Cyber crime,viroba baharini; Ndugu zanguni tutumieni mitandao ya kijamii vizuri. Lissu alisema hakuna aliye salama

Hv hao watu wanajuaje kua namba flan imetukana au imecomment neno baya wakati mamilion ya watu wanatumia simu tena kwa wakati mmoja
 
Kwasasa ni zamu yake lkn nauhakika iko siku siku yake watu watakapokuja kudai ndg zao na kuhitaji taarifa zao hapo ndipo patakua patamu
 
Sio mpenzi sana wa kuanzisha uzi ila nimelazimika kuandika uzi siku ya Leo.Sababu zilizonisukuma kuandika uzi ni kuhusu chalii mmoja hapa kapagawa baada ya kupigiwa simu na kuambiwa aripoti makao makuu kitengo cha cyber kusaidia upepelezi na kuhojiwa,..jamaa anachokumbuka Mara ya mwisho ali-like post ya Mange mwanzo nilidhani ni matapeli ila hali inaonyesha ni kweli japo jamaa anasema alitoa like tu na hakuna mahala alicomment au kupost ,ila itakua alienda further japo sijui

Siku chache nyuma kuna MTU huku mtaani alimtuhumu rais kuwa ana mkono kwenye tukio la Lissu kilichotokea jamaa kachukuliwa na watu wasiojulikana huku mashuhuda wakishuhudia na watu wamemtafuta vituo vyote vya polisi wamemkosa hawajui atakua wapi na imepita mawiki haijulikani yupo hai,kwenye viroba au kafa.

Hii ni mifano michache ila nina mifano 2 mingine ambayo ni worse haifai kuzungumza ya watu kupotea baada ya kushindwa kuzuia midomo yao.

Ndugu zanguni wana JF ,wananchi nawapendeni sana chungeni midomo yenu na tumieni facebook na Instagram vizuri majamaa wapo active ,msi comment na kupost vitu vya kuwashwa washwa kwenye mitandao ya fb na Instagram kwa manufaa yako na familia yako na pia chunga mdomo wako kwenye hadhira ya watu hata kama unawashwa washwa .


Kama watu wanachukuliwa na kupotea hovyo halafu hawaonekani vituoni wanakwenda wapi ? Watu 2 wamepotea kwa kuisema hovyo régime na mashuhuda wameona wakichukuliwa lkn cha kushanga vituo vyote wametafutwa wamekosekana halafu juzi tunaona watu wamefungwa vitambaa vyeusi na wamefungwa kwenye viroba na kudumbukizwa baharini na taarifa hazitolewi mpaka wavuvi walipoamua kutoa taarifa kwenye media ..

Kama hawapo vituoni wanakuwaga wapi ???

Sasa na wewe kwa kuandika hayo maneno hapa kwenye JF si utakuwa umejihatarishia maisha? Maana na wewe si watakuteka pia. Au pengine wewe ni mmoja wao hao "wasiojulikana". Upo hapa kututegea ss wananchi
 
kwa jf hadi sasa hakuna aliye potea ila huko facebook wengi wanapotea sababu kwenye account zao wameweka ndugu zao na marafiki na icha zao hivyo ni rahisi kufatiliwa
 
Kama hupendi udikteta bora ubaki JF tu

Ndugu yangu kwa sheria mpya iliyopitishwa bunge hivi karibuni, huu ndio mwisho wa mitandao kama JF ambapo mtu unaweza ukasema lolote. Muda si mrefu JF inaweza ikafungiwa kama magazeti tanavyofungiwa usambazaji. This is the beginning of the end of free speech in Tanzania as we know it. Fuckin Hell..!!!
 
Back
Top Bottom