CWT madai haya niyapeleke wapi?

DT125

JF-Expert Member
Oct 19, 2011
380
573
Naomba msaada wako Rais wangu wa CWT.
  1. Mie na walimu wenzangu wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro tuliopata likizo ya Juni mwaka huu hatujalipwa nauli ya likizo mpaka sasa, licha ya kuambiwa nauli hizo zilitoka na kuliwa. Katibu wa CWT wilaya analijuwa hili. Nisaidieni nipate pesa zangu.
  2. Nilipewa barua ya kupanda daraja baadae nikaambiwa imefutwa serikali haina fedha, Katibu wenu wa wilaya Mr. Maneno mengi analijuwa hili.
  3. Walibandika majina kwenye mbao za matangazo tunaositahili malipo mbalimbali ikiwa ni pamoja na uhamisho, matibabu, nk. lakini kila baada ya miezi sita au mwaka Katibu wenu wa Wilaya amekuwa anatuandikisha madeni upya.
  4. Tulihudhuria mafunzo ya sayansi (INSERT) mwezi Septemba mpaka leo hatujalipwa. Tukifuatilia tunaambiwa wakuu wakuu wa shule hawajalipa toka sehemu ya ada. Ukiuliza wakuu wetu wa shule wanadai ada wanatumia kununua chaki,kulipa walimu wanaojitolea kufundisha masomo ya sayansi na vitabu. Wanadai hawajapata fedha ya ruzuku toka serikali kwa mwezi wa Julai, Agosti, Septemba, Oktoba na Novemba. Licha ya kupata taarifa kuwa fedha toka TAMISEMI zimeshatumwa.

Tunaomba mtuondolee Katibu Wenu wa Wilaya, amekuwa ni kuwatisha wakuu wa idara husika na MKurugezi baadaye anapote kabisa.
 
Acha kulalamika na acha kupoteza muda na walafi tafuta njia mbadala ya kufika mbele lakn cha kwanza ilikuondoa mambo haya mabovu fundisha watoto kwa akili yako yote wampe maarifa wanayopaswa kupata ili wakati ujao wao ndio wataondoa haya na kuendelea kutowafundisha watoto ni kuendelea kudumisha tabaka hili linalopokezana kufanya haya maana watoto wao wengi hatunao shuleni kwetu. TAFUTA NJIA MBADALA ILA SIKUACHA KUFUNDISHA WATOTO
 
Back
Top Bottom