Cum cruce et gradio: Mfahamu Thomas Aquinnas moja kati ya watu wenye akili nyingi aliyewahi kuwepo

Ok hapo nimeelewa sasa kiongozi.. Nilijua nimuislam huyu mwamba
Jurjani anakupiga changa la macho...

Huyo Ibn Sina Alikuwa ni muislam...ila Hawa kina JURJANI ni miongoni mwa wale SIASA KALI...wanaoweza kumbrand yeyote kwa CHOCHOTE....na kumshambulia wasiyempenda na kumtaka...

Kwa mfano,hebu angalia anavyomkataa sheikh Hamza Yusuf Wa Zaytuna College kule California kuwa si ULAMAA(mwanazuoni,sheikh)...Yote hayo ni kwa kuwa Shaykh huyo ana mitazamo tofauti na EXTREMITIES walioko ndani ya WAISLAM....

Huyu Jurjani anaweza hata kukataa na kubishia UWEZO mkubwa aliopewa Thomas Aquinas na MWENYEZI MUNGU....

Jurjani hana jipya...nimeshajadiliana naye Katika FORUMS hizo na kumaizi kuwa ni MTU ANAYETAKA awafundishe na kuwaaminisha Wengine IMANI Yake kwa LAZIMA...

Jurjani hana kanuni njema za mijadala CONSTRUCTIVE zaidi ya ARGUMENTUM AD HOMINEM Katika yale ALIYOJILISHA NA KUJIAMINISHA....

Hapa mjadala wetu ni CHARISMATIC PHILOSOPHER Thomas Aquinas....
 
Unajua kuna muda kuacha upotevu unaenezwa ni tatizo kubwa sana. Kuna swali nimekuuliza umelikimbia. Hamza Yusuf ni Sufi na anawaita watu katika Usufi, yaani ni mzushi.

Uliza wanafunzi wakiingia katika madarsa katika chuo cha Zaytun wanafanya matendo gani ?

Yeye anasemaje kuhusu kuwafundisha watu somo la Itikadi ? Sasa sisi tunamkataa kwa upotofu wake na si dhati yake. Yaani anapingana na mafundisho sahihi ya Uislamu.

Tukirudi kwa Thomas,kwangu mimi huyu si mtu mwenye akili, sababu alikosa ala za kuujua ukweli kama walivyo kosa kina Aristoto, Plato na Wanafalsafa wengine.
Unaleta mjadala ndani ya mjadala....

Anzisha THREAD nitakuja na si hapa....

Sufi ni waislam...na wanafit kuwa ndani ya UISLAM kwa all proven criteria....

Kwako wewe...kamwe hawawezi kuwa ni waislam....ni sawa na ADVENTIST MSABATO kuwapinga Wengine kuwa si WAKRISTO,kwa Sababu tu ya kutofautiana Katika mitazamo na muktadha ya KIMAPOKEO.....

Muislam ni kila anayesema ALLAH ni Mwenyezi MUNGU Pekee na Muhammad kuwa mjumbe wake ALIEMTUMA...

Je Sufi hawaamini Katika NGUZO 5 za uislam?
Je Sufi hawaamini Katika NGUZO 6 za Imani?!!!!

Kama hawaamini hayo,basi kweli si WAISLAM...

Plz yajibu haya Katika thread yako...humu leo ni NGULI WA FIKRA Mtunduizi Thomas Aquinas.....
 
Suala la Thomas Aquinas kwa upande wangu nimelimaliza.

Pili, usiulize maswali ambayo hayahusiani na nililo kujengea hoja. Nani amesema masufi siyo Waislamu ? Labda kama unataka tuujadili Usufi kwa upana wake, ila ukiuangalia wanafanya uzushi ambao haupo katika dini.

Wako wengi wanamkiri Allah na mtume Muhammad lakini si Waislamu, mfano wao ni Mashia. Uislamu ni zaidi ya kukiri, bali kuyatendea kazi yale yote aloyo kuja nayo mtume wa Allah.

Tatu, siwezi kuanzisha mada ambayo nina uhakika kabisa mjadala wake hutauweza, kama wewe una muona Hamza Yusuf ni Ulamaa, vipi utauweza mjadala juu ya Usufi ?
 
Hebu fikiria kwa makini wala usiweke mawazo ya Karl Marx , "dini ni utumwa wa fikra " Fikiria Mungu kuandaa moto wa kuchoma viumbe vyake " fikiria mwafrika kuwakilisha nembo ya shetani. Unaishia kutishiwa ili ushike imani za kizungu. Kwa maendeleo poa sio kiimani

Sent from my TECNO-N2 using JamiiForums mobile app
 
Unajikanganya mwenyewe...

Ulisema Masufi si waislam.....na Shaykh Hamza Yusuf Si Ulamaa....

Unabadilisha gia angani eee?!!!

Ulamaa Ni mwanazuoni na mwanazuoni huwa ana TITLE ya Usheikh....

Kwa kuwa humkubali Thomas Aquinas,basi kwako pia si ULAMAA(mwanazuoni wa kikristo)?!!!!

Mzee MAJITAPO...hebu anzisha THREAD juu ya MASUFI uone Kama SITOUWEZA huo MJADALA usemao kuwa UTANISHINDA....
 
Ulisema Masufi si waislam.....na Shaykh Hamza Yusuf Si Ulamaa....
Unatakiwa uwe unatunza kumbukumbu, hakuna sehemu niliyosema Masufi si Waislamu, bali kuna sehemu niliyo sema Avecenna hakuwa Muislamu na kuna sehemu kadhalika nilisema Mashia siyo Waislamu. Sasa onyesha wapi nilisema Masufi siyo Waislamu ?
 
Tungekua tunaitafuta historia ya kina Chief mkwawa, Mwana malundi etc. Kama hivi tungekua mbali sana.
Shida kubwa ni kuwa wazee wetu hawakuwa na utamaduni wa kutunza kumbukumbu, haya mambo huenda kwa kurithishana.

Mfano mimi leo hii,nina utaratibu wa kuwa kila nikinunua kitabu lazima nikiandike vitu vifuatavyo :

1. Bei ya kitabu hicho
2. Siku niliyo nunua kitabu hicho
3. Tarehe ya Hijiriya na Miladia
4. Muda niliyo nunua kitabu hicho

Wenzetu hasa Waarabu wamejaaliwa Elimu ya nasaba, unakuta watu wana uwezo wa kukutajia nasaba yao mpaka mtu wa kumi au ishirini toka kwa babu yake. Lakini leo hii mchukue Mswahili au Mzungu mwambie akutajie watu kumi au watano toka kwa babu yake, hili huwa ni gumu mno.
 
P

Nini maana ya ulamaa kiongozi
Tamko Ulamaa lina asili ya Kiarabu, na mjengeko wake wa kisarufi una maana ya kuchuoa mpaka, yaani kama kitu kizuri basi ni kizuri sana,au kibaya basi ni kibaya sana au Muongo basi ni Muongo sana,katika Istilahi ya Nahau ya Kiarabu huingia katika kundi liitwalo "Ismul al Mubalagha". Tukirudi katika tamko "Ulamaa" ni mjuzi sana wa jambo fulani, na hasa hutumika katika Ulimwengu wa Dini, ya kuonyesha anayekusudiwa au kuegemezeaa sifa ni mjuzi sana wa jambo la Dini au Dini.

Lakini, kadhalika kuna sifa za Wanazuoni (Ulamaa).
 
Ukisoma falsafa za Karl max utaishia kuwehuka mkuu..sio mtu poa kabisa na imani yako. Inatakiwa uwe mkomavu kiimani kumsoma
Wakati fulani ukisoma falsafa za watu mbalimbali, kwa kawaida utapatwa na mvuto wa aina yake.

Kutegemea na maarifa, elimu na uelewa wa mambo alionao mtu utafahamu ukweli ni upi kati ya wanafalsafa wengi wanaosema.

Watu wote wanastahili na wanahaki ya kuheshimiwa kwasababu watu wote tuna hadhi sawa.

Lakini linapokuja suala la mawazo, mafundisho na mienendo yao, wengi wa hao wanafalsafa hawatusaidii na hawatufanyi sisi tunaokuja baada yao kuwa salama kiakili na kimaadili, kimwili na kiuchumi; maendeleo.
 

Similar Discussions

26 Reactions
Reply
Back
Top Bottom