CUF yaandaa mgomo Zanzibara!

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
CUF yaandaa mgomo dhidi ya bidhaa za BOPAR




Na Ali Suleiman, Zanzibar

CHAMA cha CUF kimesema kitaitisha mgomo Unguja na Pemba kuwataka wananchi kususia mchele unaoagizwa na kampuni ya BOPAR Enterprises baada ya kubainika kwamba ni mbovu.

Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF, Bw. Salim Bimani, alisema jana kwamba mchele unaoagizwa na kampuni hiyo ni mbovu na haufai kwa matumizi ya binadamu, na kudai kuwa Serikali inamlinda mfanyabiashara huyo.

"Tunaunga mkono juhudi za Mwakilishi wetu Shaali, kufichua uoza na kusema ukweli kuhusu mchele...ingawa ukweli huo Serikali haiutaki...tunakusudia kuitisha mgomo kuwataka wananchi wasinunue mchele wa BOPA," alisema Bw. Bimani.

Alisema wananchi wa Zanzibar wamechoka kulishwa vyakula vibovu ambayo vinahatarisha afya zao, kwani baadhi ya wagonjwa kutoka Zanzibar wanaotibiwa katika hospitali ya saratani Ocean Road, Dar es Salaam, wanakabiliwa na matatizo hayo.

"Saratani kwa asilimia kubwa inatokana na watu kula vyakula vibovu ambavyo havifai kwa matumizi ya binadamu, sasa sisi tunataka kulishughulikia tatizo hili kwa kulikomesha moja kwa moja," alisema Bw. Bimani.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) juzi ilitoa taarifa kuhusu mchele mbovu uliozusha malalamiko kwa wajumbe wengi wa Baraza hilo, ambapo ripoti yake haielezi hali halisi ya mchele huo unaolalamikiwa.

Lakini taarifa hiyo ilisema inakusudia kuwachukulia hatua kali baadhi ya watendaji wa taasisi zinazojishughulisha na vyakula kikiwamo kitengo cha kumlinda mlaji kwa kutokuwa makini katika kushughulikia tatizo hilo.

Akichangia taarifa hiyo, Mwakilishi wa CUF, Bw. Haji Faki Shaali, alisema Serikali inamlinda mfanyabiashara huyo, ambaye amekuwa akifadhili CCM.

Madai hayo yalipingwa na baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na kutakiwa Mwakilishi huyo, kutoa ushahidi wake au kuomba radhi, ambapo yeye alisema hatafanya hivyo.

Sakata la Mwakilishi wa CUF kwa sasa limepelekwa kwa Kamati ya Maadili na Kinga ya Baraza la Wawakilishi, ambayo itafanya uchunguzi wa suala hilo pamoja na mwakilishi kuwasilisha ushahidi wake.

Hatima ya Mwakilishi Shaali itajulikana mwakani, ambapo Mkutano wa Baraza la Wawakilishi utapokea ripoti na taarifa ya Kamati hiyo.


source majira
 
Ingia kwa majina yako mengine yote matatu ili at least hii thread yako ionekane imewekwa na mtu mwenye kufikiri kidogo, kisha Kada naye atakusapoti na majina yake pia
 
Ingia kwa majina yako mengine yote matatu ili at least hii thread yako ionekane imewekwa na mtu mwenye kufikiri kidogo, kisha Kada naye atakusapoti na majina yake pia

shalom si bure iko namna? hivi una hakika kama mie nnaingia kwa majina matatu? au mkuu umenipenda mie dume mwenzio hata hivyo ss watu wa zenji njoo unipm tuongee.

maana hili umelioshikia bango, nnaomba maadmin wamsaidie kuhusu mie nimeruhusu admin mujuilishe hili jee mie nna majina mangapi? na ukijua usione tabu kuusema ukweli.
 
Kwi kwi kwiiii Yupo wapi Semvulachole jamani na miss michango yake kwi kwi kwi kwi kwiiiiiii
 
shalom si bure iko namna? hivi una hakika kama mie nnaingia kwa majina matatu? au mkuu umenipenda mie dume mwenzio hata hivyo ss watu wa zenji njoo unipm tuongee.

maana hili umelioshikia bango, nnaomba maadmin wamsaidie kuhusu mie nimeruhusu admin mujuilishe hili jee mie nna majina mangapi? na ukijua usione tabu kuusema ukweli.

Mtu wa Beach,

You know for sure thats not how we operate. Admin hawezi kujihusisha na tuhuma kama hizo!
 
sasa tusaidie vp tumridhishe huyu ndugu yetu na mie kuwa safe na tuhuma zake?
 
sasa tusaidie vp tumridhishe huyu ndugu yetu na mie kuwa safe na tuhuma zake?

SIo lazima mkuu kujihusisha na tuhuma zake kama utaachana naye atajiona ********* then ataacha lakini kama unajibizana nae utakuwa unaumia tuu. Wewe kata issue kwani hata ukiwa na majina kumi yanasaidia nini? Modes hawawezi kutoa details zako kisa unatuhumuwa kuwa unajiita kwa majina tofauti.
 
SIo lazima mkuu kujihusisha na tuhuma zake kama utaachana naye atajiona ********* then ataacha lakini kama unajibizana nae utakuwa unaumia tuu. Wewe kata issue kwani hata ukiwa na majina kumi yanasaidia nini? Modes hawawezi kutoa details zako kisa unatuhumuwa kuwa unajiita kwa majina tofauti.

ahsante sana kwa ushauri wako
 
uongo upi huo? mie nimeuliza kuwa sijaona rambi rambi zao? kuuliza ni kusema uongo?

wamethibitisha kuwa wanawake sio kama chama, wakati CUF ni chama na zimetumwa na mwenyekiti wao.

saawa nimeona au kulikoni?
 
uongo upi huo? mie nimeuliza kuwa sijaona rambi rambi zao? kuuliza ni kusema uongo?

wamethibitisha kuwa wanawake sio kama chama, wakati CUF ni chama na zimetumwa na mwenyekiti wao.

saawa nimeona au kulikoni?

fanya utafiti kabla hujauliza,.
umetuhumu wala hujauliza ndugu,angalia hiyo meli uliopanda itakupeleka pabaya.,ogopa kuongopa katika jamii,.
 
sasa kuhusu huu mgumo ambao unataka kuandaliwa na cuf mnauangaliaje? hapa ndio topic tunayoongelea na sio mimi kama mimi laa unataka kuhusu mimi anzisha na mimi nipo ntachangia
 
uongo upi huo? mie nimeuliza kuwa sijaona rambi rambi zao? kuuliza ni kusema uongo?

wamethibitisha kuwa wanawake sio kama chama, wakati CUF ni chama na zimetumwa na mwenyekiti wao.

saawa nimeona au kulikoni?

Hivi hapa umeuliza au umetuhumu?
Haya hapa ni maneno yako mwenyewe:

"sijaona salam za rambi rambi za chama makini juu ya huu msiba kama chama, jee ndio hauwahusu? ndio mafisadi hawastahiki kupewa mkono wa pole?"
 
sasa kuhusu huu mgumo ambao unataka kuandaliwa na cuf mnauangaliaje? hapa ndio topic tunayoongelea na sio mimi kama mimi laa unataka kuhusu mimi anzisha na mimi nipo ntachangia

usilie sana,
huo mgomo tunauunga mkono,ufanyike tu,kwani CUF migomo hawajaianza leo,wao waendelee tu na mgomo,tunaunga mkono.
 
Nadhani suala hapa si manufaa kwao,na hili sio suala la CUF,ni suala la wananchi,kama serikali yenyewe imethibitisha kuwa huo mchele haufai,basi ni haki ya wananchi kuukataa na ikibidi kulishtaki hilo kampuni linaloingiza mchele mbovu.Hilo ni suala la afya za watu wala sio manufaa.
 
uongo upi huo? mie nimeuliza kuwa sijaona rambi rambi zao? kuuliza ni kusema uongo?

wamethibitisha kuwa wanawake sio kama chama, wakati CUF ni chama na zimetumwa na mwenyekiti wao.

saawa nimeona au kulikoni?

Unaona ulivyo na majibu yakizembe zembe. halafu kweli watu wanakutetea. Tumia basi majina yako kaka hii thread inoge.
 
sasa kuhusu huu mgumo ambao unataka kuandaliwa na cuf mnauangaliaje? hapa ndio topic tunayoongelea na sio mimi kama mimi laa unataka kuhusu mimi anzisha na mimi nipo ntachangia

kwa majina yako yote au hilo la mtu wa pwani tu...mdebwedo!
 
Back
Top Bottom