CUF wamtega Kikwete: "Asimamie mazungumzo ya muafaka"

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Chama cha Wananchi CUF kimesema kiko tayari kurejea kwenye mazungumzo ya muafaka na Chama cha Mapinduzi endapo mazungumzo hayo sasa yataongozwa na Rais Kikwete mwenyewe kama Mwenyekiti. Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba amesema leo kuwa kwa vile kamati zilizoundwa kushiriki mazungumzo hayo zimemaliza kazi zake, na kutokana utata uliotokea baada ya maamuzi ya Butiama basi ipo haja ya mazungumzo hayo kufanywa na viongozi wa juu.

Uamuzi wa CUF amesema umezingatia kuwa ni yeye Rais Kikwete aliyeahidi kutafutia ufumbuzi mpasuko wa kisiasa uliodumu visiwani Zanzibar kwa muda mrefu sasa.

Hadi sasa hivi haijajulikana kama Rais Kikwete atakuwa tayari kusimamia mazungumzo hayo yeye mwenyewe hasa baada ya wale waliotakiwa kufanya hivyo kuonekana kushindwa au kutokuwa na nguvu ya kufikia muafaka wa kweli.

Hivi karibuni Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM inatarajia kufanya kikao chake maalum kusimamia ile "agenda ya siri". Rais Kikwete amemaliza ziara yake ya siku sita mkoani Singida muda mfupi uliopita.
 
Kweli CUF iko akili nimewakubali sasa .Now JK show uongozi wako kama Rais na Mwenyekiti wa Chama chako .Maana Makamba hana nguvu ndani ya CCM sasa JK ingia mwenyewe .
 
Hadi sasa hivi haijajulikana kama Rais Kikwete atakuwa tayari kusimamia mazungumzo hayo yeye mwenyewe hasa baada ya wale waliotakiwa kufanya hivyo kuonekana kushindwa au kutokuwa na nguvu ya kufikia muafaka wa kweli.QUOTE]

Kwa hili mimi napenda kuwapongeza CUF kwa uamuzi wao na ombi lao. Ni sahihi kabisa kwa Mh. Kikwete akiwa kama ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na Kiongozi Mkuu wa dola, kulitia mkono mwenyewe jambo hili na kuhakikisha kuwa linafikia hatima yake kwa mintarafu ya kuliweka pema Taifa letu pamoja na kizazi kijacho.
 
Nina wasi wasi na uwezo wa JK kwa maswala kama haya pamoja na kuwa mshika dola na kila kitu .Kabla ya kuanza kukata tamaa wacha nimpe muda nione atasemaje .Anaweza kukubalia mwaka 2009 siku chache kabla ya uchaguzi .CUF kaeni macho CCM wanaongea huku wanatafuta namna ya kuwashinda huko Zenji.
 
Tehe Tehe hapo Kikwete haendi, aliyoyaona Butiama yanamtosha, si mmesikia kwamba kule Butiama Karume alilia?
 
Interesting!!!
Naona Cuf wameraise the wager....Ambacho sijaelewa CUF wanataka Rais aache shughuli zake za kila siku za maendeleo(kama zipo na anazifanya) akasimamie mkutano wa muafaka ambao hatujui utaisha lini? I wouldn't be surprised kama Kikwete akisema No!!!
 
Ila Ccm Wao Ndiyo Waliomfanya Kiongozi Wao Aonekane Zero Why Ile Ndiyo Ilikuwa Karata Ya Jk Kwanza Kwa Yeye Tu Kukubali Kwamba Zenji Kunawaka Moto Na Kwa Kujiamini Kwa Kutosha Akifungua Bunge Akasema Atalishugulikia Swala,sasa Naye Sidhani Kama Alikuwa Na Strateges Za Kulingiza Kule Butiama Au Alizani Itakuwa Zidumu Fikra Sahihi Za Chairman,sasa Wamemkaanga Mwenzao Sasa Ni Mwanasesere Naye Alitakiwa Awatishie Kwamba Hili Ni Swala Langu Likishindikana Basi Najiuzuru Lazima Uwe Na Ajenda Ya Kufa Na Kuzikana Kama Mwana Siasa Lisipo Tekelezwa Hili Mimi Basi,uliona Mwalimu Aliwambia 1995 Kama Sigwemisi Asipo Jitoa Mimi Ccm Basi Jamaa Waka Gwaya.
 
Hivi kuna ugumu gani wa kuwachukua hawa jamaa na kuwafungia Ngurdoto kwa wiki nzima na hawatoki huko hadi mambo yote yatengemae? Ninaamiini Rais anaweza kutumia wiki nzima kukaa na kutafutia muafaka suala la Zanzibar kuliko kutumia wiki mbili kwenye ughaibuni katika ziara zake za Kivasco.
 
Interesting!!!
Naona Cuf wameraise the wager....Ambacho sijaelewa CUF wanataka Rais aache shughuli zake za kila siku za maendeleo(kama zipo na anazifanya) akasimamie mkutano wa muafaka ambao hatujui utaisha lini? I wouldn't be surprised kama Kikwete akisema No!!!

NI BONGE LA MTEGO UNAJUA NINI SASA AKIKUBALI ITABIDI AFANYE FASTA ILI AWAHI TRIP ZA MAJUU KWENDA SHOPING MAMTONI.ZAIDI APO MWANANGU KULONDA KAZI YA JESHI LAZIMA UGANGAMALE,MWANA KULONDA MPUNGA MCHELE,LAMKA KWENDA KUGUNDA.MAMBO YAMEBADILIKA JAMAA ALISEMA SIKUMOJA NI USHINDI TU UNAVAA SUTI UNACHUKUA NCHI SASA TEHEE TEHEE,NA HAO WATOO WANAWAPELEKA WAPI KUZOMEWA KWAMBA BABA YAKO HAKUWA NA LEGAS WEWE WAJA FANYA NINI
 
Hivi kuna ugumu gani wa kuwachukua hawa jamaa na kuwafungia Ngurdoto kwa wiki nzima na hawatoki huko hadi mambo yote yatengemae? Ninaamiini Rais anaweza kutumia wiki nzima kukaa na kutafutia muafaka suala la Zanzibar kuliko kutumia wiki mbili kwenye ughaibuni katika ziara zake za Kivasco.

Mkuu Mwanakijiji,

Hivi serikali haiwezi hata kuangalia JF na kuomba msaada wa mawazo kwani nafikiri kuna watu hapa wanaweza kuwakalisha CCM na CUF na kutazama hili jambo la mwafaka.

Je una mawazo gani?
 
kazi ipo, mwaka huu mkwere ataota kipara!

Mimi sioni maana ya hii kamati ya muafaka, maana kundi kubwa la wana-CCM hususani wale wa-znz hawahafiki suala la mseto (na hii ndio agenda kuu ya kamati hii), kila litakapo pelekwa kwenye "kamati kuu" ya CCM, wana-znz wanajifanya kulia ... eti hakutakuwa na maana tena ya mapinduzi!!
 
Offcouse Hizi Ndiyo Kazi Za Raisi Wala Si Kwenda Huko,how Comes Kwako Hakunogi Unakwenda Kwa Mwenzio,mimi Nilishangaa Walipo Mwita Mkapa Kuwa One Of Fasilitors Wa Kenya Issues Ooh Kimbo Kyandesi Mr Naked Is Going To Teach Naked People How To Dress,hata Mungwana Naye Atumie Sasa Fomulaye Ya Kenya Uliona Makidai Ya Press Confress Pale Airport Ndiyo Aende Nguru Doto Siku 7 Zinatosha
 
kazi ipo, mwaka huu mkwere ataota kipara!

Mimi sioni maana ya hii kamati ya muafaka, maana kundi kubwa la wana-CCM hususani wale wa-znz hawahafiki suala la mseto (na hii ndio agenda kuu ya kamati hii), kila litakapo pelekwa kwenye "kamati kuu" ya CCM, wana-znz wanajifanya kulia ... eti hakutakuwa na maana tena ya mapinduzi!!

Mimi nafikiri hata huu mseto ni kupotezeana muda tu.


Pia kuna masuala mawili makuu ambayo kama yakizungumzwa basi kidogo patakuwa na maelewano.

1. Suala la kamati ya uchaguzi. Hii ni lazima iwe ni kamati pekee isiyo na nyizi zozote zinazoning'nia kutoka serikalini na CCM. Iwe na kamati yenye watu mbalimbali wanaoteuliwa na vyama vyote vya upinzani katika Tanzania na wanalipwa na fungu maalumu lililotengwa na vyama hivyo.

Kamati hii inakuwa hai pale kunapokuwa na uchaguzi tu, na baada ya uchaguzi inavunjwa.

2. Ni "register" ya kudumu la wapiga kura lenye picha na alama za vidole za wananchi wote wenye umri wa kupiga kura.
Hapa tena wawakilishi wa vyama vyote vya siasa watasimamia zoezi zima la utayarishaji wa register hii na itakuwa ni mwisho wa register ambazo zimewahi kuwepo katika historia ya Tanzania.

Hii "register" si kwa Zanzibar tu bali kwa Tanzania nzima.

Nafikiri haya mambo mawili yakiwa ya kwanza kutatuliwa ndio yafuate mengine.

Haya ndio maoni yangu.
 
Interesting!!!
Naona Cuf wameraise the wager....Ambacho sijaelewa CUF wanataka Rais aache shughuli zake za kila siku za maendeleo(kama zipo na anazifanya) akasimamie mkutano wa muafaka ambao hatujui utaisha lini? I wouldn't be surprised kama Kikwete akisema No!!!

kwa nini aseme NO?
Mbona alipanda ndege na kwenda mpaka marekani kwenda kuzungumzia ule ambao wenyewe wanauita mgogoro wa zimbabwe ile hali hata matokeo ya uchaguzi yalikuwa hayajatangazwa?
na mbona aliweza kuvuka mpaka kuingia kenya na kwenda kusisitiza suluhu ipatikane kwa nini ashindwe hapa kwake ambako anaweza kwenda hata kwa boti?
maandiko yanasema "ondoa kwanza boriti lililopo jichoni mwako ndipo utoe kibanzi kilichopo kwenye jicho la mwenzako".
 
kwa nini aseme NO?
.
KWA KWELI SIONI HAPO MUGWANA AKIINGIZA VIATU VYAKE WAKATI WENNYE MUAFAKA HAWATAKI,KULA YA MAONI MEANS NO MUAKAKA SASA MUNGWANA SASA KESHAANZA JUA HATA KIDOGO HANA HESHIMA CCM, ATASEMA NO,WEWE SIKIZA TU MR POROJO MAKAMBA ATATOA.
 
ni miezi takriban mitatu tu ya mtafaruku kenya imepata muafa na utulivu umerudi sasa wanajipanga na kuanza kuinua uchumi.
sasa ndugu zangu hawa toka mwaka 1995 wao wananung'unikia matokeo kisha uchaguzi ukija wananyamaza, wakishindwa wanaamka tena sasa kweli hapo kuna wapinzani jamani?...mi nawapa tu ushauri, watazame ni mbinu gani ametumia Raila na ODM pentagon kuhakikisha wanagawana madaraka na kibaki, kisha na wao waitumie hiyo hiyo.
 
Huyu msanii anaweza kusimamia chochote kile kikawa na mafanikio? Chama chake kimemshinda, serikali imemshinda sasa Watanzania wameanza kugundua makosa makubwa ya kumchagua kama Rais. Chama kinaenda alijojo na serikali inaenda alijojo lakini yeye kama kapteni bado anafanya usanii tu. Sidhani kama kutakuwa na mafanikio yoyote hata yeye akisimamia mazungumzo hayo. La kuvunda....
 
Ni nani aliyekuwa amejitoa ktk muafaka jamani? CCM au CUF? Mnawapa masifa yasiyowastahili hawa jamaa!! JK aaache mambo makubwa ya nchi aende akashughulikie muafaka ? Muafaka wa nini? Kwani kuna watu bado wako Shimoni au? JK komaa na mambo muhimu siasa za Wapemba na Waunguja Mkapa alizimaliza 2001 . Ni nani aliyechinja askari tena tokea 2001? Visima vina kinyesi kama 2001? Hata maalim sasa kanyoa madevu. Muafaka wa nini?
 
Back
Top Bottom