kuendelea kufahamiana. Mwisho wa siku najua jina lake kwa kusikia anaitwa, napata namba yake kwa njia yoyote ya utulivu ila sio kwake. Mazingira kama hayo asiponielewa basi kakaza kichwa mwenyewe
Ok lakini kwangu mimi sio kawaida au bora ujitambulishe mimi fulani nimepata nambaako kutoka kwa fulani ningependa tujuane or watsoever lakini sio blah blah coz unaulizwa namba umepata wapi...
 
Ilikuwa ni suala la kumjibu ulipoitoa namba yake,ni jeuri kuuliza hilo swali?
Kwanza we jamaa ni mzembe kama umeshindwa kumface mwanamke ukaomba namba

Wavulana kwanini mna ujinga mwingi namna hii?

Suala sio kumface, jana nilienda tunapokutanaga nikitegemea nitamkuta sikumkuta nikamwambia rafiki yake bhana yule rafiki yako nimempenda. Sasa yeye akasema ni jambo jema, nikamwambia vipi naweza kumpata wapi nikimkosa hapa akasema hafahamu labda anisaidie namba yake kwa sababu tubapigaga stori mara kwa mara hatakuwa na utata. Sasa wewe tumekumushana ukanimumbuka na nimekuambia siku hiyo nilitarajia utakuja hujaja kwenye glosari ninetafuta bamna ya kuwasiliana nawewe unakomaa nikuambie aliyenioa namba yako.
 
Yeah sio mbaya ukisema kama dhamiri yako ni njema!

Ujue iko hivi mkuu, Mimi huwaga sina utaratibu wa kumuomba namba mtu nikiyemuona kwa mara ya kwanza. So nikipata bahati ya kuonana naye hata mara nne hivi napiga naye stori ndio naomba namba ili safari yetu isiwe ngumu sana kuanza kuhangaishana kwa maswali ya watoto wa miaka 18.

Siwezi kuosema dhamiri yangu siku hiyo hiyo asee, nitajitahidi kuwa karibu yako kusoma character na namna vile unavyokuwaga ikitokea mtu kaelezea hisia zake. So nitakuwa karibu yako kwa siku kadhaa, nitakuomba labda twende out mara kadhaa huko ndio nitasema dhamiri yangu.
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom