Dada alivyojielezea kwenye tangazo jipya la tigo kwenye televisheni

Garfield

Senior Member
Jan 13, 2020
109
368
Wakuu habari?

Kuna tangazo jipya la mtandao wa TIGO naliona wiki kadhaa sasa likimuonyesha mwanaharakati mmoja akiacha 10,000 kwa mkewe/mpenzi wake na akimuelewesha kuwa ndio kiasi alichonacho.

Jamaa anarudi magetoni anakuta mama katoa diko la bei mbayaa (ukilinganisha na 10,000 alioacha kama kodi ya meza)

Sasa kuna namna yule dada anamchanganulia yule mwanaharakati amejibana vipi kununua bundle za tigo mpaka akabaki na chenchi ndefu iliotosha kupendezesha meza.

Asee palee anapomuambia "Ndio nilivoitumiaa babaa" kwa sauti ya kudeka na kumtoa nyoka pangoni mpaka kwenye tiles mimi hoii wakuu..!!!

Link ya video ya Tangazo hilo.



Jamani wanawake muwe mnatuongelesha vile kila tukirudi kutoka vibaruani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Unazingua jombaa!

Sent using Jamii Forums mobile app
Sizingui jombaa we angalia tangazo kipindi anatoa maelezo yake nilihamisha macho nikipimishia maneno na kilichopo mezani Sasa hapo kilichokuwa kikiendelea kichwani mwangu jini la vipigo lilikuwa mkabala kufanya yake!.. walahi isingekuwa kujiambia mwenyewe kuwa nitulize mshono hilo tangazo lingebadilika kuwa action movie!
 
Sizingui jombaa we angalia tangazo kipindi anatoa maelezo yake nilihamisha macho nikipimishia maneno na kilichopo mezani Sasa hapo kilichokuwa kikiendelea kichwani mwangu jini la vipigo lilikuwa mkabala kufanya yake!.. walahi isingekuwa kujiambia mwenyewe kuwa nitulize mshono hilo tangazo lingebadilika kuwa action movie!
Hahaha, kama kweli vile

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom