Kufuatia kuibuka kwa ushindani wa vyama vya siasa nchini mara baada ya uchaguzi mkuu wa 2010 sasa chama cha wananchi CUF kimejipanga kurudi kwenye siasa za mapambano maarufu kama "harakati". Hayo yalisemwa jana katika uwanja wa Zakhiem uliopo eneo la Mbagala jijini Dar es salaam wakati chama hiko kilipompokea Bw Philipo ambaye amehamia kwenye chama hiko akitokea CCM.
Akizungumza kwa ukakamavu mkubwa na sauti ya kiharakati Naibu katibu mkuu bara wa CUF Bw Julius Mtatiro amenukuliwa akisema "Suluhisho la matatizo yetu watanzania ni kuing'oa CCM immediately" huku akishangiliwa na umati uliokusanyika uwanjani hapo katika mkutano huo ulioanza majira ya saa nane mpaka saa kumi na mbili jioni.
Katika mkutano huo CUF imetangaza maazimio kadhaa ikiwa ni pamoja na kuwania kiti cha ubunge katika jimbo la Igunga , sambamba na hilo pia chama hiko kimelitangaza rasmi jarida lake linalokwenda kwa jina la "Mwana Harakati"
www.novakambota.com