D.Cameron apakia treni kukwepa gharama!

Nyamgluu

JF-Expert Member
Mar 10, 2006
3,160
1,717
Leo ktk CNN walikua wakiongelea ziara ya waziri mkuu wa uingereza huko USA. Jamaa alipakia treni kutoka washington hadi newyork ili kuonyesha kujali expenses in "his cash strapped country."
Kwa mantiki hio marais wote wa africa wakiwa mtoni ingebidi watembelee treni! No wonder jamaa wanabana usaidizi wao kwetu,ikiwezekana wazuie kabisa.
 
Wangefanya la maana zaidi kama wangeacha kuzinyonya nchi ndogo zinazokabiliwa na umaskini wa kutupa, otherwise hizo zitabakia ni sarakasi tu za kisiasa.
 
maraisi wetu wa afrika hawawezi kufanya kitu kama hicho kwani wao wanataka nafasi ya uraisi kugomboa maisha yaona sio kugomboa nchi.hawana uchungu na nchi zao kihasi cha kujaribu kuepuka gharama kama hizo na ndio maana wanaongezeana mishahara kila kukicha.
 
Marais wetu hata hapa kwetu... hawawezi kufanya hayo...
Wao sio tena wa public transport regardless nchi zao ziko dependency kiasi gani..
Hawafikirii tena juu ya nchi zao miaka 100 ijayo zaidi ni wao familia zao na washkaji...ukiwa mbali nao kama sasa..endelea kulipa kodi waishi vyema..
Tunahitaji viongozi wenye vision za kuiondoa Africa kwenye lindi hili la umaskini wa mali na fikra...
Uwezo tunao...nia thabiti ipo..????
 
Wangefanya la maana zaidi kama wangeacha kuzinyonya nchi ndogo zinazokabiliwa na umaskini wa kutupa, otherwise hizo zitabakia ni sarakasi tu za kisiasa.

Hehe yani wao waache tabia za kutunyonya sisi SIO sisi tuache tabia ya kukubali kunyonywa nao!?
 
Hehe yani wao waache tabia za kutunyonya sisi SIO sisi tuache tabia ya kukubali kunyonywa nao!?
Mkuu,

Naamini wao wanamchango mkubwa zaidi wa kuwa chachu ya mabadiliko kwetu. Ukweli ni kwamba tangia wakae mezani mwaka 1884 kutugawana, hawa mabwana they never let us go mpaka wa leo hii.
 
Sarkozy nae kama wiki mbili zilizopita hakufanya garden party ya revolution day na akasema Ufaransa ita save dola laki tisa kwa party hiyo moja tu........

pata picha mkwere anaacha kufanya viji party ikulu!
 
Marais wetu hata hapa kwetu... hawawezi kufanya hayo...
Wao sio tena wa public transport regardless nchi zao ziko dependency kiasi gani..
Hawafikirii tena juu ya nchi zao miaka 100 ijayo zaidi ni wao familia zao na washkaji...ukiwa mbali nao kama sasa..endelea kulipa kodi waishi vyema..
Tunahitaji viongozi wenye vision za kuiondoa Africa kwenye lindi hili la umaskini wa mali na fikra...
Uwezo tunao...nia thabiti ipo..????
Utamtambuaje kiongozi mwenye nia ya kweli?
Elimu sio kigezo kama mjadala wa ma "Dr" ulivyobaini.
Kuwa na vision nayo si kigezo kwasababu wengi tu wanapanda jukwaani na kuongea vizuri. I cn almst say being visionary is equivilant to being a politician.
Kuangalia "track record" nayo si sawa mana tutazuia vijana wengi katika uongozi bcoz track record means experience.
Sasa NITAMTAMBUAJE!
 
Mkuu,

Naamini wao wanamchango mkubwa zaidi wa kuwa chachu ya mabadiliko kwetu. Ukweli ni kwamba tangia wakae mezani mwaka 1884 kutugawana, hawa mabwana they never let us go mpaka wa leo hii.

Why should they!? They are benefiting from us na bado tunawatukuza why should they stop if we dont make a stance to make them stop! Sio makosa yao ni yakwetu.
Kuna topic ya barua ya botha 1985 kwa wenzake. Ina ukweli mtupu kuhusu fikra za wazungu kwetu. Wanachotofautiana ni degree tu ya imani hiohio ambayo king of apartheid kaisema.
By the way nimeipenda sana ile barua ya botha.
 
sio yeye tu,hata blair nae alikuwa anapanda treni,afrika ilitokea rais wa zambia marehemu mwanawasa alipanda daladala,rais wa zamani wa ghana rawlings aliingia migodini,rais wa burkina faso blaise compaore alifanya mazoezi kucheza mpira na wachezaji wake kama kuwapa changamoto walipokuwa wanaandaa kombe la mataifa huru ya afrika 1998,na hata mawaziri wengi wa ulaya wakienda nchi kama south africa wanakuwa simpo wanajichanganya kwenye pub/baa na watu wa kawaida,david james kipa wa england nae alienda malawi akakaa kule nyuma ktk pick up yani kama mvua inanyesha inamlowesha.
 
sio yeye tu,hata blair nae alikuwa anapanda treni,afrika ilitokea rais wa zambia marehemu mwanawasa alipanda daladala,rais wa zamani wa ghana rawlings aliingia migodini,rais wa burkina faso blaise compaore alifanya mazoezi kucheza mpira na wachezaji wake kama kuwapa changamoto walipokuwa wanaandaa kombe la mataifa huru ya afrika 1998,na hata mawaziri wengi wa ulaya wakienda nchi kama south africa wanakuwa simpo wanajichanganya kwenye pub/baa na watu wa kawaida,david james kipa wa england nae alienda malawi akakaa kule nyuma ktk pick up yani kama mvua inanyesha inamlowesha.

? :eek2: ? Relevance of your post to the topic at hand ni nini? Hao walifanya hivyo kuonyesha kupunguza gharama za serikali yao au kwa sababu zao nyingine. Na david james ana fit vipi hapa?
 
alipakia treni, lakini hiyo treli ilikuwa na ulinzi sawa na ule wanaopewaga wananchi ziku za kawaida?, alikaa kiti sawa na cha wananchi au alikuwa na behewa sepcial?....kiini macho tu hicho. ubepari wameuleta wenyewe halafu wanajifanya kuukwepa.
 
? :eek2: ? Relevance of your post to the topic at hand ni nini? Hao walifanya hivyo kuonyesha kupunguza gharama za serikali yao au kwa sababu zao nyingine. Na david james ana fit vipi hapa?
nataka kukuonyesha wenzetu hawakomplikate maisha hata wakiwa watu maarufu kama sisi wabongo wengi wetu
 
Leo ktk CNN walikua wakiongelea ziara ya waziri mkuu wa uingereza huko USA. Jamaa alipakia treni kutoka washington hadi newyork ili kuonyesha kujali expenses in "his cash strapped country."
Kwa mantiki hio marais wote wa africa wakiwa mtoni ingebidi watembelee treni! No wonder jamaa wanabana usaidizi wao kwetu,ikiwezekana wazuie kabisa.

sio treni tu,hata ndege aliyopanda kuja nayo USA alipanda cheaper business class....cheki hapo chini.

David Cameron’s flight saves £200k | The Sun |News
 
hahaaaa mkwere wetu hakubali kabisa ...apande treni???? mtajuaje yeye ni Raisi wa nji hii
 
alipakia treni, lakini hiyo treli ilikuwa na ulinzi sawa na ule wanaopewaga wananchi ziku za kawaida?, alikaa kiti sawa na cha wananchi au alikuwa na behewa sepcial?....kiini macho tu hicho. ubepari wameuleta wenyewe halafu wanajifanya kuukwepa.

Chukua tano mzee hiyo kweli kabisa manake wanapigia kelele anything relating to communist and still they try to practise it...Hapo ndo unafiki mkali unapoonekana
 
Wakati wa kubana matumizi: Wilaya na Mikoa mipya! Kujenga majumba ya serikali tena;! kukaribisha timu ya Brazil kwa dakika 90 na kulipa mamilioni! Na kadhalika kadhalika!
 
Usanii mtupu, ndio yale yale ya Malechela wakati alipo kua waziri mkuu,kwenda kazini asubuhi sawa na wafanyakazi wengine kuoneysha eti ni mchapakazi kwamba anawahi kazini ,hali iliyo sababisha foleni kubwa sana asubuhi na wengine kucheleweshwa mashuleni na makazini, pia sawa na huyu Chelsea clinton kufunga ndoa siku ambayo wengine wana funga na inasadikiwa kutasababisha njia kufungwa na wengine ku tumia muda mrefu kufika wanapo takiwa, , Imagine JK apande daladala kwenda kazini tutatosha njiani? Na imagine hapo vurugu la Union Station ilikuaje waliifunga u alipanda tuu kama kawaida?
 
alipakia treni, lakini hiyo treli ilikuwa na ulinzi sawa na ule wanaopewaga wananchi ziku za kawaida?, alikaa kiti sawa na cha wananchi au alikuwa na behewa sepcial?....kiini macho tu hicho. ubepari wameuleta wenyewe halafu wanajifanya kuukwepa.



Hapo hata mimi ndio najiuliza, alikodiwa behewa au alipanda na watu kama kawaida , ulinzi ulitumia kiasi gani ukizingatia hizo terror threats.
Sikiwepo enzi hizo ila nasikia marehemu Sokoine alikua na suruali mbili na Viatu pair moja , eti kubana matumizi wakati kafia kwenye Marcedez na kukiwa na msafara mkubwa, sasa sijui hapo ilikua ujamaa upi.
Lipumba naye kuna wakati alitu ambia atasafiri economy class akiwa raisi. aka pingwa na Cheyo vibaya sana .
 
Back
Top Bottom