CWT yaanza kusambaza ujumbe wa simu (sms) za mgomo kwa walimu nchi nzima

Sitachoka

JF-Expert Member
Nov 17, 2011
3,030
1,303
HEBU TIZAMA TOFAUTI HII YA KUTISHA YA VIWANGO VYA MISHAHARA KWA WATUMISHI WA UMMA WA TZ! (Ajira mpya cheti)

Mwl 244,400/= Afya 472,000/= Kilimo/mifugo 959,400/= Sheria 630,000/=


Diploma mwl 325,700/= Afya 682,000/= KLM/MFG 1,133,600/= sheria 871,500/=


degree mwl 469,200/= Afya 802,200/= Klm/MFG 1,354,000/= Sheria 1,166,000/= Je upo tayari kuvumilia kunyanyaswa hivo katika utumishi wa umma wa taifa moja lenye soko la bidhaa lililo na mfumuko wa bei wa kutisha? Ungana na Cwt kudai nyongeza ya mishahara 100%, Teaching allowance hardship allowance. Wape sms hii walimu 20 tu! Mshikamano daima.
 
hawana kitu hawa wakitwa kwenye kikao cha majadiliano na kupewa sitting allowance zao inakuwa basi kuna badhi wanaamini kuwa CWT ni tawi/jumuhiya ya chama
 
Kinachofurahisha ni kuwa kila mara Walimu huwa wanajiandaa kugoma kisha wananyong'onyea taratibu. Nilipozungumza na baadhi yao kwa nini wakasema huwa wengi wamecheza kanyanga kwenye vyeti kwa hiyo wanajua wakiweka msimamo mchujo ukaanza wataumbuka wengi.

Hata hivyo nashauri kuwa ikiwa umeshasajiliwa, kubwa ni kusimamia haki, haijalishi vitisho ni heri kufa kishujaa. Swali ni kuwa ili kupata watu wa afya, mifugo sheria nk, je wanahitaji waalimu kuwafikisha hapo; ikiwa ndivyo basi waalimu wana mahali pa kuanzia.
 
Kinachofurahisha ni kuwa kila mara Walimu huwa wanajiandaa kugoma kisha wananyong'onyea taratibu. Nilipozungumza na baadhi yao kwa nini wakasema huwa wengi wamecheza kanyanga kwenye vyeti kwa hiyo wanajua wakiweka msimamo mchujo ukaanza wataumbuka wengi.

Hata hivyo nashauri kuwa ikiwa umeshasajiliwa, kubwa ni kusimamia haki, haijalishi vitisho ni heri kufa kishujaa. Swali ni kuwa ili kupata watu wa afya, mifugo sheria nk, je wanahitaji waalimu kuwafikisha hapo; ikiwa ndivyo basi waalimu wana mahali pa kuanzia.

point mwana jamii
 
Naskia kuna CWT ASILI na CWT KAMPUNI au cwt original na cwt academia...
Mkishagawanyika namna hii sahauni habari ya kugoma, mtaambiwa ualimu ni wito

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
hawana kitu hawa wakitwa kwenye kikao cha majadiliano na kupewa sitting allowance zao inakuwa basi kuna badhi wanaamini kuwa CWT ni tawi/jumuhiya ya chama
mkuu umesema kweli kabisa viongoz wa cwt ndio wanaotuangusha sisi waalim but hata wao sasa hivi tutawatoa na tutadai haki yetu hadi kieleweke
 
HEBU TIZAMA TOFAUTI HII YA KUTISHA YA VIWANGO VYA MISHAHARA KWA WATUMISHI WA UMMA WA TZ! (Ajira mpya cheti)

Mwl 244,400/= Afya 472,000/= Kilimo/mifugo 959,400/= Sheria 630,000/=


Diploma mwl 325,700/= Afya 682,000/= KLM/MFG 1,133,600/= sheria 871,500/=


degree mwl 469,200/= Afya 802,200/= Klm/MFG 1,354,000/= Sheria 1,166,000/= Je upo tayari kuvumilia kunyanyaswa hivo katika utumishi wa umma wa taifa moja lenye soko la bidhaa lililo na mfumuko wa bei wa kutisha? Ungana na Cwt kudai nyongeza ya mishahara 100%, Teaching allowance hardship allowance. Wape sms hii walimu 20 tu! Mshikamano daima.

nimezisambaza zaidi za 150 mpaka sms za bure zikakata.
 
Tatizo la walimu ni waoga kama makondoo. Yaani tunapangana kabisa tugome, lakini mwisho wa siku tukitishiwa kidogo tu ndiyo tunaanza kukatishana tamaa. Hii sekta itabaki ya kimasikini daima kwa kuwa walimu hawana solidarity kabisa. Sasa mwaka ule mmeandaa kila kitu ilikuwaje muache mgomo eti kutokana na order ya mahakama? Who is mahakama bwana mbele ya kudai haki halali tuliyonyimwa for years?
 
Naskia kuna CWT ASILI na CWT KAMPUNI au cwt original na cwt academia...
Mkishagawanyika namna hii sahauni habari ya kugoma, mtaambiwa ualimu ni wito

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

kaka hii cwt ndio iliyojaa wake za makatibu wakuu, wakurugenzi na hata mawaziri so usitegeme hawa watakuwa nyuma ya mwalim mnyonge anayekatwa almost 16% ya msahara wake kwa ajili ya cwt ambayo haina manufaa kwake. yeye anaallowance mpaka za mafuta ya kumleta kazini pasi kutumia mshahara wake anaish kwa mgongo wa mume lol. siipend hata kuiskia natafuta wadau wanaotaka kujiondoa kama mimi ili kama tunakuwa mbuzi wa kafara basi kieleweke ila ni mbaya kabisa
 
Huu ni mwaka wa kujikomboa kwa Madaktari na Waalimu. Serikali yenu imekuwa ikiwaadaa kwa muda mrefu sana. Sasa ni wakati wa kuichukulia hatua!


:bounce:! :bounce:
 
Walimu hatuwezi kugoma kabla Mukoba hajafungasha mikoba yake na kutuachia chama chetu, anawafanya walimu kama watoto wadogo anawaanda kwaajili ya mgomo wakisha kuwa tayali anasitisha mgomo kwa madai eti serikali inatimiza masharti walopewa, kumbe masharti yenyewe ni kukiuza chama. Sasa walimu tunaanza mgomo wa kumtoa Mkoba na katibu wake and then ndo tunaigomea serikali. TUMECHOKA KUPELEKWA PELEKWA
 
Tatizo la walimu ni waoga kama makondoo. Yaani tunapangana kabisa tugome, lakini mwisho wa siku tukitishiwa kidogo tu ndiyo tunaanza kukatishana tamaa. Hii sekta itabaki ya kimasikini daima kwa kuwa walimu hawana solidarity kabisa. Sasa mwaka ule mmeandaa kila kitu ilikuwaje muache mgomo eti kutokana na order ya mahakama? Who is mahakama bwana mbele ya kudai haki halali tuliyonyimwa for years?

mkuu sikiliza nikwambaie wengi wa waalim ambao wameshika nafasi za uongozi huko ct ni wa shule za msingi na hawa wana experience ya miaka kama 20 au 15 hivi. waalim hawa ni wake wa wakurugenzi, makatibu wakuu mameneja wa mashirika ya umma so wako na kuwasilikiza waume zao zaid. hawa wakitoka kwenye vikao huwa wanakwenda kuwaambia na waume zao wanakwenda kuyapresent hivyo tunakuja kuwa defeated baadae.

pia kuna kundi la waalim wa primary ambao ni waoaga na hasa ikitanguliwa na elim yao, matokeo yake ni kukwamisha kila kitu. baadhi ya waalim pia huwa wamefika kwa kuwa waalim so to them wanaresist kila kitu. wanhofia kukosa unga wa watoto.

but kuna kundi la vijana ambao wanajivunia elimu zao katika kiwango cha elim ya juu na hawa wako tayari kwa lolote but ni wachache sana uilinganisha na makundi mengine. so po ndipo penye tatizo but mm natangaza nia wazi ya kugoma hadi kieleweke juu ya waalim jamani hata teching allowance hatuna wala overtime lol!
 
mi nadhan wanaotakiwa kugoma kwa sasa ni wananchi!mbona walimu wapo ktk mgomo siku nyingi kama mnabisha chekini matokeo!walimu c kama madaktari ambao madhara ya mgomo ni hpo hpo,kwa wao impact ni kwa generation nzima ijayo!kiukwel ni bora mwanangu aende garage mapema kuliko shule ya kata coz walimu wapo ktk mgomo!
 
Amini usiamini taifa letu litapata mapinduzi ya kweli kama walimu hasa wa shule za msingi watatoka usingizini walimo sasa hivi. Hili ni kundi muhimu sana kwa mapinduzi ya kweli Tanzania
 
Jamani walimu wananyonywa kweli kwenye mishahara yaani degree holder anazidiwa na wa afya ambaye ana diploma.Walimu komaeni ndo mtapata haki zenu.
 
Waalimu mmepata div four zenu mkapewa kazi ili msife njaa bado mnalalamika. Ktk sekta inayoongoza kuwa na failure wengi ni ualimu. Mkifukuzwa ualimu mtaenda wapi? Wengine ni Waalimu UPE, nao wanadai fadhila. Kufundisha hamfundishi, mnadai maslahi. Gomeeni muone, tunawafuta kazi mkalime.
 
Siwaungi mkono kwani ualimu ni wito kwa sasa,we huoni wanaosomea ualimu ni waliofeli form4&6?hilo ni chaka la vilaza,tena hyo wanayolipwa ni nying sana ingepunguzwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom