Kuna taarifa iliyoletwa humu toka kwa katibu mkuu utumishi kwenda kwa maafisa utumishi ikiwataka wafanye marekebisho ya barua walizonazo watumishi ambazo walikabidhiwa tangu mwaka 2016 baada ya kupanda madaraja na baadaye kusitishwa ili kupisha zoezi la kuwaondoa watumishi hewa n'a wale wenye vyeti feki. Zoezi lilifanyika n'a rais aliahidi wale wote wanaostahili kupanda watapandishwa mwezi huu wa novemba n'a kulipwa malimbikizo yao yote tangu tarehe za barua zao walizonazo miongoni. Sasa iweje barua iliyotumwa kwa maafisa utumishi ielekeze barua za watumishi zibadilishwe tarehe na zisomeke kuanzia mwedición novemba 2017 kwa maana ya kuwa fanyia watumishi wasilipwe malimbikizo yao. Kama kweli barua hii ni ya kweli tafadhali tucta na cwt simamieni hili ili kutetea haki zao watumishi haw. Inauma sana.