nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
*Wabunge sita watua Igunga kuongeza nguvu
Na Peter Mwenda, Igunga
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimekionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuacha mara moja kutangaza
kudanganya wananchi wa Jimbo la Igunga kuwa chama hicho kisipewe kura kwa madai kuwa ni CCM-B.
Akizungumza katika mkutano wa kampeni ya uchaguzi mdogo Jimbo la Igunga juzi, Kaimu Katibu Mkuu wa CUF-Bara, Bw. Julius Mtatizo alisema CHADEMA imekuwa ikiwadanganya wananchi kuwa CUF ni CCM-B, wasikichague kwa sababu hakitaleta maendeleo jambo ambalo ni udanganyifu ambao unastahili adhabu.
Alisema CUF imevumilia sana kauli hizo na sasa imefika kikomo, hivyo kilichobaki ni wao kuweka hadharani mabaya ya CHADEMA kwa sababu ya upotoshaji huo kwa wapiga kura wa Igunga.
Bw. Mtatiro alisema cha kushangaza, ni kwa nini CHADEMA iseme uongo wakati CUF haijawahi kusema mtindo wa uongozi wa upendeleo uliopo katika chama hicho, ambao hauna tofauti na yale yanayofanywa na chama tawala CCM.
"Mfumo wa uongozi wa CHADEMA hauna tofauti na ule wa CCM kwa sababu ule mfumo wa uongozi wa kupeana ulipo CCM ambao hautawahi kutokea CUF," alisema Bw. Mtatiro.
Alisema CHADEMA ilipata viti maalumu 36 na kushindwa kugawa kwa kuzingatia uwakilishi wa wananchi, bali walipendeleana wao kwa wao kwa kugawa viti 16 kwa mkoa wa Kilimanjaro pekee ambako viongozi wa chama hicho, walitoa kwa wake zao, wadogo zao na jamaa zao.
Alisema CUF Tanzania bara na Zanzibar walipata viti maalum kumi ambavyo ilivigawa bila upendeleo Dodoma (Bi. Moza Abeid), Mwanza (Bi. Mkiwa Kimwanga , Tanga Bi, Amina Mwidau, Mtwara (Bi. Clara Mwatuka, Kaskazini Pemba (Bi. Riziki Omar Juma), Mjini Magharibi Bi. Amina Amour na Kusini Magharibi (Bi. Thuwaiba Idris) ambao wanakilisha wa wananchi badala ya kulimbikizia kundi chache.
Alisema suala la Serikali ya Umoja Zanzibar ni mfumo uliofikiwa na Wazinzibari wenyewe ili kuondoa uhasama uliokuwepo, sasa inakuaje CHADEMA iseme CUF imeingia mkataba wa urafiki na CCM.
Wabunge waongeza nguvu
Wabunge sita wa CUF kutoka Zanzibar waliokuwa katika msiba wa meli ya M.V Spice Islanders wamewasili Igunga kuanza kampeni za kumnadi mgombea wa chama hicho, Bw. Leopold Mahona.
Wakitambulishwa katika mkutano wa kampeni uliofanyika Kata ya Nanga juzi jioni, Kaimu Katibu Mkuu wa CUF Bara, Bw. Julius Mtatiro alisema pamoja kuwa msiba huo ni mkubwa na umegusa familia za wabunge hao, wamekuja kuongeza nguvu kuhakikisha chama hicho kinachukua kiti.
Waliotambulishwa ni Mbunge wa Nungwi ambako meli hiyo ilizama, Bw. Yusuf Haji Khamis, Bw. Rashid Ali Omar (Kojani), Mohamed Habib Mnyaa (Mkanyageni), Haroub Mohamed Shamis (Chonga), Bw. Salim Hemed Khamis (Chambani).
Katika mkutano huo mgombea ubunge wa CUF, Bw. Leopold Mahona alisema akichaguliwa atahakikisha wananchi wa Kata hiyo wataondokewa na kero zinazowasumbua kwa miaka mingi bila kupatiwa ufumbuzi