Geza Ulole
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 59,163
- 79,320
Ndugu wana-JF
Nimejaribu kuskiiza hotuba ya Bwana Jussa (MB wa jimbo la Mji Mkongwe-Visiwani) na katika yoote aliyosema nimegundua kuna mapungufu yafuatayo haswa kwenye swala la mafuta! Sheria za kimataifa zinasema pwani inakuwa mali ya nchi kavu mpaka nautical miles 200 sasa tujiulize ukichukulia Pemba ambayo inasemekana pwani yake ya Mashariki ina mkondo wa mafuta kama anavyodai, ipo katika umbali gani toka pwani? Hebu tufikirie katika mazingira yaa Zanzibar na Tanganyika ni nchi mbili, Je hivi visiwa viwili vya Unguja na Pemba, je haviko ndani ya 200 nm za pwani ya Tanganyika (yaani overlapping the Tanganyika territorial waters)?
Wakati mwingine wanasiasa wanapenda siasa za kutia ujinga ulio na hamasa na ushawishi kwa wananchi wakiwa wanajua fika kwamba kuna masuala yenye utata na majibu yake ni mazungumzo na makubaliano kupitia wataalam maana haya masuala si mageni katika ulimwengu huu na hayajaanza leo na hapa nchini mwetu pekee! Japokuwa huyu Mh amemtukana Mh Sitta (mwenye umri kama wa babake) ila ukweli unabaki palepale kama leo hii visiwa vinajitenga bado tutagawana (formula ikitengenezwa na wataalam ikizingatia pia ratio division ya resources inayotokana na vitu kama urefu wa pwani baina ya nchi zijazo mbili yaani Tanganyika na Zanzibar) na hivi visiwa mafuta yale yatakayogunduliwa iwe ya kikombe cha chai au cha kahawa ya muuza kashata au upawa wa muuza mafuta ya kupikia maana swala hili si rahisi namna ile kama linavyoelezwa na Bw Jussa bali ni suala zito na lenye kizungumkuti mkuu (a very contentious issue)! Namuomba Bwana Jussa apitie shared transboundary resources kama zile kati ya UK na Norway aone jinsi wataalam walivyokaa na kuandika formula ya kushiriki katika kula matunda ya mafuta yale! Asijidanganye ati yale ni mafuta ya Zanzibar (Waunguja na Wapemba) pekee bali yale ni mafuta ya hata Tanganyika (Wabara) maana visiwa hivi viwili vipo ndani ya nautical miles 200 zinazoongelewa na International laws of the Sea under special economic zones.
Namshauri huyu jamaa aache kuwatia ujinga ama ujuha ama sintofahamu Wazanzibari wenzie na zile siasa za "chao ni chetu ila chetu si chao" maana mwisho wa siku itikadi hizi za kiradikali zitaleta vurugu toka kwa Watu wa Zanzibar kwa kutotambua ukweli ni upi baada ya kujazwa upuuzi wa propaganda! Ni haya tu ningependa wana JF tujue na tuwe macho na siasa za chokochoko na zenye kuleta jazba, ushabiki na uzandiki usio na punje ya akili bali ujuha mtupu!
MY TAKE
Naona hii habari inahusiana na hii topic tunaona hapa mama Tibaijuka ameenda kuomba mile 150 za ziada hii itafanya mile 350 toka pwani ya Tanzania kuwa chini ya Mamlaka ya JMT! Natumai Jussa anaona haya! Na ningependa ajibu kitu humu ndani kama ana hoja za maana tumjibu
17th January 12
Tanzania kuwasilisha ombi UN kuongezewa eneo la bahari
Muhibu Said
Tanzania imetangaza kuwasilisha maombi Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa (UN), jijini New York, nchini Marekani, kudai umiliki wa eneo la ziada nje ya maili 200 za Ukanda wa Kiuchumi Baharini (EEZ) katika Bahari Kuu ya Hindi, ili iweze kulifanyia utafiti zaidi kuhusu rasilimali zilizoko chini ya bahari kwa lengo la kuinua uchumi wa nchi.
Kwa mujibu wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, rasilimali hizo ni pamoja na mafuta, gesi na madini.
Eneo hilo linatokana na ongezeko lingine tena maili 150 na hivyo kufanya jumla ya mpaka hadi maili 350, ambazo ni sawa na kilomita 560 kutoka kwenye ‘baseline'.
Waziri Tibaijuka alisema maombi hayo yanatarajiwa kupelekwa na jopo la wataalamu kutoka Tanzania Bara na Zanzibar na wajumbe wawili kutoka Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, litaongozwa na Waziri Tibaijuka.
Alisema wanatarajia kuwasilisha andiko la utafiti wa kisayansi la kudai eneo hilo katika Shirika la UN Linaloshughilikia Mikataba Sheria za Baharini (UNCLOS) kesho na kwamba, baadaye Aprili, mwaka huu, watakwenda tena UN kutetea andiko hilo.
Alisema baada ya kutetea andiko hilo huko UN, Kamisheni ya Masuala ya Baharini itafanya uamuzi kuhusu maombi yao na kwamba, anaamini hatua waliyoifikia watafanikiwa.
Waziri Tibaijuka alisema kazi ya kukamilisha andiko hilo iliyoanza mwaka 2007 na kugharimu zaidi ya Sh. bilioni 5.2, imesimamiwa na wizara yake na tafiti zimefanyika kwa kutumia wataalamu kutoka sekta za ardhi, maji, mawasiliano, sayansi na teknolojia, sheria na wataalamu wa masuala ya baharini kutoka vyuo vikuu.
NIPASHE
http://www.ippmedia.com/frontend/functions/print_article.php?l=37564
http://www.thecitizen.co.tz/news/-/19231-tibaijuka-rep-is-mistaken
Nimejaribu kuskiiza hotuba ya Bwana Jussa (MB wa jimbo la Mji Mkongwe-Visiwani) na katika yoote aliyosema nimegundua kuna mapungufu yafuatayo haswa kwenye swala la mafuta! Sheria za kimataifa zinasema pwani inakuwa mali ya nchi kavu mpaka nautical miles 200 sasa tujiulize ukichukulia Pemba ambayo inasemekana pwani yake ya Mashariki ina mkondo wa mafuta kama anavyodai, ipo katika umbali gani toka pwani? Hebu tufikirie katika mazingira yaa Zanzibar na Tanganyika ni nchi mbili, Je hivi visiwa viwili vya Unguja na Pemba, je haviko ndani ya 200 nm za pwani ya Tanganyika (yaani overlapping the Tanganyika territorial waters)?
Wakati mwingine wanasiasa wanapenda siasa za kutia ujinga ulio na hamasa na ushawishi kwa wananchi wakiwa wanajua fika kwamba kuna masuala yenye utata na majibu yake ni mazungumzo na makubaliano kupitia wataalam maana haya masuala si mageni katika ulimwengu huu na hayajaanza leo na hapa nchini mwetu pekee! Japokuwa huyu Mh amemtukana Mh Sitta (mwenye umri kama wa babake) ila ukweli unabaki palepale kama leo hii visiwa vinajitenga bado tutagawana (formula ikitengenezwa na wataalam ikizingatia pia ratio division ya resources inayotokana na vitu kama urefu wa pwani baina ya nchi zijazo mbili yaani Tanganyika na Zanzibar) na hivi visiwa mafuta yale yatakayogunduliwa iwe ya kikombe cha chai au cha kahawa ya muuza kashata au upawa wa muuza mafuta ya kupikia maana swala hili si rahisi namna ile kama linavyoelezwa na Bw Jussa bali ni suala zito na lenye kizungumkuti mkuu (a very contentious issue)! Namuomba Bwana Jussa apitie shared transboundary resources kama zile kati ya UK na Norway aone jinsi wataalam walivyokaa na kuandika formula ya kushiriki katika kula matunda ya mafuta yale! Asijidanganye ati yale ni mafuta ya Zanzibar (Waunguja na Wapemba) pekee bali yale ni mafuta ya hata Tanganyika (Wabara) maana visiwa hivi viwili vipo ndani ya nautical miles 200 zinazoongelewa na International laws of the Sea under special economic zones.
Namshauri huyu jamaa aache kuwatia ujinga ama ujuha ama sintofahamu Wazanzibari wenzie na zile siasa za "chao ni chetu ila chetu si chao" maana mwisho wa siku itikadi hizi za kiradikali zitaleta vurugu toka kwa Watu wa Zanzibar kwa kutotambua ukweli ni upi baada ya kujazwa upuuzi wa propaganda! Ni haya tu ningependa wana JF tujue na tuwe macho na siasa za chokochoko na zenye kuleta jazba, ushabiki na uzandiki usio na punje ya akili bali ujuha mtupu!
MY TAKE
Naona hii habari inahusiana na hii topic tunaona hapa mama Tibaijuka ameenda kuomba mile 150 za ziada hii itafanya mile 350 toka pwani ya Tanzania kuwa chini ya Mamlaka ya JMT! Natumai Jussa anaona haya! Na ningependa ajibu kitu humu ndani kama ana hoja za maana tumjibu
17th January 12
Tanzania kuwasilisha ombi UN kuongezewa eneo la bahari
Muhibu Said
Tanzania imetangaza kuwasilisha maombi Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa (UN), jijini New York, nchini Marekani, kudai umiliki wa eneo la ziada nje ya maili 200 za Ukanda wa Kiuchumi Baharini (EEZ) katika Bahari Kuu ya Hindi, ili iweze kulifanyia utafiti zaidi kuhusu rasilimali zilizoko chini ya bahari kwa lengo la kuinua uchumi wa nchi.
Kwa mujibu wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, rasilimali hizo ni pamoja na mafuta, gesi na madini.
Eneo hilo linatokana na ongezeko lingine tena maili 150 na hivyo kufanya jumla ya mpaka hadi maili 350, ambazo ni sawa na kilomita 560 kutoka kwenye ‘baseline'.
Waziri Tibaijuka alisema maombi hayo yanatarajiwa kupelekwa na jopo la wataalamu kutoka Tanzania Bara na Zanzibar na wajumbe wawili kutoka Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, litaongozwa na Waziri Tibaijuka.
Alisema wanatarajia kuwasilisha andiko la utafiti wa kisayansi la kudai eneo hilo katika Shirika la UN Linaloshughilikia Mikataba Sheria za Baharini (UNCLOS) kesho na kwamba, baadaye Aprili, mwaka huu, watakwenda tena UN kutetea andiko hilo.
Alisema baada ya kutetea andiko hilo huko UN, Kamisheni ya Masuala ya Baharini itafanya uamuzi kuhusu maombi yao na kwamba, anaamini hatua waliyoifikia watafanikiwa.
Waziri Tibaijuka alisema kazi ya kukamilisha andiko hilo iliyoanza mwaka 2007 na kugharimu zaidi ya Sh. bilioni 5.2, imesimamiwa na wizara yake na tafiti zimefanyika kwa kutumia wataalamu kutoka sekta za ardhi, maji, mawasiliano, sayansi na teknolojia, sheria na wataalamu wa masuala ya baharini kutoka vyuo vikuu.
NIPASHE
http://www.ippmedia.com/frontend/functions/print_article.php?l=37564
Tibaijuka: Rep is mistaken |