CHIEFMANGU
JF-Expert Member
- Dec 19, 2016
- 499
- 736
Ni siku kadhaa zimepita toka niwasimulie mkasa ulionipata kutoka kwa mdada wa ki Iraq,ahsante Mungu hilo lilipita.
Ninajiuliza nimemkosea nini Mungu wangu,kwa haya ninayoyapitia!!!? Kama wiki mbili zilizopita,nilikutana na mwanamke maeneo ya stand ya mabasi Dodoma,alikuwa mchangamfu sana kwa bahati mbaya huwa sina kawaida ya kujichekesha chekesha kwa wadada hasa nisio wafahamu.
Dada huyu alinichangamkia kupita maelezo nikajiuliza kunani anichangamkie namna hii!!! cha jabu alikuwa akiniita majina yangu,hapo kidogo nikapata ujasiri wa kuongea naye,akajitambulisha pale kumbe ni mtu wa kwetu Mbeya huko,na anatokea kijiji jirani na kwetu,kaka yake nilisoma naye,(baada ya kunikumbusha,nikagundua ni kweli).
Baada ya kufahamiana,tukapanda gari moja (bus)kuelekea Morogoro (ndiko ninakoishi,yeye aliniambia anaishi Kilosa,ni Nurse huko).Tukiwa kwenye gari tuliongea mengi kuhusu kwetu Mbeya,na mwishowe tukabadilishana namba,tulipofika Dumila alishuka,mimi naikaendelea na safari kurudi Morogoro.
Alinitafuta mara kwa mara,akinijulia hali,namimi kadhalika nilimtafuta mara kadhaa kumjulia hali,baadaye aliniuliza maswali kadhaa ya kichokozi,kama kutaka kujua endapo nimeoa au lah,nikamdanganya kuwa nimeoa,juzi aliniambia leo ana safari ya kuja Morogoro mjini,nikamkaribisha.
Leo majira ya saa nne alikuwa safarini kuja Moro,namimi pasipo kuwa na shaka yoyote,nimeenda kumpokea kama ndugu yangu,nimemkaribisha kwangu alipofika na kukuta nipo mwenyewe ameshangaa sana.
Baadaye nikwambia twende tukale kwa kuwa mimi kwangu napika lakini mara chache sana,tukiwa tunakula nikaona macho yake kuna jambo yanaashiria,kwani alikuwa akinitazama macho fulani hivi,nikamuuliza kama ana mahusiano,akaniambia hapana,alishakuwa na mtu lakini walishindana,na sasa yupo single!!
Nikamuuliza kama anaweza kulala leo kwangu,akasita kidogo then akambia "bro ntakuja next week nikae hata siku tatu hivi sio mbaya" nikamsimulia na mkasa ulionipata juu ya muiraq na mama wa mtoto akanipa pole sana,nimemsindikiza akaondoka.akiwa njiani akanitext "nahisi maumivu ya tumbo kama mp hivi" na mimi nikamjibu "Pole sana,una hakika ni mp or chakula nilichokulisha leo?"
Sasa balaa lake ni usiku huu,nikiwa nimekaa zangu nasoma kitabu simu yangu imeita,baada ya kupokea nikasikia sauti ya mwanaume ananiuliza (kwa ustaarabu kabisa)naongea na fulani (anataja jina langu) nikamjibu ndiyo,
YEYE;Unaishi wapi?
MIMI;Kwani wewe ni nani?
YEYE;Wewe nitajie tu,then nitakwambia
MIMI;Siwezi kutoa details zangu ilhali sijui naongea na nani
YEYE;Unamfahamu fulani (anataja jina la yule msichana)
MIMI;Ndiyo namfahamu,kwani vipi?
YEYE;Huyu ni mke wangu,aliniaga anaenda semina,lakini cha ajabu amerudi hapa na sms zako za mapenzi mkizungumzia MP,imekuwaje??
kiukweli nimejikuta napandwa na hasira dhidi ya dada huyu,nimejiuliza kwanini hakuniambia ukweli tuuu,mwenye mke anaonekana haamini kabisa kuwa mkewe sina uhusiano naye wa kimapenzi kutokana na sms alizoziona,mbaya zaidi ni kwamba muda mfupi baadaye jamaa kanipigia simu akiwa anampiga mkewe,namsikia anavyolia na jamaa anamwambia mke wake "nakuua leo,"
Mpaka muda huu sijui ni nini kimeendelea huko,nimekosa amani kabisaa,hata usingizi sipati hata kidogo,ndugu zangu nifanye nini ili nirudi kuwa NORMAL???
Ninajiuliza nimemkosea nini Mungu wangu,kwa haya ninayoyapitia!!!? Kama wiki mbili zilizopita,nilikutana na mwanamke maeneo ya stand ya mabasi Dodoma,alikuwa mchangamfu sana kwa bahati mbaya huwa sina kawaida ya kujichekesha chekesha kwa wadada hasa nisio wafahamu.
Dada huyu alinichangamkia kupita maelezo nikajiuliza kunani anichangamkie namna hii!!! cha jabu alikuwa akiniita majina yangu,hapo kidogo nikapata ujasiri wa kuongea naye,akajitambulisha pale kumbe ni mtu wa kwetu Mbeya huko,na anatokea kijiji jirani na kwetu,kaka yake nilisoma naye,(baada ya kunikumbusha,nikagundua ni kweli).
Baada ya kufahamiana,tukapanda gari moja (bus)kuelekea Morogoro (ndiko ninakoishi,yeye aliniambia anaishi Kilosa,ni Nurse huko).Tukiwa kwenye gari tuliongea mengi kuhusu kwetu Mbeya,na mwishowe tukabadilishana namba,tulipofika Dumila alishuka,mimi naikaendelea na safari kurudi Morogoro.
Alinitafuta mara kwa mara,akinijulia hali,namimi kadhalika nilimtafuta mara kadhaa kumjulia hali,baadaye aliniuliza maswali kadhaa ya kichokozi,kama kutaka kujua endapo nimeoa au lah,nikamdanganya kuwa nimeoa,juzi aliniambia leo ana safari ya kuja Morogoro mjini,nikamkaribisha.
Leo majira ya saa nne alikuwa safarini kuja Moro,namimi pasipo kuwa na shaka yoyote,nimeenda kumpokea kama ndugu yangu,nimemkaribisha kwangu alipofika na kukuta nipo mwenyewe ameshangaa sana.
Baadaye nikwambia twende tukale kwa kuwa mimi kwangu napika lakini mara chache sana,tukiwa tunakula nikaona macho yake kuna jambo yanaashiria,kwani alikuwa akinitazama macho fulani hivi,nikamuuliza kama ana mahusiano,akaniambia hapana,alishakuwa na mtu lakini walishindana,na sasa yupo single!!
Nikamuuliza kama anaweza kulala leo kwangu,akasita kidogo then akambia "bro ntakuja next week nikae hata siku tatu hivi sio mbaya" nikamsimulia na mkasa ulionipata juu ya muiraq na mama wa mtoto akanipa pole sana,nimemsindikiza akaondoka.akiwa njiani akanitext "nahisi maumivu ya tumbo kama mp hivi" na mimi nikamjibu "Pole sana,una hakika ni mp or chakula nilichokulisha leo?"
Sasa balaa lake ni usiku huu,nikiwa nimekaa zangu nasoma kitabu simu yangu imeita,baada ya kupokea nikasikia sauti ya mwanaume ananiuliza (kwa ustaarabu kabisa)naongea na fulani (anataja jina langu) nikamjibu ndiyo,
YEYE;Unaishi wapi?
MIMI;Kwani wewe ni nani?
YEYE;Wewe nitajie tu,then nitakwambia
MIMI;Siwezi kutoa details zangu ilhali sijui naongea na nani
YEYE;Unamfahamu fulani (anataja jina la yule msichana)
MIMI;Ndiyo namfahamu,kwani vipi?
YEYE;Huyu ni mke wangu,aliniaga anaenda semina,lakini cha ajabu amerudi hapa na sms zako za mapenzi mkizungumzia MP,imekuwaje??
kiukweli nimejikuta napandwa na hasira dhidi ya dada huyu,nimejiuliza kwanini hakuniambia ukweli tuuu,mwenye mke anaonekana haamini kabisa kuwa mkewe sina uhusiano naye wa kimapenzi kutokana na sms alizoziona,mbaya zaidi ni kwamba muda mfupi baadaye jamaa kanipigia simu akiwa anampiga mkewe,namsikia anavyolia na jamaa anamwambia mke wake "nakuua leo,"
Mpaka muda huu sijui ni nini kimeendelea huko,nimekosa amani kabisaa,hata usingizi sipati hata kidogo,ndugu zangu nifanye nini ili nirudi kuwa NORMAL???